< 1 Peter 1 >

1 Peter, an apostle of Jesus Christ, to the sojourners that are dispersed through Pontus, Galatia, Cappadocia, Asia, and Bithynia,
Mimi Petro, mtume wa Yesu Kristo nawaandikia ninyi wateule wa Mungu Baba, ambao mmetawanyika na mnaishi kama wakimbizi huko Ponto, Galatia, Kapadokia, Asia na Bithunia.
2 elect according to the foreknowledge of God the Father, by the sanctification of the Spirit, in order to obedience, and sprinkling of the blood of Jesus Christ: grace be to you, and peace be multiplied.
Mungu Baba aliwateua ninyi kufuatana na kusudi lake, na mmefanywa watakatifu na Roho, mpate kumtii Yesu Kristo na kusafishwa kwa damu yake. Nawatakieni neema na amani tele.
3 Blessed be the God and Father of our Lord Jesus Christ, who, according to his abundant mercy, has, by the resurrection of Jesus Christ from the dead, regenerated us for a living hope
Asifiwe Mungu na Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo! Kwa huruma yake kuu alitufanya tuzaliwe upya kwa kumfufua Yesu kutoka wafu. Ametujalia tumaini lenye uzima,
4 in respect to an inheritance incorruptible, and undefiled, and that fades not away, reserved in heaven for us,
na hivyo tunatazamia kupata baraka zile ambazo Mungu aliwawekea watu wake. Mungu amewawekeeni baraka hizo mbinguni ambako haziwezi kuoza au kuharibika au kufifia.
5 who are kept secure by the power of God through faith, to a salvation ready to be revealed in the last time:
Hizo zitakuwa zenu ninyi ambao kwa imani mnalindwa salama kwa nguvu ya Mungu kwa ajili ya wokovu ambao uko tayari kufunuliwa mwishoni mwa nyakati.
6 in which you rejoice, though now for a little while, since it is needful, you are in sorrow under various temptations;
Furahini kuhusu jambo hilo, ijapokuwa sasa, kwa kitambo kidogo, itawabidi kuhuzunika kwa sababu ya majaribio mbalimbali mnayoteseka.
7 that your faith, when proved, being much more precious than gold, which perishes though it be tried by fire, may be found to be for praise and honor and glory, at the revelation of Jesus Christ;
Shabaha yake ni kuthibitisha imani yenu. Hata dhahabu yenyewe ambayo huharibika, hujaribiwa kwa moto; hali kadhalika na imani yenu ambayo ni ya thamani zaidi kuliko dhahabu, ni lazima ijaribiwe ipate kuwa thabiti. Hapo mtapokea sifa na utukufu na heshima Siku ile Yesu Kristo atakapofunuliwa.
8 whom, though you have not seen him, yet you love; on whom not now looking, but believing, you rejoice with joy unspeakable, and full of glory,
Ninyi mnampenda ingawaje hamjamwona, na mnamwamini ingawa hamumwoni sasa. Hivyo, mnafurahi kwa furaha tukufu isiyoelezeka,
9 receiving the end of your faith, the salvation of your souls.
kwa sababu mnapokea wokovu wa roho zenu ambao ni lengo la imani yenu.
10 Concerning which salvation the prophets that prophesied of the grace that should be for you, did inquire, and search diligently,
Manabii walipeleleza kwa makini na kufanya uchunguzi juu ya wokovu huo, wakabashiri juu ya neema hiyo ambayo ninyi mngepewa.
11 inquiring what things, and what time, the Spirit of Christ that was in them did signify, when it testified, beforehand, the sufferings of Christ, and the glories that should follow them;
Walijaribu kujua nyakati na mazingira ya tukio hilo, yaani wakati alioudokezea Roho wa Kristo aliyekuwa ndani yao, akibashiri juu ya mateso yatakayompata Kristo na utukufu utakaofuata.
12 to whom it was revealed, that, not for themselves, but for us, they ministered the things that are now preached to you by those who have made known to you the gospel, through the Holy Spirit sent down from heaven; into which things angels desire to look.
Mungu aliwafunulia kwamba wakati walipokuwa wanasema juu ya hayo mambo ambayo ninyi mmekwisha sikia sasa kutoka kwa wale wajumbe waliowatangazieni Habari Njema kwa nguvu ya Roho Mtakatifu aliyetumwa kutoka mbinguni, hiyo kazi yao haikuwa kwa faida yao wenyewe, bali kwa ajili yenu. Hayo ndiyo mambo ambayo hata malaika wangependa kuyafahamu.
13 Wherefore, gird up the loins of your mind; be watchful, and hope constantly for the grace that is to be brought to you at the revelation of Jesus Christ:
Kwa hiyo, basi, muwe tayari kabisa kwa nia, na kukesha. Wekeni tumaini lenu lote katika baraka ile mtakayopewa wakati Yesu Kristo atakapoonekana!
14 as obedient children, not conforming yourselves to the desires which you formerly had in your ignorance;
Kama watoto wa Mungu wenye utii, msikubali kamwe kufuata tena tamaa mbaya mlizokuwa nazo wakati mlipokuwa wajinga.
15 but as he who has called you is holy, so be you holy in all your behavior:
Bali mnapaswa kuwa watakatifu katika mwenendo wenu wote, kama vile yule aliyewaiteni ni mtakatifu.
16 because it is written, Be you holy, for I am holy.
Maandiko yasema: “Muwe watakatifu, kwa kuwa mimi ni mtakatifu.”
17 And since you call on the Father, who, without respect of persons, judges according to every man’s work, pass the time of your sojourning in fear:
Mnapomtaja Mungu ninyi humwita Baba. Basi, jueni kwamba yeye humhukumu kila mmoja kadiri ya matendo yake, bila ubaguzi. Hivyo tumieni wakati wenu uliowabakia hapa ugenini katika kumcha Mungu.
18 because you know that you were not redeemed with corruptible things, as silver or gold, from your vain mode of life received by tradition from your fathers,
Maana mnajua kwamba ninyi mlikombolewa katika mwenendo wenu usiofaa ambao mliupokea kutoka kwa wazee wenu, si kwa vitu vyenye kuharibika: kwa fedha na dhahabu;
19 but with the precious blood of Christ, as of a lamb without spot and blemish,
bali mlikombolewa kwa damu tukufu ya Kristo, ambaye alikuwa kama mwana kondoo asiye na dosari wala doa.
20 who was indeed foreordained before the foundation of the world, but manifested in these last times for you,
Yeye alikuwa ameteuliwa na Mungu kabla ya ulimwengu kuumbwa, akafunuliwa siku hizi za mwisho kwa ajili yenu.
21 who through him do believe in God who raised him from the dead, and gave him glory, that your faith and hope might be in God.
Kwa njia yake, ninyi mnamwamini Mungu aliyemfufua kutoka wafu na kumpa utukufu; na hivyo imani na matumaini yenu yako kwa Mungu.
22 Having purified your souls in obeying the truth through the Spirit, to unfeigned love of the brethren, love one another with a pure heart fervently,
Maadamu sasa, kwa kuutii ukweli, ninyi mmezitakasa roho zenu na kuwapenda wenzenu bila unafiki, basi, pendaneni kwa moyo wote.
23 having been begotten again, not with corruptible seed, but with incorruptible, by the word of God, which lives and abides forever. (aiōn g165)
Maana kwa njia ya neno hai la Mungu, ninyi mmezaliwa upya, si kama watoto wa baba awezaye kufa, bali baba asiyekufa milele. (aiōn g165)
24 For all flesh is as grass, and all the glory of man as the flower of grass; the grass withers, and its flower fails away:
Kama Maandiko yasemavyo: “Kila binadamu ni kama nyasi, na utukufu wake wote ni kama maua ya porini. Nyasi hunyauka na maua huanguka.
25 but the word of the Lord abides forever: and this is the word which has been preached as gospel to you. (aiōn g165)
Lakini neno la Bwana hudumu milele.” Neno hilo ni hiyo Habari Njema iliyohubiriwa kwenu. (aiōn g165)

< 1 Peter 1 >