< Genesis 2 >
1 Thus the heavens and the earth were completed in all their vast array.
Kwa hiyo mbingu na dunia zikakamilika, pamoja na vyote vilivyomo.
2 And by the seventh day God had finished the work He had been doing; so on that day He rested from all His work.
Katika siku ya saba Mungu alikuwa amekamilisha kazi aliyokuwa akiifanya, hivyo siku ya saba akapumzika kutoka kazi zake zote.
3 Then God blessed the seventh day and sanctified it, because on that day He rested from all the work of creation that He had accomplished.
Mungu akaibariki siku ya saba akaifanya takatifu, kwa sababu katika siku hiyo alipumzika kutoka kazi zote za kuumba alizokuwa amefanya.
4 This is the account of the heavens and the earth when they were created, in the day that the LORD God made them.
Haya ndiyo maelezo ya mbingu na dunia wakati zilipoumbwa. Bwana Mungu alipoziumba mbingu na dunia,
5 Now no shrub of the field had yet appeared on the earth, nor had any plant of the field sprouted; for the LORD God had not yet sent rain upon the earth, and there was no man to cultivate the ground.
hapakuwepo na mche wa shambani uliokuwa umejitokeza ardhini, wala hapakuwepo na mmea wa shamba uliokuwa umeota, kwa kuwa Bwana Mungu alikuwa hajanyeshea mvua juu ya nchi, na hapakuwepo mtu wa kuilima ardhi,
6 But springs welled up from the earth and watered the whole surface of the ground.
lakini umande ulitokeza kutoka ardhini na kunyesha uso wote wa nchi:
7 Then the LORD God formed man from the dust of the ground and breathed the breath of life into his nostrils, and the man became a living being.
Bwana Mungu alimuumba mtu kutoka mavumbi ya ardhi, akampulizia pumzi ya uhai puani mwake, naye mtu akawa kiumbe hai.
8 And the LORD God planted a garden in Eden, in the east, where He placed the man He had formed.
Basi Bwana Mungu alikuwa ameotesha bustani upande wa mashariki, katika Edeni, huko akamweka huyo mtu aliyemuumba.
9 Out of the ground the LORD God gave growth to every tree that is pleasing to the eye and good for food. And in the middle of the garden were the tree of life and the tree of the knowledge of good and evil.
Bwana Mungu akafanya aina zote za miti ziote kutoka ardhini, miti yenye kupendeza macho na mizuri kwa chakula. Katikati ya bustani ulikuwepo mti wa uzima na mti wa kujua mema na mabaya.
10 Now a river flowed out of Eden to water the garden, and from there it branched into four headwaters:
Mto wa kunyeshea bustani ulitiririka toka Edeni, kuanzia hapa ukagawanyika kuwa mito minne.
11 The name of the first river is Pishon; it winds through the whole land of Havilah, where there is gold.
Mto wa kwanza uliitwa Pishoni, nao huzunguka nchi yote ya Havila ambako kuna dhahabu.
12 And the gold of that land is pure, and bdellium and onyx are found there.
(Dhahabu ya nchi hiyo ni nzuri, bedola na vito shohamu pia hupatikana huko.)
13 The name of the second river is Gihon; it winds through the whole land of Cush.
Jina la mto wa pili ni Gihoni, ambao huzunguka nchi yote ya Kushi.
14 The name of the third river is Hiddekel; it runs along the east side of Assyria. And the fourth river is the Euphrates.
Jina la mto wa tatu ni Tigrisi, unaopita mashariki ya Ashuru. Mto wa nne ni Frati.
15 Then the LORD God took the man and placed him in the Garden of Eden to cultivate and keep it.
Bwana Mungu akamchukua huyo mtu, akamweka kwenye Bustani ya Edeni ailime na kuitunza.
16 And the LORD God commanded him, “You may eat freely from every tree of the garden,
Bwana Mungu akamwagiza huyo mtu, akamwambia, “Uko huru kula matunda ya mti wowote katika bustani,
17 but you must not eat from the tree of the knowledge of good and evil; for in the day that you eat of it, you will surely die.”
lakini kamwe usile matunda ya mti wa kujua mema na mabaya, kwa maana siku utakapokula matunda yake, hakika utakufa.”
18 The LORD God also said, “It is not good for the man to be alone. I will make for him a suitable helper.”
Bwana Mungu akasema, “Si vyema huyu mtu awe peke yake. Nitamfanyia msaidizi wa kumfaa.”
19 And out of the ground the LORD God formed every beast of the field and every bird of the air, and He brought them to the man to see what he would name each one. And whatever the man called each living creature, that was its name.
Basi Bwana Mungu alikuwa amefanyiza kutoka ardhi wanyama wote wa porini na ndege wote wa angani. Akawaleta kwa huyu mtu aone atawaitaje, nalo jina lolote alilokiita kila kiumbe hai, likawa ndilo jina lake.
20 The man gave names to all the livestock, to the birds of the air, and to every beast of the field. But for Adam no suitable helper was found.
Hivyo Adamu akawapa majina wanyama wote wa kufugwa, ndege wa angani, na wanyama wote wa porini. Lakini kwa Adamu hakupatikana msaidizi wa kumfaa.
21 So the LORD God caused the man to fall into a deep sleep, and while he slept, He took one of the man’s ribs and closed up the area with flesh.
Hivyo Bwana Mungu akamfanya Adamu kulala usingizi mzito, naye alipokuwa amelala akachukua moja ya mbavu zake, akapafunika mahali pale kwa nyama.
22 And from the rib that the LORD God had taken from the man, He made a woman and brought her to him.
Kisha Bwana Mungu akamfanya mwanamke kutoka kwenye ule ubavu aliouchukua kutoka kwa huyo mwanaume, akamleta huyo mwanamke kwa huyo mwanaume.
23 And the man said: “This is now bone of my bones and flesh of my flesh; she shall be called ‘woman,’ for out of man she was taken.”
Huyo mwanaume akasema, “Huyu sasa ni mfupa wa mifupa yangu na nyama ya nyama yangu, ataitwa ‘mwanamke,’ kwa kuwa alitolewa katika mwanaume.”
24 For this reason a man will leave his father and mother and be united to his wife, and they will become one flesh.
Kwa sababu hii mwanaume atamwacha baba yake na mama yake na kuambatana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja.
25 And the man and his wife were both naked, and they were not ashamed.
Adamu na mkewe wote wawili walikuwa uchi, wala hawakuona aibu.