< 1 Corinthians 3 >

1 Brothers, I could not address you as spiritual, but as worldly—as infants in Christ.
Ndugu zangu, mimi sikuweza kusema nanyi kama watu wa kiroho, bali kama watu wa mwilini, kama watoto wachanga katika Kristo.
2 I gave you milk, not solid food, for you were not yet ready for solid food. In fact, you are still not ready,
Naliwanywesha maziwa, wala si chakula kigumu, kwa kuwa hamkuwa tayari kwa hicho chakula. Naam, hata sasa hamko tayari.
3 for you are still worldly. For since there is jealousy and dissension among you, are you not worldly? Are you not walking in the way of man?
Ninyi bado ni watu wa mwilini. Kwa kuwa bado kuna wivu na magombano miongoni mwenu, je, ninyi si watu wa mwilini? Je, si mwaendelea kama watu wa kawaida?
4 For when one of you says, “I follow Paul,” and another, “I follow Apollos,” are you not mere men?
Kwa maana mmoja anaposema, “Mimi ni wa Paulo,” na mwingine, “Mimi ni wa Apolo,” je, ninyi si wanadamu wa kawaida?
5 What then is Apollos? And what is Paul? They are servants through whom you believed, as the Lord has assigned to each his role.
Kwani, Apolo ni nani? Naye Paulo ni nani? Ni watumishi tu ambao kupitia wao mliamini, kama vile Bwana alivyompa kila mtu huduma yake.
6 I planted the seed and Apollos watered it, but God made it grow.
Mimi nilipanda mbegu, Apolo akatia maji, lakini Mungu ndiye aliikuza.
7 So neither he who plants nor he who waters is anything, but only God, who makes things grow.
Hivyo mwenye kupanda na mwenye kutia maji si kitu, bali Mungu peke yake ambaye huifanya ikue.
8 He who plants and he who waters are one in purpose, and each will be rewarded according to his own labor.
Apandaye mbegu ana lengo sawa na yule atiaye maji na kila mmoja atalipwa kulingana na kazi yake.
9 For we are God’s fellow workers; you are God’s field, God’s building.
Kwa kuwa sisi tu watendakazi pamoja na Mungu. Ninyi ni shamba la Mungu, jengo la Mungu.
10 By the grace God has given me, I laid a foundation as an expert builder, and someone else is building on it. But each one must be careful how he builds.
Kwa neema Mungu aliyonipa, niliweka msingi kama mjenzi stadi na mtu mwingine anajenga juu yake. Lakini kila mmoja inampasa awe mwangalifu jinsi anavyojenga.
11 For no one can lay a foundation other than the one already laid, which is Jesus Christ.
Kwa maana hakuna mtu yeyote awezaye kuweka msingi mwingine wowote isipokuwa ule uliokwisha kuwekwa, ambao ni Yesu Kristo.
12 If anyone builds on this foundation using gold, silver, precious stones, wood, hay, or straw,
Kama mtu yeyote akijenga juu ya msingi huu kwa kutumia dhahabu, fedha, vito vya thamani, miti, majani au nyasi,
13 his workmanship will be evident, because the Day will bring it to light. It will be revealed with fire, and the fire will prove the quality of each man’s work.
kazi yake itaonekana ilivyo, kwa kuwa Siku ile itaidhihirisha. Itadhihirishwa kwa moto, nao moto utapima ubora wa kazi ya kila mtu.
14 If what he has built survives, he will receive a reward.
Kama kile alichojenga kitabaki, atapokea thawabu yake.
15 If it is burned up, he will suffer loss. He himself will be saved, but only as if through the flames.
Kama kazi kitateketea, atapata hasara, ila yeye mwenyewe ataokolewa, lakini tu kama mtu aliyenusurika kwenye moto.
16 Do you not know that you yourselves are God’s temple, and that God’s Spirit dwells in you?
Je, hamjui ya kwamba ninyi wenyewe ni hekalu la Mungu na kwamba Roho wa Mungu anakaa ndani yenu?
17 If anyone destroys God’s temple, God will destroy him; for God’s temple is holy, and you are that temple.
Kama mtu yeyote akiliharibu hekalu la Mungu, Mungu atamwangamiza; kwa maana hekalu la Mungu ni takatifu, na ninyi ndiyo hilo hekalu.
18 Let no one deceive himself. If any of you thinks he is wise in this age, he should become a fool, so that he may become wise. (aiōn g165)
Msijidanganye. Kama mtu yeyote miongoni mwenu akidhani kuwa ana hekima kwa viwango vya dunia hii, inampasa awe mjinga ili apate kuwa na hekima. (aiōn g165)
19 For the wisdom of this world is foolishness in God’s sight. As it is written: “He catches the wise in their craftiness.”
Kwa maana hekima ya ulimwengu huu ni upuzi mbele za Mungu. Kama ilivyoandikwa: “Mungu huwanasa wenye hekima katika hila yao,”
20 And again, “The Lord knows that the thoughts of the wise are futile.”
tena, “Bwana anajua kwamba mawazo ya wenye hekima ni ubatili.”
21 Therefore, stop boasting in men. All things are yours,
Hivyo basi, mtu asijivune kuhusu wanadamu! Vitu vyote ni vyenu,
22 whether Paul or Apollos or Cephas or the world or life or death or the present or the future. All of them belong to you,
ikiwa ni Paulo au Apolo au Kefa au dunia au uzima au mauti, au wakati uliopo au wakati ujao, haya yote ni yenu
23 and you belong to Christ, and Christ belongs to God.
na ninyi ni wa Kristo, naye Kristo ni wa Mungu.

< 1 Corinthians 3 >