< 1 Corinthians 15 >

1 Now, brothers, I want to remind you of the gospel I preached to you, which you received, and in which you stand firm.
Basi ndugu zangu nataka niwakumbushe kuhusu Injili niliyowahubiria, mkaipokea na ambayo katika hiyo mmesimama.
2 By this gospel you are saved, if you hold firmly to the word I preached to you. Otherwise, you have believed in vain.
Kwa Injili hii mnaokolewa mkishikilia kwa uthabiti neno nililowahubiria ninyi. La sivyo, mmeamini katika ubatili.
3 For what I received I passed on to you as of first importance: that Christ died for our sins according to the Scriptures,
Kwa maana yale niliyopokea ndiyo niliyowapa ninyi, kama yenye umuhimu wa kwanza: Kwamba Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi zetu, kama yasemavyo Maandiko,
4 that He was buried, that He was raised on the third day according to the Scriptures,
ya kuwa alizikwa na alifufuliwa siku ya tatu, kama yasemavyo Maandiko,
5 and that He appeared to Cephas and then to the Twelve.
na kwamba alimtokea Kefa, kisha akawatokea wale kumi na wawili.
6 After that, He appeared to more than five hundred brothers at once, most of whom are still living, though some have fallen asleep.
Baadaye akawatokea wale ndugu waumini zaidi ya 500 kwa pamoja, ambao wengi wao bado wako hai, ingawa wengine wamelala.
7 Then He appeared to James, then to all the apostles.
Ndipo akamtokea Yakobo na kisha mitume wote.
8 And last of all He appeared to me also, as to one of untimely birth.
Mwisho wa wote, akanitokea mimi pia, ambaye ni kama aliyezaliwa si kwa wakati wake.
9 For I am the least of the apostles and am unworthy to be called an apostle, because I persecuted the church of God.
Kwa maana mimi ndiye mdogo kuliko mitume wote, nisiyestahili kuitwa mtume, kwa sababu nililitesa kanisa la Mungu.
10 But by the grace of God I am what I am, and His grace to me was not in vain. No, I worked harder than all of them—yet not I, but the grace of God that was with me.
Lakini kwa neema ya Mungu nimekuwa hivi nilivyo na neema yake kwangu haikuwa kitu bure. Bali nilizidi sana kufanya kazi kuliko mitume wote, lakini haikuwa mimi, bali ni ile neema ya Mungu iliyokuwa pamoja nami.
11 Whether, then, it was I or they, this is what we preach, and this is what you believed.
Hivyo basi, kama ilikuwa mimi au wao, hili ndilo tunalohubiri, na hili ndilo mliloamini.
12 But if it is preached that Christ has been raised from the dead, how can some of you say that there is no resurrection of the dead?
Basi kama tumehubiri ya kwamba Kristo alifufuliwa kutoka kwa wafu, mbona baadhi yenu mnasema hakuna ufufuo wa wafu?
13 If there is no resurrection of the dead, then not even Christ has been raised.
Lakini kama hakuna ufufuo wa wafu, basi hata Kristo hakufufuliwa.
14 And if Christ has not been raised, our preaching is worthless, and so is your faith.
Tena ikiwa Kristo hakufufuliwa kutoka kwa wafu, kuhubiri kwetu kumekuwa ni bure na imani yenu ni batili.
15 In that case, we are also exposed as false witnesses about God. For we have testified about God that He raised Christ from the dead, but He did not raise Him if in fact the dead are not raised.
Zaidi ya hayo, twaonekana kuwa mashahidi wa uongo kuhusu Mungu, kwa sababu tumeshuhudia kumhusu Mungu kwamba alimfufua Kristo kutoka kwa wafu, lakini hilo haliwezi kuwa kweli kama wafu hawafufuliwi.
16 For if the dead are not raised, then not even Christ has been raised.
Kwa kuwa kama wafu hawafufuliwi, basi hata Kristo hajafufuka.
17 And if Christ has not been raised, your faith is futile; you are still in your sins.
Tena kama Kristo hajafufuliwa, imani yenu ni batili; nanyi bado mko katika dhambi zenu.
18 Then those also who have fallen asleep in Christ have perished.
Hivyo basi, wote waliolala katika Kristo wamepotea.
19 If our hope in Christ is for this life alone, we are to be pitied more than all men.
Ikiwa tumaini letu ndani ya Kristo ni kwa ajili ya maisha haya tu, sisi tunastahili kuhurumiwa kuliko watu wote.
20 But Christ has indeed been raised from the dead, the firstfruits of those who have fallen asleep.
Lakini kweli Kristo amefufuliwa kutoka kwa wafu, tunda la kwanza la wale wote waliolala.
21 For since death came through a man, the resurrection of the dead comes also through a man.
Kwa maana kama vile mauti ilivyokuja kwa njia ya mtu mmoja, vivyo hivyo, ufufuo wa wafu umekuja kwa njia ya mtu mmoja.
22 For as in Adam all die, so in Christ all will be made alive.
Kwa maana kama vile katika Adamu watu wote wanakufa, vivyo hivyo katika Kristo wote watafanywa hai.
23 But each in his own turn: Christ the firstfruits; then at His coming, those who belong to Him.
Lakini kila mmoja kwa wakati wake: Kristo, tunda la kwanza kisha, wale walio wake, wakati atakapokuja.
24 Then the end will come, when He hands over the kingdom to God the Father after He has destroyed all dominion, authority, and power.
Ndipo mwisho utafika, wakati atakapomkabidhi Mungu Baba ufalme, akiisha angamiza kila utawala na kila mamlaka na nguvu.
25 For He must reign until He has put all His enemies under His feet.
Kwa maana lazima Kristo atawale mpaka awe amewaweka adui zake wote chini ya miguu yake.
26 The last enemy to be destroyed is death.
Adui wa mwisho atakayeangamizwa ni mauti.
27 For “God has put everything under His feet.” Now when it says that everything has been put under Him, this clearly does not include the One who put everything under Him.
Kwa maana Mungu “ameweka vitu vyote chini ya miguu yake.” Lakini isemapo kwamba “vitu vyote” vimewekwa chini yake, ni wazi kwamba Mungu aliyetiisha vitu vyote chini ya Kristo hayumo miongoni mwa hivyo vilivyotiishwa.
28 And when all things have been subjected to Him, then the Son Himself will be made subject to Him who put all things under Him, so that God may be all in all.
Atakapokuwa amekwisha kuyafanya haya, ndipo Mwana mwenyewe atatiishwa chini yake yeye aliyetiisha vitu vyote, ili Mungu awe yote katika yote.
29 If these things are not so, what will those do who are baptized for the dead? If the dead are not raised at all, why are people baptized for them?
Basi kama hakuna ufufuo, watafanyaje wale wabatizwao kwa ajili ya wafu? Kama wafu hawafufuliwi kamwe, mbona watu wanabatizwa kwa ajili yao?
30 And why do we endanger ourselves every hour?
Nasi kwa upande wetu kwa nini tunajihatarisha kila saa?
31 I face death every day, brothers, as surely as I boast about you in Christ Jesus our Lord.
Kama majivuno yangu kwa ajili yenu katika Kristo Yesu Bwana wetu ni kweli, ndugu zangu, ninakufa kila siku.
32 If I fought wild beasts in Ephesus for human motives, what did I gain? If the dead are not raised, “Let us eat and drink, for tomorrow we die.”
Kama kwa sababu za kibinadamu tu nilipigana na wanyama wakali huko Efeso, ningekuwa nimepata faida gani? Kama wafu hawafufuliwi, “Tuleni na kunywa, kwa kuwa kesho tutakufa.”
33 Do not be deceived: “Bad company corrupts good character.”
Msidanganyike: “Ushirika na watu wabaya huharibu tabia njema.”
34 Sober up as you ought, and stop sinning; for some of you are ignorant of God. I say this to your shame.
Zindukeni mwe na akili kama iwapasavyo, wala msitende dhambi tena; kwa maana watu wengine hawamjui Mungu. Nasema mambo haya ili mwone aibu.
35 But someone will ask, “How are the dead raised? With what kind of body will they come?”
Lakini mtu anaweza kuuliza, “Wafu wafufuliwaje? Watakuwa na mwili wa namna gani?”
36 You fool! What you sow does not come to life unless it dies.
Ninyi wapumbavu kiasi gani? Mpandacho hakiwi hai kama hakikufa.
37 And what you sow is not the body that will be, but just a seed, perhaps of wheat or something else.
Mpandapo, hampandi mwili ule utakao kuwa, bali mwapanda mbegu tu, pengine ya ngano au ya kitu kingine.
38 But God gives it a body as He has designed, and to each kind of seed He gives its own body.
Lakini Mungu huipa mbegu umbo kama alivyokusudia mwenyewe na kila aina ya mbegu huipa umbo lake.
39 Not all flesh is the same: Men have one kind of flesh, animals have another, birds another, and fish another.
Kwa maana nyama zote si za aina moja. Binadamu wana nyama ya aina moja, wanyama wana aina nyingine, kadhalika ndege na samaki wana nyama tofauti.
40 There are also heavenly bodies and earthly bodies. But the splendor of the heavenly bodies is of one degree, and the splendor of the earthly bodies is of another.
Pia kuna miili ya mbinguni na miili ya duniani, lakini fahari wa ile miili ya mbinguni ni wa aina moja na fahari wa ile miili ya duniani ni wa aina nyingine.
41 The sun has one degree of splendor, the moon another, and the stars another; and star differs from star in splendor.
Jua lina fahari ya aina moja, mwezi nao una fahari yake na nyota pia, nazo nyota hutofautiana katika fahari.
42 So will it be with the resurrection of the dead: What is sown is perishable; it is raised imperishable.
Hivyo ndivyo itakavyokuwa wakati wa ufufuo wa wafu. Ule mwili wa kuharibika uliopandwa, utafufuliwa usioharibika,
43 It is sown in dishonor; it is raised in glory. It is sown in weakness; it is raised in power.
unapandwa katika aibu, unafufuliwa katika utukufu, unapandwa katika udhaifu, unafufuliwa katika nguvu,
44 It is sown a natural body; it is raised a spiritual body. If there is a natural body, there is also a spiritual body.
unapandwa mwili wa asili, unafufuliwa mwili wa kiroho. Kama kuna mwili wa asili, basi kuna mwili wa kiroho pia.
45 So it is written: “The first man Adam became a living being;” the last Adam a life-giving spirit.
Kwa hiyo imeandikwa, “Mtu wa kwanza Adamu alifanyika kiumbe hai”; Adamu wa mwisho, yeye ni roho iletayo uzima.
46 The spiritual, however, was not first, but the natural, and then the spiritual.
Lakini si ule wa kiroho uliotangulia, bali ni ule wa asili, kisha ule wa kiroho.
47 The first man was of the dust of the earth, the second man from heaven.
Mtu wa kwanza aliumbwa kwa mavumbi ya ardhini, mtu wa pili alitoka mbinguni.
48 As was the earthly man, so also are those who are of the earth; and as is the heavenly man, so also are those who are of heaven.
Kama vile alivyokuwa yule wa ardhini, ndivyo walivyo wale walio wa ardhini; na kwa vile alivyo mtu yule aliyetoka mbinguni, ndivyo walivyo wale walio wa mbinguni.
49 And just as we have borne the likeness of the earthly man, so also shall we bear the likeness of the heavenly man.
Kama vile tulivyochukua mfano wa mtu wa ardhini, ndivyo tutakavyochukua mfano wa yule mtu aliyetoka mbinguni.
50 Now I declare to you, brothers, that flesh and blood cannot inherit the kingdom of God, nor does the perishable inherit the imperishable.
Ndugu zangu nisemalo ni hili: nyama na damu haviwezi kuurithi ufalme wa Mungu, wala kuharibika kurithi kutokuharibika.
51 Listen, I tell you a mystery: We will not all sleep, but we will all be changed—
Sikilizeni, nawaambia siri: Sote hatutalala, lakini sote tutabadilishwa
52 in an instant, in the twinkling of an eye, at the last trumpet. For the trumpet will sound, the dead will be raised imperishable, and we will be changed.
ghafula, kufumba na kufumbua, parapanda ya mwisho itakapolia. Kwa kuwa parapanda italia, nao wafu watafufuliwa na miili isiyoharibika, nasi tutabadilishwa.
53 For the perishable must be clothed with the imperishable, and the mortal with immortality.
Kwa maana mwili huu wa kuharibika lazima uvae kutokuharibika, nao huu wa kufa lazima uvae kutokufa.
54 When the perishable has been clothed with the imperishable and the mortal with immortality, then the saying that is written will come to pass: “Death has been swallowed up in victory.”
Kwa hiyo, mwili huu wa kuharibika utakapovaa kutokuharibika, nao huu mwili wa kufa utakapovaa kutokufa, ndipo lile neno lililoandikwa litakapotimia: “Mauti imemezwa kwa kushinda.”
55 “Where, O Death, is your victory? Where, O Death, is your sting?” (Hadēs g86)
“Kuko wapi, ee mauti, kushinda kwako? Uko wapi, ee mauti, uchungu wako?” (Hadēs g86)
56 The sting of death is sin, and the power of sin is the law.
Uchungu wa mauti ni dhambi na nguvu ya dhambi ni sheria.
57 But thanks be to God, who gives us the victory through our Lord Jesus Christ!
Lakini ashukuriwe Mungu, yeye atupaye ushindi kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo.
58 Therefore, my beloved brothers, be steadfast and immovable. Always excel in the work of the Lord, because you know that your labor in the Lord is not in vain.
Kwa hiyo, ndugu zangu wapenzi, simameni imara, msitikisike, mzidi sana katika kuitenda kazi ya Bwana, kwa maana mnajua ya kuwa, kazi yenu katika Bwana si bure.

< 1 Corinthians 15 >