< Galatians 1 >
1 Paul, an apostle—sent not from men nor by man, but by Jesus Christ and God the Father, who raised Him from the dead—
Paulo mtume: si mtume wa wanadamu wala aliyetumwa na mwanadamu, bali na Yesu Kristo na Mungu Baba aliyemfufua Yesu kutoka kwa wafu;
2 and all the brothers with me, To the churches of Galatia:
na ndugu wote walio pamoja nami: Kwa makanisa ya Galatia:
3 Grace and peace to you from God our Father and the Lord Jesus Christ,
Neema iwe nanyi na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana wetu Yesu Kristo,
4 who gave Himself for our sins to rescue us from the present evil age, according to the will of our God and Father, (aiōn )
aliyejitoa kwa ajili ya dhambi zetu ili apate kutuokoa katika ulimwengu huu wa sasa ulio mbaya, sawasawa na mapenzi yake yeye aliye Mungu na Baba yetu. (aiōn )
5 to whom be glory forever and ever. Amen. (aiōn )
Utukufu una yeye milele na milele. Amen. (aiōn )
6 I am amazed how quickly you are deserting the One who called you by the grace of Christ and are turning to a different gospel—
Nashangaa kwamba mnamwacha upesi hivyo yeye aliyewaita kwa neema ya Kristo na kuifuata Injili nyingine,
7 which is not even a gospel. Evidently some people are troubling you and trying to distort the gospel of Christ.
ambayo kwa kweli si Injili kamwe, ila kwa dhahiri kuna watu wanaowachanganya na wanaotaka kuipotosha Injili ya Kristo.
8 But even if we or an angel from heaven should preach a gospel contrary to the one we preached to you, let him be under a curse!
Lakini hata ikiwa sisi au malaika atokaye mbinguni akihubiri Injili nyingine tofauti na ile tuliyowahubiria sisi, basi mtu huyo alaaniwe milele!
9 As we have said before, so now I say again: If anyone is preaching to you a gospel contrary to the one you received, let him be under a curse!
Kama vile tulivyokwisha kusema kabla, sasa nasema tena, ikiwa mtu yeyote atawahubiria Injili kinyume na ile mliyoipokea na alaaniwe milele!
10 Am I now seeking the approval of men, or of God? Or am I striving to please men? If I were still trying to please men, I would not be a servant of Christ.
Je, sasa mimi ninatafuta kukubaliwa na wanadamu au kukubaliwa na Mungu? Au nataka kuwapendeza wanadamu? Kama ningekuwa bado najaribu kuwapendeza wanadamu, nisingekuwa mtumishi wa Kristo.
11 For I certify to you, brothers, that the gospel I preached was not devised by man.
Ndugu zangu, nataka mjue kwamba Injili niliyowahubiria haikutokana na wanadamu.
12 I did not receive it from any man, nor was I taught it; rather, I received it by revelation from Jesus Christ.
Kwa maana mimi sikuipokea hiyo Injili kutoka kwa mwanadamu, wala sikufundishwa na mtu, bali niliipata kwa ufunuo kutoka kwa Yesu Kristo.
13 For you have heard of my former way of life in Judaism, how severely I persecuted the church of God and tried to destroy it.
Ninyi mmekwisha kusikia juu ya maisha yangu ya zamani nilipokuwa katika dini ya Kiyahudi, jinsi nilivyolitesa kanisa la Mungu kwa nguvu na kujaribu kuliangamiza.
14 I was advancing in Judaism beyond many of my contemporaries and was extremely zealous for the traditions of my fathers.
Nami niliendelea sana katika dini ya Kiyahudi kuliko Wayahudi wengi wa rika yangu maana nilijitahidi sana katika desturi za baba zangu.
15 But when God, who set me apart from my mother’s womb and called me by His grace, was pleased
Lakini ilipompendeza Mungu, aliyenitenga tangu tumboni mwa mama yangu na kuniita kwa neema yake,
16 to reveal His Son in me so that I might preach Him among the Gentiles, I did not rush to consult with flesh and blood,
alimdhihirisha Mwanawe kwangu, ili nipate kumhubiri miongoni mwa watu wa Mataifa. Mimi sikushauriana na mwanadamu yeyote,
17 nor did I go up to Jerusalem to the apostles who came before me, but I went into Arabia and later returned to Damascus.
wala sikupanda kwenda Yerusalemu kuwaona hao waliokuwa mitume kabla yangu, bali nilikwenda mara moja Arabuni na kisha nikarudi Dameski.
18 Only after three years did I go up to Jerusalem to confer with Cephas, and I stayed with him fifteen days.
Kisha baada ya miaka mitatu nilipanda kwenda Yerusalemu kuonana na Kefa na nilikaa naye siku kumi na tano.
19 But I saw none of the other apostles except James, the Lord’s brother.
Lakini sikumwona mtume mwingine yeyote isipokuwa Yakobo, ndugu yake Bwana.
20 I assure you before God that what I am writing to you is no lie.
Nawahakikishia mbele za Mungu kuwa ninayowaandikia si uongo.
21 Later I went to the regions of Syria and Cilicia.
Baadaye nilikwenda sehemu za Syria na Kilikia.
22 I was personally unknown, however, to the churches of Judea that are in Christ.
Lakini mimi binafsi sikujulikana kwa makanisa ya huko Uyahudi yaliyo katika Kristo.
23 They only heard the account: “The man who formerly persecuted us is now preaching the faith he once tried to destroy.”
Wao walisikia habari tu kwamba, “Mtu yule ambaye hapo kwanza alikuwa akitutesa sasa anahubiri imani ile ile aliyokuwa akijaribu kuiangamiza.”
24 And they glorified God because of me.
Nao wakamtukuza Mungu kwa sababu yangu.