< Colossians 3 >

1 Therefore, since you have been raised with Christ, strive for the things above, where Christ is seated at the right hand of God.
Basi, kwa kuwa mmefufuliwa pamoja na Kristo, yatafuteni yaliyo juu, Kristo alikoketi mkono wa kuume wa Mungu.
2 Set your minds on things above, not on earthly things.
Yafikirini mambo yaliyo juu, wala si ya duniani.
3 For you died, and your life is now hidden with Christ in God.
Kwa maana ninyi mlikufa, nao uhai wenu sasa umefichwa pamoja na Kristo katika Mungu.
4 When Christ, who is your life, appears, then you also will appear with Him in glory.
Wakati Kristo, aliye uzima wenu, atakapotokea, ndipo nanyi mtakapotokea pamoja naye katika utukufu.
5 Put to death, therefore, the components of your earthly nature: sexual immorality, impurity, lust, evil desires, and greed, which is idolatry.
Kwa hiyo, ueni kabisa chochote kilicho ndani yenu cha asili ya kidunia: yaani uasherati, uchafu, tamaa mbaya, mawazo mabaya na ulafi, ambayo ndiyo ibada ya sanamu.
6 Because of these, the wrath of God is coming on the sons of disobedience.
Kwa sababu ya mambo haya, ghadhabu ya Mungu inakuja.
7 When you lived among them, you also used to walk in these ways.
Ninyi pia zamani mlienenda katika mambo haya mlipoishi maisha hayo.
8 But now you must put aside all such things as these: anger, rage, malice, slander, and filthy language from your lips.
Lakini sasa yawekeni mbali nanyi mambo kama haya yote: yaani hasira, ghadhabu, uovu, masingizio na lugha chafu kutoka midomoni mwenu.
9 Do not lie to one another, since you have taken off the old self with its practices,
Msiambiane uongo, kwa maana mmevua kabisa utu wenu wa kale pamoja na matendo yake,
10 and have put on the new self, which is being renewed in knowledge in the image of its Creator.
nanyi mmevaa utu mpya, unaofanywa upya katika ufahamu sawasawa na mfano wa Muumba wake.
11 Here there is no Greek or Jew, circumcised or uncircumcised, barbarian, Scythian, slave, or free, but Christ is all and is in all.
Hapa hakuna Myunani wala Myahudi, aliyetahiriwa wala asiyetahiriwa, asiyestaarabika wala aliyestaarabika, mtumwa wala mtu huru, bali Kristo ni yote, na ndani ya wote.
12 Therefore, as the elect of God, holy and beloved, clothe yourselves with hearts of compassion, kindness, humility, gentleness, and patience.
Kwa hiyo, kwa kuwa ninyi mmekuwa wateule wa Mungu, watakatifu wapendwao sana, jivikeni moyo wa huruma, utu wema, unyenyekevu, upole na uvumilivu.
13 Bear with one another and forgive any complaint you may have against someone else. Forgive as the Lord forgave you.
Vumilianeni na kusameheana mtu akiwa na lalamiko lolote dhidi ya mwenzake. Sameheaneni kama vile Bwana alivyowasamehe ninyi.
14 And over all these virtues put on love, which is the bond of perfect unity.
Zaidi ya maadili haya yote jivikeni upendo, ambao ndio unaofunga kila kitu pamoja katika umoja mkamilifu.
15 Let the peace of Christ rule in your hearts, for to this you were called as members of one body. And be thankful.
Amani ya Kristo na itawale mioyoni mwenu, kwa kuwa ninyi kama viungo vya mwili mmoja mmeitiwa amani. Tena kuweni watu wa shukrani.
16 Let the word of Christ richly dwell within you as you teach and admonish one another with all wisdom, and as you sing psalms, hymns, and spiritual songs with gratitude in your hearts to God.
Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu, mkifundishana na kuonyana katika hekima yote, mkimwimbia Mungu zaburi, nyimbo na tenzi za rohoni, huku mkiwa na shukrani mioyoni mwenu.
17 And whatever you do, in word or deed, do it all in the name of the Lord Jesus, giving thanks to God the Father through Him.
Lolote mfanyalo, ikiwa ni kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu, mkimshukuru Mungu Baba katika yeye.
18 Wives, submit to your husbands, as is fitting in the Lord.
Ninyi wake, watiini waume zenu, kama inavyostahili katika Bwana.
19 Husbands, love your wives and do not be harsh with them.
Ninyi waume, wapendeni wake zenu, wala msiwe na uchungu dhidi yao.
20 Children, obey your parents in everything, for this is pleasing to the Lord.
Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika mambo yote, kwa maana hivi ndivyo inavyompendeza Bwana.
21 Fathers, do not provoke your children, so they will not become discouraged.
Ninyi akina baba, msiwachokoze watoto wenu, wasije wakakata tamaa.
22 Slaves, obey your earthly masters in everything, not only to please them while they are watching, but with sincerity of heart and fear of the Lord.
Ninyi watumwa, watiini mabwana zenu wa hapa duniani katika mambo yote. Fanyeni hivyo si wakiwepo tu, wala si kwa kutafuta upendeleo wao, bali kwa moyo mnyofu na kumcha Bwana.
23 Whatever you do, work at it with your whole being, for the Lord and not for men,
Lolote mfanyalo, fanyeni kwa moyo kama watu wanaomtumikia Bwana, na si wanadamu,
24 because you know that you will receive an inheritance from the Lord as your reward. It is the Lord Christ you are serving.
kwa kuwa mnajua kwamba mtapokea urithi wenu kutoka kwa Bwana ukiwa thawabu yenu. Ni Bwana Yesu Kristo mnayemtumikia.
25 Whoever does wrong will be repaid for his wrong, and there is no favoritism.
Yeyote atendaye mabaya atalipwa kwa ajili ya mabaya yake, wala hakuna upendeleo.

< Colossians 3 >