< 3 John 1 >

1 The elder to the beloved Gaius, whom I love in the truth.
Mimi mzee nakuandikia wewe Gayo, rafiki yangu, ninayekupenda kweli.
2 Beloved, I pray above all things that you may prosper and be in health, even as your soul prospers.
Mpenzi wangu, nakutakia mafanikio mema ya kila aina; nakutakia afya njema ya mwili kama ulivyo nayo rohoni.
3 For I rejoiced greatly when the brethren came and testified to the truth that is in you, even as you walk in the truth.
Nimefurahi sana ndugu kadhaa walipofika hapa, wakaiambia juu ya uaminifu wako kuhusu ukweli; naam, wewe unaishi daima katika ukweli.
4 I have no greater joy than to hear that my children walk in the truth.
Hakuna kitu kinachonifurahisha zaidi kuliko kusikia kwamba watoto wangu wanaishi katika ukweli.
5 Beloved, you do faithfully whatever you do to the brethren, and to strangers,
Mpenzi wangu, wewe ni mwaminifu kila mara unapowahudumia ndugu, hata kama ni wageni.
6 who have testified to your love before the church: if you conduct these on their journey, in a manner worthy of God, you will do well:
Ndugu hao wamelieleza kanisa hapa habari za upendo wako. Tafadhali uwasaidie waendelee na safari yao kwa namna itakayompendeza Mungu,
7 for, on account of his name, they went out, taking nothing from the Gentiles.
Maana wanaanza safari yao katika utumishi wa Kristo bila kupokea msaada wowote kutoka kwa watu wasioamini.
8 We, therefore, ought to receive such, that we may be fellow-helpers to the truth.
Basi, sisi tunapaswa kuwasaidia watu hawa, ili nasi tupate kushiriki katika kazi yao kwa ajili ya ukweli.
9 I wrote to the church; but Diotrephes, who loves to have the pre-eminence among them, receives us not.
Niliandika barua fupi kwa hilo kanisa; lakini Diotrefe, ambaye hupenda kuwa kiongozi wao, hataki kabisa kunisikiliza.
10 Therefore, if I come, I will remember his works which he does, prating against us with malicious words: and not content with these things, he does not himself receive the brethren, but both forbids those who are willing, and casts them out of the church.
Basi, nitakapokuja nitayafichua mambo yote anayofanya, maneno mabaya anayotutolea na uongo anaosema juu yetu. Isitoshe, yeye hukataa kuwakaribisha hao ndugu walio safarini, na hata huwazuia watu wengine wanaotaka kuwakaribisha, na hujaribu kuwafukuzia nje ya kanisa.
11 Beloved, do not imitate that which is evil, but that which is good. He that does good is of God: he that does evil has not seen God.
Mpenzi wangu, usifuate mfano mbaya, bali mfano mwema. Kila atendaye mema ni wa Mungu; lakini anayetenda mabaya hajapata kumwona Mungu.
12 A good report is given of Demetrius by all, and by the truth itself: and we also give our testimony, and you know that our testimony is true.
Kila mtu anamsifu Demetrio; naam, ukweli wenyewe unamsifu. Nasi pia tunatoa ushahidi wetu juu yake, nawe wajua kwamba tunachosema ni kweli.
13 I had many things to write, but I will not communicate them to you with ink and pen.
Ninayo bado mengi ya kukwambia, lakini sipendi kuyaandika kwa kalamu na wino.
14 But I trust that I shall shortly see you, and we will speak mouth to mouth. Peace be to you. Our friends here salute you. Salute our friends with you by name.
Natumaini kukuona karibuni na hapo tutazungumza ana kwa ana. Nakutakia amani. Rafiki zako wanakusalimu. Wasalimu rafiki zetu wote kila mmoja binafsi.

< 3 John 1 >