< Genesis 21 >
1 Now the LORD attended to Sarah as He had said, and the LORD did for Sarah what He had promised.
Yahwe akamsikiliza Sara kwa umakini kama alivyo kuwa amemwambia, Yahwe akamfanyia Sara kama alivyo kuwa amemwahidi.
2 So Sarah conceived and bore a son to Abraham in his old age, at the very time God had promised.
Sara akachukua mimba na akamzalia Abraham mtoto wa kiume katika uzee wake, katika muda ule ule ambao Mungu alikuwa amemwambia.
3 And Abraham gave the name Isaac to the son Sarah bore to him.
Abraham akamwita jina mwanawe, ambaye alizaliwa kwake, na Sara, Isaka.
4 When his son Isaac was eight days old, Abraham circumcised him, as God had commanded him.
Abraham akamtahiri mwanawe Isaka alipofikisha siku nane, kama vile Mungu alivyokuwa amemwagiza.
5 Abraham was a hundred years old when his son Isaac was born to him.
Abraham alikuwa na umri wa miaka mia moja wakati mwanawe Isaka anazaliwa kwake.
6 Then Sarah said, “God has made me laugh, and everyone who hears of this will laugh with me.”
Sara akasema, “Mungu amenifanya nicheke; kila mtu atakaye sikia atacheka pamoja na nami.”
7 She added, “Who would have told Abraham that Sarah would nurse children? Yet I have borne him a son in his old age.”
Pia akasema, “Nani angesema kwa Abraham kwamba Sara atalea mtoto, na sasa kweli nimemzalia mtoto wakiume katika uzee wake!”
8 So the child grew and was weaned, and Abraham held a great feast on the day Isaac was weaned.
Mtoto akakua na akaachishwa kunyonya, na Abraham akafanya sherehe kubwa katika siku ambayo Isaka aliachishwa.
9 But Sarah saw that the son whom Hagar the Egyptian had borne to Abraham was mocking her son,
Sara akamwona mwana wa Hajiri Mmisri, ambaye alikuwa amezaliwa kwa Abraham, akidhihaki.
10 and she said to Abraham, “Expel the slave woman and her son, for the slave woman’s son will never share in the inheritance with my son Isaac!”
Kwa hiyo akamwambia Abraham, “Mfukuze huyu mwanamke huyu mtumwa pamoja na mtoto wake: kwa kuwa mtoto huyu wa mwanamke mtumwa hawezi kuwa mrithi pamoja na mwanangu Isaka.”
11 Now this matter distressed Abraham greatly because it concerned his son Ishmael.
Jambo hili likamuhuzunisha sana Abraham kwa sababu ya mwanawe.
12 But God said to Abraham, “Do not be distressed about the boy and your maidservant. Listen to everything that Sarah tells you, for through Isaac your offspring will be reckoned.
Lakini Mungu akamwambia Abraham, “Usihuzunike kwa sababu ya kijana huyu, na kwa sababu ya mwanamke huyu mtumwa wako. Sikiliza maneno asemayo Sara juu ya jambo hili, kwa sababu itakuwa kupitia Isaka kwamba uzao wako utaitwa.
13 But I will also make a nation of the slave woman’s son, because he is your offspring.”
Nitamfanya pia mtoto wa mjakazi kuwa taifa, kwa sababu ni uzao wako.”
14 Early in the morning, Abraham got up, took bread and a skin of water, put them on Hagar’s shoulders, and sent her away with the boy. She left and wandered in the Wilderness of Beersheba.
Abraham akaamka asubuhi na mapema, akachukua mkate na kiriba cha maji, akampatia Hajiri, akiweka juu ya bega lake. Akamtoa kijana akampatia Hajiri na akawaondoa. Hajiri akaondoka akapotea katika jangwa la Beerisheba.
15 When the water in the skin was gone, she left the boy under one of the bushes.
Maji yalipokwisha kwenye kiriba akamtelekeza kijana katika moja ya vichaka.
16 Then she went off and sat down nearby, about a bowshot away, for she said, “I cannot bear to watch the boy die!” And as she sat nearby, she lifted up her voice and wept.
Kisha akaondoka, na akakaa umbali kidogo na yule kijana, umbali kama wa kutupa mshale, kwa vile alisema, “Na nisitazame kifo cha mtoto.” Alipokuwa amekaa kumkabili, akapaza sauti yake akalia.
17 Then God heard the voice of the boy, and the angel of God called to Hagar from heaven, “What is wrong, Hagar? Do not be afraid, for God has heard the voice of the boy where he lies.
Mungu akasikia kilio cha kijana, na malaika wa Mungu akamwita Hajiri kutoka mbinguni, akamwambia, “Nini kinakusumbua? Usiogope, kwa kuwa Mungu amesikia kilio cha kijana mahali alipo.
18 Get up, lift up the boy, and take him by the hand, for I will make him into a great nation.”
Inuka msimamishe mtoto, na umtie moyo; kwa kuwa nitamfanya kuwa taifa kubwa.”
19 Then God opened her eyes, and she saw a well of water. So she went and filled the skin with water and gave the boy a drink.
Kisha Mungu akayafunua macho ya Hajiri, natazama akaona kisima cha maji. Akaenda akajaza kiriba maji, na akampatia kijana akanywa.
20 And God was with the boy, and he grew up and settled in the wilderness and became a great archer.
Mungu akawa pamoja na kijana, na akakua. Akaishi jangwani akawa mwindaji.
21 And while he was dwelling in the Wilderness of Paran, his mother got a wife for him from the land of Egypt.
Akaishi katka jangwa la Parani, na mama yake akampatia mke kutoka Misri.
22 At that time Abimelech and Phicol the commander of his army said to Abraham, “God is with you in all that you do.
Ikawa kwamba katika wakati ule Abimeleki na Fikoli kamanda wa jeshi lake akamwambia Abraham, akisema, “Mungu yuko pamoja na wewe katika yote uyatendayo.
23 Now, therefore, swear to me here before God that you will not deal falsely with me or my children or descendants. Show to me and to the country in which you reside the same kindness that I have shown to you.”
Sasa niapie kwa Mungu kwamba hutanifanyia baya, wala mwanangu, wala uzao wangu. Onesha kwangu na kwa nchi ambayo umekuwa ukikaa agano lile lile la uaminifu ambalo nimekuonesha wewe.”
24 And Abraham replied, “I swear it.”
Abraham akasema, “Nina apa.”
25 But when Abraham complained to Abimelech about a well that Abimelech’s servants had seized,
Abraham pia akamlalamikia Abimeleki kuhusu kisima cha maji ambacho watumishi wa Abimeleki wamekinyang'anya.
26 Abimelech replied, “I do not know who has done this. You did not tell me, so I have not heard about it until today.”
Abimeleki akasema, “Sijui ni nani amefanya jambo hili. Hukuniambia mapema; na sijalisikia ila leo hii.”
27 So Abraham brought sheep and cattle and gave them to Abimelech, and the two men made a covenant.
Kwa hiyo Abraham akachukua kondoo na ng'ombe maksai akampatia Abimeleki, na wawili hawa wakafanya agano.
28 Abraham separated seven ewe lambs from the flock,
Kisha Abraham akatenga wanakondoo wa kike saba pekeyao.
29 and Abimelech asked him, “Why have you set apart these seven ewe lambs?”
Abimeleki akamwambia Abraham, “Nini maana ya hawa wanakondoo wa kike saba ambao umewatenga pekeyao?”
30 He replied, “You are to accept the seven ewe lambs from my hand as my witness that I dug this well.”
Akajibu, “Hawa wanakondoo wa kike saba utawapokea kutoka mkonono mwangu, ili kwamba uwe ushahidi kwangu, kuwa nichimba kisima hiki.”
31 So that place was called Beersheba, because it was there that the two of them swore an oath.
Kwa hiyo akaita mahali pale Beerisheba, kwa sababu mahali pale wote wawili wali apa kiapo.
32 After they had made the covenant at Beersheba, Abimelech and Phicol the commander of his army got up and returned to the land of the Philistines.
Walifanya agano hapo Bersheba, kisha Abimeleki na Fikoli, amiri wa jeshi, wakarudi katika nchi ya Wafilisti.
33 And Abraham planted a tamarisk tree in Beersheba, and there he called upon the name of the LORD, the Eternal God.
Abraham akapanda mti wa mkwaju katika Beerisheba. Na pale akamwabudu Yahwe, Mungu wa milele.
34 And Abraham resided in the land of the Philistines for a long time.
Abraham akasalia kuwa mgeni katika nchi ya Wafilisti kwa siku nyingi.