< Hebrews 2 >

1 Therefore, we ought to give the more earnest heed to the things which we have heard, lest we let them glide away.
Kwa sababu hiyo tunapaswa kuzingatia kwa makini zaidi yote tuliyosikia, ili tusije tukapotoshwa.
2 For if the word spoken by angels was steadfast, and every transgression and disobedience received a just punishment,
Ujumbe ule waliopewa wazee wetu na malaika ulionyeshwa kuwa kweli, hata mtu yeyote ambaye hakuufuata au hakuutii aliadhibiwa kama alivyostahili.
3 how shall we escape, if we neglect so great salvation? which at first began to be spoken by the Lord, and was confirmed to us by those who heard him;
Basi, sisi tutaokokaje kama hatuujali wokovu mkuu kama huu? Kwanza Bwana mwenyewe aliutangaza wokovu huu, na wale waliomsikia walituthibitishia kwamba ni kweli.
4 God also bearing testimony with them by signs and wonders, and by various mighty deeds, and by distributions of the Holy Spirit, according to his own will.
Mungu pia aliongeza hapo ushahidi wake kwa kufanya kila namna ya miujiza na maajabu, na kwa kuwagawia watu vipaji vya Roho Mtakatifu kadiri ya mapenzi yake.
5 For not to angels has he subjected the world to come of which we speak.
Mungu hakuwaweka malaika wautawale ulimwengu ujao, yaani ulimwengu ule tunaoongea habari zake.
6 But one in a certain place testified, saying: What is man, that thou art mindful of him; or the son of man, that thou dost visit him?
Tena yasemwa mahali fulani katika Maandiko: “Mtu ni nini ee Mungu, hata umfikirie; mwanaadamu ni nini hata umjali?
7 Thou hast made him a little lower than the angels; thou hast crowned him with glory and honor;
Ulimfanya kwa kitambo kidogo kuwa chini zaidi kuliko malaika; ukamvika taji ya utukufu na heshima,
8 thou hast put all things under his feet. For, in putting all things under him, he left nothing that is not put under him: but now we do not yet see all things put under him.
ukaweka kila kitu chini ya miguu yake, avitawale.” Yasemwa kwamba Mungu alimweka mtu kuwa mtawala wa vitu vyote yaani bila kuacha hata kimoja. Hata hivyo, hatuoni bado mtu akivitawala vitu vyote sasa.
9 But we see Jesus, who was made a little lower than the angels, that he might, by the grace of God, taste death for every man―we see him, on account of his having suffered death, crowned with glory and honor.
Lakini twamwona Yesu ambaye alifanywa kwa kitambo kidogo kuwa chini zaidi kuliko malaika, ili kwa neema ya Mungu afe kwa ajili ya watu wote. Sasa tunamwona ametawazwa kwa utukufu na heshima kwa sababu ya kifo alichoteseka.
10 For it became him, for whom are all things, and by whom are all things, in bringing many sons to glory, to make the author of their salvation perfect through sufferings.
Ilikuwa haki tupu kwamba Mungu, ambaye huumba na kutegemeza vitu vyote, alimfanya Yesu kuwa mkamilifu kabisa kwa njia ya mateso, ili awalete watoto wengi waushiriki utukufu wake. Maana Yesu ndiye anayewaongoza kwenye wokovu.
11 For both he that sanctifies, and those who are sanctified, are all of one Father: for which reason, he is not ashamed to call them brethren, saying:
Yeye anawatakasa watu dhambi zao, naye pamoja na wale waliotakaswa, wote wanaye Baba mmoja. Ndiyo maana Yesu haoni aibu kuwaita hao ndugu zake;
12 I will declare thy name among my brethren; in the midst of the assembly, will I sing hymns to thee.
kama asemavyo: “Ee Mungu, nitawatangazia ndugu zangu matendo yako. Nitakusifu katika kusanyiko lao.”
13 And again: I will put my trust in him. And again: Behold, I, and the children that God has given me.
Tena asema: “Nitamwekea Mungu tumaini langu.” Na tena: “Mimi niko hapa pamoja na watoto alionipa Mungu.”
14 Since, then, the children are partakers of flesh and blood, he also, in like manner, partook of the same, that, through his death, he might deprive of power him that has the power of death, that is, the devil;
Basi, kwa vile watoto hao, kama awaitavyo, ni watu wenye mwili na damu, Yesu mwenyewe akawa kama wao na kushiriki ubinadamu wao. Alifanya hivyo ili kwa njia ya kifo chake amwangamize Ibilisi, ambaye ana mamlaka juu ya kifo,
15 and might set free those who, through fear of death, were all their lifetime subject to bondage.
na hivyo awaokoe wale waliokuwa watumwa maisha yao yote kwa sababu ya hofu yao ya kifo.
16 For, verily, he does not take hold of angels, but he takes hold of the posterity of Abraham.
Maana ni wazi kwamba yeye hakuja kwa ajili ya kuwasaidia malaika, bali kama yasemavyo Maandiko; “Anawasaidia wazawa wa Abrahamu.”
17 Wherefore, it behooved him to be made like his brethren in all things, that he might be a merciful and faithful high priest in things pertaining to God, in order to make expiation for the sins of the people.
Ndiyo maana ilimbidi awe kama ndugu zake kwa kila namna, ili awe Kuhani Mkuu wao aliye mwaminifu na mwenye huruma katika kumtumikia Mungu, ili dhambi za watu ziondolewe.
18 For, inasmuch as he himself has suffered in being tempted, he is able to help those who are tempted.
Na, anaweza sasa kuwasaidia wale wanaojaribiwa na kuteswa.

< Hebrews 2 >