< Galatians 1 >

1 Paul, an apostle—sent not from men nor by man, but by Jesus Christ and God the Father, who raised Him from the dead—
Mimi ni Paulo mtume. Mimi sio mtume kutoka kwa wanadamu wala kupitia kwa mwanadamu, lakini kupitia kwa Yesu Kristo na Mungu Baba aliyemfufua kutoka kwa wafu.
2 and all the brothers with me, To the churches of Galatia:
Pamoja na ndugu wote na mimi, ninayaandikia makanisa ya Galatia.
3 Grace and peace to you from God our Father and the Lord Jesus Christ,
Neema iwe kwenu na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo,
4 who gave Himself for our sins to rescue us from the present evil age, according to the will of our God and Father, (aiōn g165)
aliyejitoa mwenyewe kwa ajili ya dhambi zetu ili kwamba atukomboe na nyakati hizi za uovu, kutokana na mapenzi ya Mungu wetu na Baba. (aiōn g165)
5 to whom be glory forever and ever. Amen. (aiōn g165)
Kwake uwe utukufu milele na milele. (aiōn g165)
6 I am amazed how quickly you are deserting the One who called you by the grace of Christ and are turning to a different gospel—
Ninashangaa kwamba mnageukia haraka kwenye injili nyingine. Ninashangaa kwamba mnageukia mbali kutoka kwake yeye aliyewaita kwa neema ya Kristo.
7 which is not even a gospel. Evidently some people are troubling you and trying to distort the gospel of Christ.
Hakuna injili nyingine, lakini kuna baadhi ya watu wanao wasababishieni nyinyi matatizo na kutaka kubadilisha injili ya Kristo.
8 But even if we or an angel from heaven should preach a gospel contrary to the one we preached to you, let him be under a curse!
Lakini hata kama ni sisi au malaika kutoka mbinguni atatangaza kwenu injili tofauti na ile tuliyoitangaza kwenu, na alaaniwe.
9 As we have said before, so now I say again: If anyone is preaching to you a gospel contrary to the one you received, let him be under a curse!
Kama tulivyo sema mwanzoni, na sasa nasema tena, “Kama kuna mtu atawatangazia kwenu injili tofauti na mliyoipokea, na alaaniwe.”
10 Am I now seeking the approval of men, or of God? Or am I striving to please men? If I were still trying to please men, I would not be a servant of Christ.
Kwani sasa hivi ninatafuta uthibitisho wa watu au Mungu? Ninatafuta kuwafurahisha wanadamu? Kama ninaendelea kujaribu kuwafurahisha wanadamu, mimi sio mtumishi wa Kristo.
11 For I certify to you, brothers, that the gospel I preached was not devised by man.
Ndugu, ninataka ninyi mjue kwamba injili niliyoitangaza haitokani na wanadamu.
12 I did not receive it from any man, nor was I taught it; rather, I received it by revelation from Jesus Christ.
Sikuipokea kutoka kwa mtu, wala sikufundishwa. Badala yake, ilikuwa ni kwa ufunuo wa Yesu Kristo kwangu.
13 For you have heard of my former way of life in Judaism, how severely I persecuted the church of God and tried to destroy it.
Mmekwisha sikia juu ya maisha yangu ya nyuma katika dini ya Kiyahudi, jinsi nilivyokuwa nikilitesa kwa ukali kanisa la Mungu zaidi ya kipimo na kuliteketeza.
14 I was advancing in Judaism beyond many of my contemporaries and was extremely zealous for the traditions of my fathers.
Nilikuwa nimeendelea katika Dini ya Kiyahudi zaidi ya ndugu zangu wengi Wayahudi. Nilikuwa na bidii sana katika tamaduni za baba zangu.
15 But when God, who set me apart from my mother’s womb and called me by His grace, was pleased
Lakini Mungu alipendezwa kunichagua mimi kutoka tumboni mwa mama. Aliniita mimi kupitia neema yake
16 to reveal His Son in me so that I might preach Him among the Gentiles, I did not rush to consult with flesh and blood,
kumdhihirisha Mwanawe ndani yangu, ili kwamba nimtangaze yeye miongoni mwa watu wa mataifa. Wala sikutafuta ushauri wa mwili na damu
17 nor did I go up to Jerusalem to the apostles who came before me, but I went into Arabia and later returned to Damascus.
na sikupanda kwenda Yerusalem kwa wale waliokuwa mitume kabla yangu. Badala yake nilienda Uarabuni na baadae kurudi Damesiki.
18 Only after three years did I go up to Jerusalem to confer with Cephas, and I stayed with him fifteen days.
Kisha baada ya miaka mitatu nilipanda kwenda Yerusalemu kumtembelea Kefa, nikakaa naye kwa siku kumi na tano.
19 But I saw none of the other apostles except James, the Lord’s brother.
Lakini sikuona mitume wengine isipokuwa Yakobo, ndungu yake na Bwana.
20 I assure you before God that what I am writing to you is no lie.
Tazama, mbele za Mungu, sidanganyi kwa kile niandikacho kwenu.
21 Later I went to the regions of Syria and Cilicia.
Kisha nilikwenda mikoa ya Shamu na Kilikia.
22 I was personally unknown, however, to the churches of Judea that are in Christ.
Sikuwa najulikana kwa macho kwa makanisa ya Uyahudi yale yaliyokuwa katika Kristo,
23 They only heard the account: “The man who formerly persecuted us is now preaching the faith he once tried to destroy.”
lakini walikuwa wakisikia tu, “Yeye aliyekuwa akitutesa sasa anatangaza imani aliyokuwa akiiharibu.”
24 And they glorified God because of me.
Walikuwa wakimtukuza Mungu kwa ajili yangu.

< Galatians 1 >