< Psalms 6 >
1 For the Chief Musician; on stringed instruments, set to the Sheminith. A Psalm of David. O Jehovah, rebuke me not in thine anger, Neither chasten me in thy hot displeasure.
Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za muziki. Mtindo wa sheminithi. Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, usinikemee katika hasira yako, wala usiniadhibu katika ghadhabu yako.
2 Have mercy upon me, O Jehovah; for I am withered away: O Jehovah, heal me; for my bones are troubled.
Unirehemu Bwana, kwa maana nimedhoofika; Ee Bwana, uniponye, kwa maana mifupa yangu ina maumivu makali.
3 My soul also is sore troubled: And thou, O Jehovah, how long?
Nafsi yangu ina uchungu mwingi. Mpaka lini, Ee Bwana, mpaka lini?
4 Return, O Jehovah, deliver my soul: Save me for thy lovingkindness’ sake.
Geuka Ee Bwana, unikomboe, uniokoe kwa sababu ya fadhili zako.
5 For in death there is no remembrance of thee: In Sheol who shall give thee thanks? (Sheol )
Hakuna mtu anayekukumbuka akiwa amekufa. Ni nani awezaye kukusifu akiwa kuzimu? (Sheol )
6 I am weary with my groaning; Every night make I my bed to swim; I water my couch with my tears.
Nimechakaa kwa kulia kwa huzuni; usiku kucha nafurikisha kitanda changu kwa machozi; nimelowesha viti vyangu vya fahari kwa machozi.
7 Mine eye wasteth away because of grief; It waxeth old because of all mine adversaries.
Macho yangu yamedhoofika kwa kuhuzunika, yamedhoofika kwa sababu ya adui zangu wote.
8 Depart from me, all ye workers of iniquity; For Jehovah hath heard the voice of my weeping.
Kaeni mbali nami, ninyi nyote mtendao mabaya, kwa maana Bwana amesikia kulia kwangu.
9 Jehovah hath heard my supplication; Jehovah will receive my prayer.
Bwana amesikia kilio changu kwa huruma, Bwana amekubali sala yangu.
10 All mine enemies shall be put to shame and sore troubled: They shall turn back, they shall be put to shame suddenly.
Adui zangu wote wataaibika na kufadhaika, watarudi nyuma kwa aibu ya ghafula.