< John 20 >

1 And early on the first day of the week, while it was yet dark, Mary Magdalene came to the tomb, and saw that the stone had been taken away from the tomb.
Alfajiri na mapema Jumapili, kukiwa bado na giza, Maria Magdalene alikwenda kaburini, akaliona lile jiwe limeondolewa mlangoni pa kaburi.
2 Then she ran and came to Simon Peter, and to the other disciple whom Jesus loved, and said to them: They have taken away the Lord out of the tomb, and we know not where they have laid him.
Basi, akaenda mbio hadi kwa Petro na yule mwanafunzi mwingine ambaye Yesu alimpenda, akawaambia, “Wamemwondoa Bwana kaburini, na wala hatujui walikomweka.”
3 Then Peter and the other disciple went out, and came to the tomb.
Petro pamoja na yule mwanafunzi mwingine wakaenda kaburini.
4 And the two ran together; and the other disciple outran Peter, and came first to the tomb;
Wote wawili walikimbia lakini yule mwanafunzi mwingine alikimbia mbio zaidi kuliko Petro, akatangulia kufika kaburini.
5 and he stooped down and saw the linen cloths lying, but he did not go in.
Alipoinama na kuchungulia ndani, aliona sanda, lakini hakuingia ndani.
6 Then came Simon Peter, following him; and he went into the tomb, and saw the linen cloths lying,
Simoni Petro naye akaja akimfuata, akaingia kaburini; humo akaona sanda,
7 and the handkerchief that had been on his head, not lying with the linen cloths, but folded in a place by itself.
na kile kitambaa alichofungwa Yesu kichwani. Hicho kitambaa hakikuwekwa pamoja na hiyo sanda, bali kilikuwa kimekunjwa na kuwekwa mahali peke yake.
8 Then, therefore, the other disciple, who came first to the tomb, went in, and saw, and believed.
Kisha yule mwanafunzi mwingine aliyemtangulia kufika kaburini, akaingia pia ndani, akaona, akaaamini.
9 For, as yet, they did not know the scripture, that he must rise from the dead.
(Walikuwa bado hawajaelewa Maandiko Matakatifu yaliyosema kwamba ilikuwa lazima afufuke kutoka wafu).
10 Then the disciples went away again by themselves.
Basi, hao wanafunzi wakarudi nyumbani.
11 But Mary stood without near the tomb, weeping; and as she wept, she stooped down and looked into the tomb,
Maria alikuwa amesimama nje ya kaburi, akilia. Huku akiwa bado analia, aliinama na kuchungulia kaburini,
12 and saw two angels in white raiment, sitting, the one at the head, and the other at the foot, where the body of Jesus had lain.
akawaona malaika wawili waliovaa mavazi meupe, wameketi pale mwili wa Yesu ulipokuwa umelazwa, mmoja kichwani na wa pili miguuni.
13 And they said to her: Woman, why do you weep? She said to them: They have taken away my Lord, and I know not where they have laid him.
Hao malaika wakamwuliza, “Mama, kwa nini unalia?” Naye akawaambia, “Wamemwondoa Bwana wangu, na wala sijui walikomweka!”
14 Having said this, she turned back, and saw Jesus standing, and knew not that it was Jesus.
Baada ya kusema hayo, aligeuka nyuma, akamwona Yesu amesimama hapo, lakini asitambue ya kuwa ni Yesu.
15 Jesus said to her: Woman, why do you weep? Whom do you seek? Supposing that it was the gardener, she said to him: Sir, if you have taken him hence, tell me where you have laid him, and I will take him away.
Yesu akamwuliza, “Mama, kwa nini unalia? Unamtafuta nani?” Maria, akidhani kwamba huyo ni mtunza bustani, akamwambia, “Mheshimiwa, kama ni wewe umemwondoa, niambie ulikomweka, nami nitamchukua.”
16 Jesus said to her: Mary. She turned, and said to him: Rabboni; which is, translated, Teacher.
Yesu akamwambia, “Maria!” Naye Maria akageuka, akamwambia kwa Kiebrania, “Raboni” (yaani “Mwalimu”).
17 Jesus said to her: Touch me not, for I have not yet ascended to my Father: but go to my brethren, and say to them, I ascend to my Father and your Father, and to my God and your God.
Yesu akamwambia, “Usinishike; sijakwenda bado juu kwa Baba. Lakini nenda kwa ndugu zangu uwaambie: nakwenda juu kwa Baba yangu na Baba yenu, Mungu wangu na Mungu wenu.”
18 Mary Magdalen came and told the disciples that she had seen the Lord, and that he had said these things to her.
Hivyo Maria Magdalene akaenda akawapa habari wale wanafunzi kuwa amemwona Bwana, na kwamba alikuwa amemwambia hivyo.
19 Then, on that day, the first day of the week, when it was evening, and the doors of the house in which the disciples were assembled had been closed for fear of the Jews, Jesus came and stood in the midst, and said to them: Peace be to you.
Ilikuwa jioni ya siku hiyo ya Jumapili. Wanafunzi walikuwa wamekutana pamoja ndani ya nyumba, na milango ilikuwa imefungwa kwa sababu waliwaogopa viongozi wa Wayahudi. Basi, Yesu akaja, akasimama kati yao, akawaambia, “Amani kwenu!”
20 And having said this, he showed them his hands and his side. Then the disciples rejoiced, when they saw the Lord.
Alipokwisha sema hayo, akawaonyesha mikono yake na ubavu wake. Basi, hao wanafunzi wakafurahi mno kumwona Bwana.
21 Then Jesus said to them again: Peace be to you. As my Father has sent me, so I send you.
Yesu akawaambia tena, “Amani kwenu! Kama vile Baba alivyonituma mimi, nami nawatuma ninyi.”
22 And when he had said this, he breathed on them, and said to them: Receive the Holy Spirit.
Alipokwisha sema hayo, akawapulizia na kuwaambia, “Pokeeni Roho Mtakatifu.
23 Whosever sins you forgive, they are forgiven them: whosever sins you retain, they are retained.
Mkiwasamehe watu dhambi zao, wamesamehewa; msipowaondolea, hawasamehewi.”
24 But Thomas, one of the twelve, who is called Didymus, was not with them when Jesus came.
Thoma mmoja wa wale kumi na wawili (aitwaye Pacha), hakuwa pamoja nao wakati Yesu alipokuja.
25 Then the other disciples said to him: We have seen the Lord. But he said to them: Unless I see in his hands the print of the nails, and put my finger in the print of the nails, and put my hand into his side, I will not believe.
Basi, wale wanafunzi wengine wakamwambia, “Tumemwona Bwana.” Thoma akawaambia, “Nisipoona mikononi mwake alama za misumari, na kutia kidole changu katika kovu hizo, na kutia mkono wangu ubavuni mwake, sitasadiki.”
26 And after eight days, again his disciples were within, and Thomas was with them. Then Jesus came, though the doors had been closed, and stood in the midst, and said: Peace be to you.
Basi, baada ya siku nane hao wanafunzi walikuwa tena pamoja mle ndani, na Thoma alikuwa pamoja nao. Milango ilikuwa imefungwa, lakini Yesu akaja, akasimama kati yao, akasema, “Amani kwenu!”
27 Then he said to Thomas: Reach hither your finger, and behold my hands; and reach hither your hand, and put it into my side; and be not faithless, but believing.
Kisha akamwambia Thoma, “Lete kidole chako hapa uitazame mikono yangu; lete mkono wako ukautie ubavuni mwangu. Usiwe na mashaka, ila amini!”
28 And Thomas answered and said to him: My Lord and my God.
Thoma akamjibu, “Bwana wangu na Mungu wangu!”
29 Jesus said to him: Because you have seen me you have believed: blessed are they who, though they have not seen, yet have believed.
Yesu akamwambia, “Je, unaamini kwa kuwa umeniona? Heri yao wale ambao hawajaona, lakini wameamini.”
30 Many other signs truly did Jesus in the presence of his disciples, which are not written in this book;
Yesu alifanya mbele ya wanafunzi wake ishara nyingine nyingi ambazo hazikuandikwa katika kitabu hiki.
31 but these are written, that you may believe that Jesus is the Christ, the Son of God, and that by believing you may have life through his name.
Lakini hizi zimeandikwa ili mpate kuamini kwamba Yesu ni Kristo, Mwana wa Mungu; na kwa kuamini mpate kuwa na uzima kwa nguvu ya jina lake.

< John 20 >