< Luke 10 >

1 And after these things, the Lord appointed seventy others, also, and sent them, two and two, before his face, into every city and place to which he himself was about to go.
Baada ya hayo, Bwana aliwachagua wengine sabini na wawili, akawatuma wawiliwawili, wamtangulie katika kila kijiji na mahali ambapo yeye mwenyewe alitaka kwenda.
2 He said, therefore, to them: The harvest truly is great, but the laborers are few; pray, therefore, the Lord of the harvest that he send out laborers into his harvest.
Akawaambia, “Mavuno ni mengi, lakini wavunaji ni wachache. Kwa hivyo, mwombeni mwenye shamba atume wavunaji shambani mwake.
3 Go; behold, I send you as lambs in the midst of wolves.
Sasa nendeni; fahamuni kwamba ninawatuma ninyi kama kondoo wanaokwenda kati ya mbwa mwitu.
4 Carry no purse, nor bag, nor sandals; and salute no one on the road.
Msichukue mfuko wa fedha, mkoba, wala viatu; msimsalimu mtu yeyote njiani.
5 Whatever house you enter, first say, Peace be to this house.
Mkiingia katika nyumba yoyote, kwanza wasalimuni hivi: Amani iwe katika nyumba hii!
6 And if a son of peace be there, your peace shall rest on him; but, if not, it shall return upon you.
Kama akiwako mwenye kupenda amani, amani yenu itakaa naye, la sivyo, itawarudieni.
7 And in that house remain, eating and drinking what they have to give; for the laborer is worthy of his hire; go not from house to house.
Kaeni katika nyumba hiyo mkila na kunywa wanavyowapeni, maana mfanyakazi anastahili mshahara wake. Msiende mara nyumba hii mara nyumba ile.
8 And whatever city you enter, and they receive you, eat what is set before you;
Kama mkifika mji fulani na watu wakiwakaribisha, kuleni wanavyowapeni.
9 and heal those in it who are sick, and say to them: The kingdom of God has come near to you.
Ponyeni wagonjwa walioko huko, waambieni watu: Ufalme wa Mungu umekaribia kwenu.
10 But whatever city you enter, and they receive you not, go out into the streets of it, and say:
Lakini mkiingia katika mji wowote, wasipowakaribisheni, tokeni; nanyi mpitapo katika barabara zao semeni:
11 Even the dust of your city, which cleaves to us, we do wipe off against you; yet know this, that the kingdom of God has come near to you.
Hata mavumbi ya mji wenu yaliyoshikamana na miguu yetu tunawakung'utieni. Lakini, jueni kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.
12 I say to you, It shall be more tolerable, in that day, for Sodom, than for that city.
Hakika nawaambieni, siku ile mji huo utapata adhabu kubwa zaidi kuliko ile ya watu wa Sodoma.
13 Alas for thee, Chorazin! alas for thee, Bethsaida! for, if the mighty works which have been done in you, had been done in Tyre and Sidon, they would have repented long ago, sitting in sackcloth and ashes.
“Ole wako Korazini! Ole wako Bethsaida! Maana, kama miujiza iliyofanyika kwenu ingalifanyika kule Tiro na Sidoni, watu wake wangalikwishavaa mavazi ya gunia kitambo, na kukaa katika majivu kuonyesha kwamba wametubu.
14 But for Tyre and Sidon it shall be more tolerable in the judgment, than for you.
Hata hivyo, Siku ya Hukumu ninyi mtapata adhabu kubwa zaidi kuliko ile ya watu wa Tiro na Sidoni.
15 And thou, Capernaum, who hast been exalted to heaven, shalt be brought down to hades. (Hadēs g86)
Na wewe Kafarnaumu, unataka kujikweza mpaka mbinguni? La; utaporomoshwa mpaka Kuzimu.” (Hadēs g86)
16 He that hears you, hears me; and he that rejects you, rejects me; and he that rejects me, rejects him that sent me.
Halafu akasema, “Anayewasikiliza ninyi, ananisikiliza mimi; na anayekataa kuwapokea ninyi, anakataa kunipokea mimi. Yeyote anayekataa kunipokea, anakataa kumpokea yule aliyenituma.”
17 And the seventy returned with joy, and said: Lord, even the demons are subject to us through thy name.
Baadaye, wale sabini na wawili walirudi wamejaa furaha, wakisema, “Bwana, hata pepo wametutii tulipolitaja jina lako.”
18 And he said to them: I saw Satan, like lightning from heaven, falling.
Yeye akawaambia, “Nilimwona Shetani jinsi alivyokuwa anaporomoka kama umeme kutoka mbinguni.
19 Behold, I give you authority to tread on serpents and scorpions, and authority over all the power of the enemy; and nothing shall by any means hurt you.
Naam, nimewapeni uwezo wa kukanyaga nyoka na ng'e, na uwezo juu ya nguvu zote za yule adui; hakuna chochote kitakachowadhuru.
20 However, rejoice not in this, that the spirits are subject to you; but rejoice that your names are written in heaven.
Hata hivyo, msifurahi kwa sababu pepo wamewatii, bali furahini kwa sababu majina yenu yameandikwa mbinguni.”
21 In that hour Jesus rejoiced in spirit, and said: I thank thee, Father, Lord of heaven and earth, because thou hast hid these things from the wise and prudent, and hast revealed them to babes; even so, Father, for so it seemed good in thy sight.
Saa ileile, Yesu akafurahi kwa uwezo wa Roho Mtakatifu, akasema, “Nakushukuru ee Baba, Bwana wa mbingu na dunia, kwa kuwa umewaficha wenye hekima na elimu mambo haya, ukawafumbulia wadogo. Naam, Baba, ndivyo ilivyokupendeza.”
22 All things are delivered to me by my Father; and no one knows who the Son is but the Father, and who the Father is but the Son, and he to whom the Son will reveal him.
Kisha akasema, “Baba yangu ameweka yote mikononi mwangu. Hakuna amjuaye Mwana ni nani ila Baba, wala amjuaye Baba ni nani ila Mwana, na yeyote yule ambaye Mwana anataka kumfunulia hayo.”
23 And he turned to his disciples, and said privately: Blessed are the eyes that see what you see.
Halafu akawaelekea wafuasi wake akawaambia, “Heri wanaoona yale mnayoyaona ninyi!
24 For I say to you, that many prophets and kings desired to see what you see, and did not see; and to hear what you hear, and did not hear.
Hakika, manabii na wafalme walitamani kuona yale mnayoyaona ninyi wasiyaone, na kusikia yale mnayoyasikia wasiyasikie.”
25 And, behold, a certain lawyer stood up to tempt him, and said: Teacher, what shall I do to inherit eternal life? (aiōnios g166)
Baadaye mwalimu mmoja wa Sheria alisimama akamwuliza akitaka kumtega, “Mwalimu, nifanye nini ili nipate uzima wa milele?” (aiōnios g166)
26 He said to him: What is written in the law? How do you read?
Yesu akamwuliza, “Imeandikwa nini katika Sheria? Unaelewaje?”
27 He answered and said: You shall love the Lord your God with your whole heart, and with your whole soul, and with your whole strength, and with your whole understanding, and your neighbor as yourself.
Akamjibu, “Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote, kwa nguvu zako zote na kwa akili yako yote. Na, mpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe.”
28 He said to him: You have answered correctly; do this, and you shall live.
Yesu akawaambia, “Vema! Fanya hivyo, nawe utaishi.”
29 But, wishing to justify himself, he said to Jesus: And who is my neighbor?
Lakini yeye akitaka kujihakikishia kuwa mwema akamwuliza Yesu, “Na jirani yangu ni nani?”
30 And Jesus answered and said: A certain man went down from Jerusalem to Jericho, and fell among; robbers, who stripped him of his raiment, and wounded him, and went away, leaving him half dead.
Yesu akamjibu, “Mtu mmoja alikuwa anashuka kutoka Yerusalemu kwenda Yeriko. Alipokuwa njiani, alivamiwa na majambazi, wakamnyang'anya mali yake na kumpiga, wakamwacha amelala pale nusu mfu.
31 And by chance a certain priest went down along that road, and when he saw him, he passed by on the other side.
Kumbe, kuhani mmoja akawa anapita barabara ileile, akamwona, akapita kando.
32 In like manner, also, a Levite, when he came to the place, went and looked on him, and passed by on the other side.
Hali kadhalika na Mlawi mmoja, alipofika mahali akamwona, akapita kando.
33 But a certain Samaritan, who was on a journey, came near him; and when he saw him, he had compassion on him.
Lakini Msamaria mmoja aliyekuwa anasafiri, alifika pale yule mtu alipokuwa, naye alipomwona, alimwonea huruma.
34 And he went to him, and bound up his wounds, pouring in oil and wine; and he put him on his own beast, and carried him to an inn, and took care of him.
Akamwendea, akamtibu majeraha yake kwa kumtia mafuta na divai; na kuyafunga halafu akampandisha juu ya punda wake akampeleka katika nyumba moja ya wageni akamuuguza.
35 And on the morrow, when he departed, he took out two denarii, and gave them to the innkeeper, and said to him: Take care of him; and whatever you spend more, on my return, I will repay you.
Kesho yake akatoa fedha dinari mbili akampa yule mwenye nyumba, akamwambia, Muuguze mtu huyu; na chochote utakachotumia zaidi, nitakulipa nitakaporudi.”
36 Which, then, of these three do you think was neighbor to him that fell among the robbers?
Kisha Yesu akauliza, “Kati ya hao watatu, ni yupi aliyeonyesha kuwa jirani yake yule aliyevamiwa na majambazi?”
37 He replied: He that showed mercy to him. Jesus said to him: Go, and do you likewise.
Yule mwalimu wa Sheria akamjibu, “Ni yule aliyemwonea huruma.” Yesu akamwambia, “Nenda ukafanye vivyo hivyo.”
38 And it came to pass, as they continued their journey, that he entered a certain village, and a certain woman named Martha received him into her house.
Walipokuwa safarini, waliingia katika kijiji kimoja na mwanamke mmoja, aitwaye Martha, alimkaribisha nyumbani kwake.
39 And she had a sister called Mary, who also sat at the feet of Jesus, and heard his word.
Martha alikuwa na dada yake aitwaye Maria; huyu aliketi karibu na Yesu akisikiliza mafundisho yake.
40 But Martha made herself busy with much serving; and she came to him, and said: Lord, dost thou not care that my sister has left me to serve alone? Bid her, therefore, that she help me.
Lakini Martha alikuwa anashughulika na mambo mengi. Basi, akamwendea Yesu, akamwambia, “Bwana, hivi hujali kwamba dada yangu ameniacha nishughulike peke yangu? Mwambie basi, anisaidie.”
41 But Jesus answered and said to her: Martha, Martha, you are anxious and troubled about many things:
Lakini Bwana akamjibu, “Martha, Martha, unahangaika na kusumbuka kwa mambo mengi.
42 one thing is needful; and Mary has chosen the good part, which shall not be taken from her.
Kitu kimoja tu ni muhimu. Maria amechagua kitu bora zaidi ambacho hakuna mtu atakayemnyag'anya.”

< Luke 10 >