< Luke 6 >

1 And it came to pass, on the first sabbath after the second day of the feast, that he was going through the fields of grain; and his disciples pulled the ears and ate, rubbing them in their hands.
Siku moja ya Sabato, Yesu alikuwa anapita katika mashamba ya ngano, na wanafunzi wake wakaanza kukwanyua masuke ya ngano, wakaondoa punje zake kwa mikono, wakala.
2 And some of the Pharisees said to them: Why are you doing what it is not lawful to do on the sabbath-days?
Baadhi ya Mafarisayo wakawauliza, “Mbona mnafanya jambo ambalo si halali siku ya Sabato?”
3 And Jesus answered and said to them: Have you not read even that which David did, when he was hungry himself, and those who were with him,
Yesu akawajibu, “Je, hamjasoma jinsi alivyofanya Daudi pamoja na wenzake wakati walipokuwa na njaa?
4 that he entered the house of God, and took the loaves of the presence, and ate, and gave to those also who were with him, which it is not lawful, except for the priests alone, to eat?
Yeye aliingia ndani ya nyumba ya Mungu, akachukua ile mikate iliyowekwa mbele ya Mungu, akala na kuwapa wenzake. Kisheria, ni makuhani tu peke yao ndio walioruhusiwa kula mikate hiyo.”
5 And he said to them: The Son of man is Lord also of the sabbath.
Hivyo akawaambia, “Mwana wa Mtu ni Bwana wa Sabato.”
6 And it came to pass, on another sabbath, that he entered the synagogue and taught; and a man was there, whose right hand was withered.
Siku nyingine ya Sabato, Yesu aliingia katika sunagogi, akafundisha. Mle ndani mlikuwa na mtu ambaye mkono wake wa kuume ulikuwa umepooza.
7 And the scribes and Pharisees watched closely, whether he would heal on the sabbath-day, that they might find an accusation against him.
Walimu wa Sheria na Mafarisayo walitaka kupata kisingizio cha kumshtaki Yesu na hivyo wakawa wanangojea waone kama angemponya mtu siku ya Sabato.
8 But he knew their thoughts; and he said to the man that had the withered hand: Rise, and stand forth in the midst. And he arose, and stood.
Lakini Yesu alijua mawazo yao, akamwambia yule mwenye mkono uliopooza, “Inuka, simama katikati.” Yule mtu akaenda akasimama katikati.
9 Then Jesus said to them, I will ask you a question: Which is lawful on the sabbath, to do good, or to do evil? to save life, or to kill?
Kisha Yesu akawaambia, “Nawaulizeni, je, ni halali siku ya Sabato kutenda jambo jema au kutenda jambo baya; kuokoa maisha au kuyaangamiza?”
10 And looking round upon them all, he said to him: Stretch forth your hand. And he did so; and his hand was restored like the other.
Baada ya kuwatazama wote waliokuwa pale, akamwambia yule mtu, “Nyosha mkono wako.” Naye akafanya hivyo, na mkono wake ukawa mzima tena.
11 But they were filled with madness, and began to consult with one another what they should do to Jesus.
Lakini wao wakakasirika sana, wakajadiliana jinsi ya kumtendea Yesu maovu.
12 And it came to pass in those days, that he went out into the mountain to pray; and he spent the night in prayer to God.
Siku moja Yesu alikwenda mlimani kusali, akakesha huko usiku kucha akimwomba Mungu.
13 And when it was day, he called to him his disciples; and from them he chose twelve, whom he also named apostles:
Kesho yake aliwaita wanafunzi wake, na miongoni mwao akachagua kumi na wawili ambao aliwaita mitume:
14 Simon, whom he also named Peter, and Andrew his brother, James and John, Philip and Bartholomew,
Simoni (ambaye Yesu alimpa jina Petro) na Andrea ndugu yake, Yakobo na Yohane, Filipo na Bartholomayo,
15 Matthew and Thomas, James the son of Alphæus, and Simon who is called Zelotes,
Mathayo na Thoma, Yakobo wa Alfayo na Simoni (aliyeitwa Zelote),
16 Judas the brother of James, and Judas Iscariot, who was also the traitor.
Yuda wa Yakobo na Yuda Iskarioti ambaye baadaye alikuwa msaliti.
17 And he came down with them, and stood in a plain; and with him stood a multitude of his disciples, and a great number of people from all Judea and Jerusalem, and the sea-coast of Tyre and Sidon, who had come to hear him, and to be healed of their diseases,
Baada ya kushuka mlimani pamoja na mitume, Yesu alisimama mahali palipokuwa tambarare. Hapo palikuwa na kundi kubwa la wanafunzi wake na umati wa watu waliotoka pande zote za Yudea na Yerusalemu na pwani ya Tiro na Sidoni. Wote walifika kumsikiliza Yesu na kuponywa magonjwa yao.
18 and those who were oppressed by evil spirits; and they were cured.
Aliwaponya pia wote waliokuwa wanasumbuliwa na pepo wachafu.
19 And the whole multitude sought to touch him: for power went forth from him, and healed them all.
Watu wote walitaka kumgusa, kwa maana nguvu ilikuwa inatoka ndani yake na kuwaponya wote.
20 And he lifted up his eyes on his disciples, and said: Blessed are you that are poor, for yours is the kingdom of God.
Yesu akawageukia wanafunzi wake, akasema: “Heri ninyi mlio maskini, maana Ufalme wa Mungu ni wenu.
21 Blessed are you that hunger now, for you shall be satisfied. Blessed are you that weep now, for you shall laugh.
Heri ninyi mnaosikia njaa sasa, maana baadaye mtashiba. Heri ninyi mnaolia sasa, maana baadaye mtacheka kwa furaha.
22 Blessed are you when men shall hate you, and shall withdraw themselves from you, and reproach you, and cast out your name as evil, on account of the Son of man.
“Heri yenu ninyi iwapo watu watawachukia, watawatenga, watawatukana na kuwaharibieni jina kwa ajili ya Mwana wa Mtu!
23 Rejoice in that day, and leap for joy; for behold, your reward is great in heaven: for so did their fathers to the prophets.
Wakati hayo yatakapotokea, furahini na kucheza, maana hakika tuzo lenu ni kubwa mbinguni. Kwa maana wazee wao waliwatendea manabii vivyo hivyo.
24 But alas for you that are rich! for you have received your consolation.
Lakini ole wenu ninyi mlio matajiri, maana mmekwisha pata faraja yenu.
25 Alas for you that are full! for you shall be hungry. Alas for you that laugh now! for you shall mourn and weep.
Ole wenu ninyi mnaoshiba sasa, maana baadaye mtasikia njaa. Ole wenu ninyi mnaocheka kwa furaha sasa, maana baadaye mtaomboleza na kulia.
26 Alas for you, when men shall speak well of you! for so did their fathers to the false prophets.
Ole wenu ninyi iwapo watu wote wanawasifu, maana wazee wao waliwafanyia manabii wa uongo vivyo hivyo.
27 But I say to you that hear: Love your enemies; do good to them that hate you;
“Lakini nawaambieni ninyi mnaonisikiliza: wapendeni adui zenu, watendeeni mema wale wanaowachukieni.
28 bless them that curse you; pray for them that abuse you.
Watakieni baraka wale wanaowalaani, na waombeeni wale wanaowatendea vibaya.
29 To him that strikes you on one cheek, offer also the other; and from him that takes away your mantle, withhold not your coat.
Mtu akikupiga shavu moja mgeuzie na la pili. Mtu akikunyang'anya koti lako mwachie pia shati lako.
30 Give to every one that asks of you; and of him that takes away your goods, ask them not again.
Yeyote anayekuomba mpe, na mtu akikunyang'anya mali yako usimtake akurudishie.
31 And as you would that men should do to you, do you also in like manner to them.
Watendeeni wengine kama mnavyotaka wawatendee ninyi.
32 And if you love them that love you, what thanks have you? for even sinners love those who love them.
“Na ikiwa mnawapenda tu wale wanaowapenda ninyi, je, mtapata tuzo gani? Hakuna! Kwa maana hata wenye dhambi huwapenda wale wanaowapenda wao.
33 And if you do good to them that do good to you, what thanks have you? for even sinners do the same.
Tena, kama mkiwatendea mema wale tu wanaowatendeeni mema, mtapata tuzo gani? Hata wenye dhambi hufanya vivyo hivyo!
34 And if you lend to them from whom you hope to receive, what thanks have you? for even sinners lend to sinners, that they may receive the same.
Na kama mnawakopesha wale tu mnaotumaini watawalipeni, je, mtapata tuzo gani? Hata wenye dhambi huwakopesha wenye dhambi wenzao ili warudishiwe kima kilekile!
35 But love your enemies, and do good, and lend, hoping for nothing in return; and your reward shall be great, and you shall be sons of the Most High: for he is kind to the unthankful and the evil.
Ila nyinyi wapendeni adui zenu, na kuwatendea mema; kopesheni bila kutazamia malipo, na tuzo lenu litakuwa kubwa, nanyi mtakuwa watoto wa Mungu aliye juu. Kwa maana yeye ni mwema kwa wale wasio na shukrani na walio wabaya.
36 Be you, therefore, merciful, as your Father also is merciful.
Muwe na huruma kama Baba yenu alivyo na huruma.
37 Judge not, and you shall not be judged; condemn not, and you shall not be condemned. Forgive, and you shall be forgiven.
“Msiwahukumu wengine, nanyi hamtahukumiwa; msiwalaumu wengine, nanyi hamtalaumiwa; wasameheni wengine, nanyi mtasamehewa.
38 Give, and it shall be given to you; good measure, pressed down, shaken together, and running over, shall men give into your lap. For with the same measure with which you measure, it shall be measured to you in return.
Wapeni wengine wanavyohitaji, nanyi mtapewa. Naam, mtapokea mikononi mwenu kipimo kilichojaa, kikashindiliwa na kusukwasukwa hata kumwagika. Kwa maana kipimo kilekile mnachotumia kwa wengine ndicho ambacho Mungu atatumia kwenu.”
39 And he spoke a parable to them: Can the blind lead the blind? Will not both fall into the pit?
Akawaambia mfano huu: “Je, kipofu anaweza kumwongoza kipofu mwenzake? La! Wote wataanguka shimoni.
40 The disciple is not above his teacher; but every accomplished disciple shall be as his teacher.
Mwanafunzi hamshindi mwalimu wake, lakini kila mwanafunzi akisha hitimu huwa kama mwalimu wake.
41 And why do you look at the splinter that is in your brother’s eye, but perceive not the beam that is in your own eye?
Unawezaje kukiona kibanzi kilicho katika jicho la mwenzio, usione boriti iliyo katika jicho lako mwenyewe?
42 Or, how can you say to your brother: Brother, let me pull out the splinter that is in your eye, when you yourself see not the beam that is in your own eye? Hypocrite, first pull the beam out of your own eye, and then you shall see clearly to pull out the splinter that is in your brother’s eye.
Au, unawezaje kumwambia mwenzako, Ndugu, ngoja nikuondoe kibanzi katika jicho lako, na huku huioni boriti iliyoko katika jicho lako mwenyewe? Mnafiki wewe! Toa kwanza boriti iliyoko jichoni mwako, na hivyo utaona sawasawa kiasi cha kuweza kuondoa kibanzi kilicho katika jicho la ndugu yako.
43 For a good tree does not produce unsound fruit; nor does an unsound tree produce good fruit.
“Mti mwema hauzai matunda mabaya, wala mti mbaya hauzai matunda mazuri.
44 For every tree is known by its own fruit. For figs are not gathered from thorns, nor are grapes gathered from brambles.
Watu huutambua mti kutokana na matunda yake. Ni wazi kwamba watu hawachumi tini katika michongoma, wala hawachumi zabibu katika mbigili.
45 The good man, out of the good treasury of his heart, brings forth that which is good; and the evil man, out of the evil treasury of his heart, brings forth that which is evil. For out of the abundance of his heart his mouth speaks.
Mtu mwema hutoa yaliyo mema kutoka katika hazina bora iliyo moyoni mwake; na mtu mbaya hutoa yaliyo mabaya katika hazina mbaya iliyo moyoni mwake, kwa maana mtu huongea kutokana na yale yaliyojaa moyoni mwake.
46 But why call me Lord, Lord, and do not the things which I command?
“Mbona mwaniita Bwana, Bwana, na huku hamtimizi yale ninayosema?
47 Every one that comes to me, and hears my words, and does them, I will show you to whom he is like.
Nitawapeni mfano unaofaa kuonyesha alivyo yeyote yule anayekuja kwangu, akasikia maneno yangu na kuyatimiza:
48 He is like a man that, when building a house, digged deep, and laid the foundation on the rock. And when a flood arose, the torrent dashed against that house, and it was not able to shake it, for it was founded on the rock.
Huyo anafanana na mtu ajengaye nyumba, ambaye amechimba chini na kuweka msingi wake juu ya mwamba; kukatokea mafuriko ya mto, mkondo wa maji ukaipiga nyumba ile, lakini haukuweza kuitikisa, kwa sababu ilikuwa imejengwa imara.
49 But he that hears, and does not, is like a man that built a house upon the earth, without a foundation, against which the torrent dashed with violence, and immediately it fell, and the ruin of that house was great.
Lakini yeyote anayesikia maneno yangu lakini asifanye chochote, huyo anafanana na mtu aliyejenga nyumba juu ya udongo, bila msingi. Mafuriko ya mto yakatokea, mkondo wa maji ukaipiga nyumba ile, ikaanguka na kuharibika kabisa!”

< Luke 6 >