< Acts 11 >

1 The apostles and brothers throughout Judea soon heard that the Gentiles also had received the word of God.
Mitume na ndugu wale waliokuwa huko Yudea walisikia kuwa wamataifa wamelipokea neno la Mungu.
2 So when Peter went up to Jerusalem, the circumcised believers took issue with him
Petro alipokuja huko Yerusalemu, lile kundi la watu waliotahiriwa wakaanza kumkosoa, Wakisema,
3 and said, “You visited uncircumcised men and ate with them.”
“Umeshikamana na watu wasiotahiriwa na kula nao!”
4 But Peter began and explained to them the whole sequence of events:
Lakini Petro alianza kueleza tukio kwa kina; akisema,
5 “I was in the city of Joppa praying, and in a trance I saw a vision of something like a large sheet being let down from heaven by its four corners, and it came right down to me.
“Nilikuwa naomba katika mji wa Yafa, na nikaona maono ya chombo kikishuka chini kama nguo kubwa ikishuka kutoka mbinguni katika pembe zake zote nne. Kikashuka kwangu.
6 I looked at it closely and saw four-footed animals of the earth, wild beasts, reptiles, and birds of the air.
Nilikitazama na kufikiri juu yake. Nikaona wanyama wenye miguu minne waishio katika nchi, na wanyama wa polini na wanyama watambaao na ndege wa angani.
7 Then I heard a voice saying to me, ‘Get up, Peter, kill and eat.’
Kisha nikasikia sauti ikisema nami, “Amka, Petro, chinja naj ule!”
8 ‘No, Lord,’ I said, ‘for nothing impure or unclean has ever entered my mouth.’
Nikasema, “Siyo hivyo, Bwana, mdomoni mwangu hakujawahi kuingia kitu chochote kisicho kitakatifu au kichafu”
9 But the voice spoke from heaven a second time, ‘Do not call anything impure that God has made clean.’
Lakini sauti ikajibu tena kutoka Mbinguni, kile Mungu alichokitangaza kuwa ni safi, usikiite najisi,
10 This happened three times, and everything was drawn back up into heaven.
Hii ilitokea mara tatu, na kila kitu kikachukuliwa mbinguni tena.
11 Just then three men sent to me from Caesarea stopped at the house where I was staying.
Tazama, wakati huo watu watatu walikuwa wamesimama mbele ya nyumba ile tulimokuwa; wametumwa kutoka Kaisaria kuja kwangu.
12 The Spirit told me to accompany them without hesitation. These six brothers also went with me, and we entered the man’s home.
Roho akaniambia kwenda nao, na nisitofautiane nao. Hawa wanaume sita wakaenda pamoja na mimi na tuliende kwenye nyumba ya mtu mmoja.
13 He told us how he had seen an angel standing in his house and saying, ‘Send to Joppa for Simon who is called Peter.
Alituambia vile alivyomwona malaika amesimama ndani ya nyumba yake akisema, “Nitume Yafa nikamlete simoni ambaye jina lake lingine ni Petro.
14 He will convey to you a message by which you and all your household will be saved.’
Atasema ujumbe kwako katika huo utaokoka wewe na nyumba yako yote.”
15 As I began to speak, the Holy Spirit fell upon them, just as He had fallen upon us at the beginning.
Nilipoanza kusema nao, Roho mtakatifu akaja juu yao kama alivyokuja kwetu mwanzoni.
16 Then I remembered the word of the Lord, as He used to say, ‘John baptized with water, but you will be baptized with the Holy Spirit.’
Nakumbuka maneno ya Bwana, alivyosema, “Yohana alibatiza kwa maji; lakini mtabatizwa katika Roho mtakatifu.”
17 So if God gave them the same gift He gave us who believed in the Lord Jesus Christ, who was I to hinder the work of God?”
Pia kama Mungu ametoa zawadi kama alizotupa sisi tulipoamini katika Bwana Yesu Kristo, mimi ni nani, kwamba naweza kumpinga Mungu?
18 When they heard this, their objections were put to rest, and they glorified God, saying, “So then, God has granted even the Gentiles repentance unto life.”
Waliposikia mambo haya, hawakurudisha, bali walimsifu Mungu na kusema, “Mungu ametoa toba kwa ajili ya wa mataifa pia”
19 Meanwhile those scattered by the persecution that began with Stephen traveled as far as Phoenicia, Cyprus, and Antioch, speaking the message only to Jews.
Basi waamini ambao mateso yalianzia kwenye kifo cha Stephano walitawanyika kutoka Yerusalemu-waamini hawa walienda mbali, hadi mpaka Foinike, Kipro na Antiokia. Waliwaambia ujumbe kuhusu Yesu peke yake kwa wayahudi na si kwa mwingine awaye yote.
20 But some of them, men from Cyprus and Cyrene, went to Antioch and began speaking to the Greeks as well, proclaiming the good news about the Lord Jesus.
Lakini baadhi yao ni watu kutoka Kipro na Krene, walikuja Antiokia na kusema na wayunani na kumhubiri Bwana Yesu.
21 The hand of the Lord was with them, and a great number of people believed and turned to the Lord.
Na mkono wa Bwana ulikuwa pamoja nao, na watu wengi waliamini na kumgeukia Bwana.
22 When news of this reached the ears of the church in Jerusalem, they sent Barnabas to Antioch.
Habari zao zikafikia masikioni mwa kanisa la Yerusalem: na wakamtuma Barnaba aende mpaka Antiokia.
23 When he arrived and saw the grace of God, he rejoiced and encouraged them all to abide in the Lord with all their hearts.
Alipokuja na kuona karama ya Mungu alifurahi; na aliwatia moyo wote kubaki na Bwana katika mioyo yao.
24 Barnabas was a good man, full of the Holy Spirit and faith, and a great number of people were brought to the Lord.
Kwa sababu alikuwa mtu mwema na amejazwa na Roho Mtakatifu na imani na watu wengi wakaongezeka katika Bwana.
25 Then Barnabas went to Tarsus to look for Saul,
Baadaye Barnaba alienda Tarso kumwona Sauli.
26 and when he found him, he brought him back to Antioch. So for a full year they met together with the church and taught large numbers of people. The disciples were first called Christians at Antioch.
Alipompata, akamleta Antiokia. Ikawa kwa mwaka mzima wakakusanyika pamoja na kanisa na kuwafundisha watu wengi. Na wanafunzi wakaitwa wakristo kwa mara ya kwanza huko Antiokia.
27 In those days some prophets came down from Jerusalem to Antioch.
Na katika siku hizi manabii wakashuka kutoka Yerusalemu mpaka Antiokia.
28 One of them named Agabus stood up and predicted through the Spirit that a great famine would sweep across the whole world. (This happened under Claudius.)
Mmoja wao ni Agabo ndilo jina lake, akasimama akiashiriwa na Roho kuwa njaa kali itatokea ulimwenguni mwote. Hii ilitokea wakati wa siku za Klaudio.
29 So the disciples, each according to his ability, decided to send relief to the brothers living in Judea.
Kwa hiyo, wanafunzi, kila mmoja alivyo fanikiwa, waliamua kupeleka misaada kwa ndugu walioko Uyahudi.
30 This they did, sending their gifts to the elders with Barnabas and Saul.
Walifanya hivi; Walituma pesa kwa mkono wa Barnaba na Sauli.

< Acts 11 >