< Proverbs 19 >
1 Better is the poor that walketh in his integrity Than he that is perverse in his lips and is a fool.
Bora mtu masikini ambaye huenenda katika uadilifu wake kuliko mwenye ukaidi katika maneno yake na ni mpumbavu.
2 Also, that the soul be without knowledge is not good; And he that hasteth with his feet sinneth.
Tena, si vizuri kuwa na hamu bila maarifa na mwenye kukimbia haraka sana hukosea njia.
3 The foolishness of man subverteth his way; And his heart fretteth against Jehovah.
Upuuzi wa mtu unaharibu maisha yake na moyo wake hughadhabika dhidi ya Yehova.
4 Wealth addeth many friends; But the poor is separated from his friend.
Utajiri huongeza marafiki wengi, bali mtu masikini hutengwa na rafiki zake.
5 A false witness shall not be unpunished; And he that uttereth lies shall not escape.
Shahidi wa uongo hatakosa adhabu na mwenye kupumua uongo hataokoka.
6 Many will entreat the favor of the liberal man; And every man is a friend to him that giveth gifts.
Wengi wataomba fadhila kutoka kwa mtu mkarimu na kila mtu ni rafiki wa yule anayetoa zawadi.
7 All the brethren of the poor do hate him: How much more do his friends go far from him! He pursueth [them with] words, [but] they are gone.
Mtu masikini huchukiwa na ndugu zake wote; je marafiki wengi kiasi gani hujitenga kutoka kwake! Anawaita, lakini wameondoka.
8 He that getteth wisdom loveth his own soul: He that keepeth understanding shall find good.
Anayepata hekima huyapenda maisha yake mwenyewe; yeye atunzaye ufahamu atapata kilicho chema.
9 A false witness shall not be unpunished; And he that uttereth lies shall perish.
Shahidi wa uongo hatakosa kuadhibiwa, bali mwenye kupumua uongo ataangamia.
10 Delicate living is not seemly for a fool; Much less for a servant to have rule over princes.
Haifai kwa mpumbavu kuishi kwa anasa- wala kwa mtumwa kutawala juu ya wafalme.
11 The discretion of a man maketh him slow to anger; And it is his glory to pass over a transgression.
Busara humfanya mtu achelewe kukasirika na utukufu wake ni kusamehe kosa.
12 The king’s wrath is as the roaring of a lion; But his favor is as dew upon the grass.
Ghadhabu ya mfalme ni kama muungurumo wa simba kijana, bali fadhila yake ni kama umande kwenye majani.
13 A foolish son is the calamity of his father; And the contentions of a wife are a continual dropping.
Mwana mpumbavu ni uharibifu kwa baba yake na mke mgomvi ni maji yanayochuruzika daima.
14 House and riches are an inheritance from fathers; But a prudent wife is from Jehovah.
Nyumba na utajiri ni urithi kutoka kwa wazazi, bali mke mwenye busara hutoka kwa Yehova.
15 Slothfulness casteth into a deep sleep; And the idle soul shall suffer hunger.
Uvivu unamtupa mtu kwenye usingizi mzito, bali asiyetamani kufanya kazi atakwenda njaa.
16 He that keepeth the commandment keepeth his soul; [But] he that is careless of his ways shall die.
Yeye anayetii amri huyaongoza maisha yake, bali mtu asiyefikiri juu ya njia zake atakufa.
17 He that hath pity upon the poor lendeth unto Jehovah, And his good deed will he pay him again.
Mwenye ukarimu kwa masikini humkopesha Yehova na atalipwa kwa kile alichofanya.
18 Chasten thy son, seeing there is hope; And set not thy heart on his destruction.
Mrudi mwanao wakati kuna matumaini na usiwe na shauku ya kumweka katika mauti.
19 A man of great wrath shall bear the penalty; For if thou deliver [him], thou must do it yet again.
Mtu mwenye hasira kali lazima alipe adhabu; kama ukimwokoa, utafanya hivyo mara mbili.
20 Hear counsel, and receive instruction, That thou mayest be wise in thy latter end.
Sikiliza ushauri na ukubali maelekezo, ili uweze kuwa na hekima mwishoni mwa maisha yako.
21 There are many devices in a man’s heart; But the counsel of Jehovah, that shall stand.
Moyoni mwa mtu kuna mipango mingi, bali kusudi la Yehova ndilo litakalo simama.
22 That which maketh a man to be desired is his kindness; And a poor man is better than a liar.
Shauku ya mtu ni uaminifu na mtu masikini ni bora kuliko muongo.
23 The fear of Jehovah [tendeth] to life; And he [that hath it] shall abide satisfied; He shall not be visited with evil.
Kumheshimu Yehova huwaelekeza watu kwenye uzima; mwenye nayo atashibishwa na hatadhurika kwa madhara.
24 The sluggard burieth his hand in the dish, And will not so much as bring it to his mouth again.
Mtu goigoi huuzika mkono wake ndani ya dishi; hataurudisha juu ya kinywa chake.
25 Smite a scoffer, and the simple will learn prudence; And reprove one that hath understanding, [and] he will understand knowledge.
Kama utampiga mwenye mzaha, wajinga watakuwa na hekima; mwelekeze mwenye ufahamu, naye atapata maarifa.
26 He that doeth violence to his father, and chaseth away his mother, Is a son that causeth shame and bringeth reproach.
Anayempora baba yake na kumfukuza mama yake ni mwana anayeleta aibu na shutuma.
27 Cease, my son, to hear instruction [Only] to err from the words of knowledge.
Mwanangu, kama utaacha kusikiliza maelekezo, utapotea kutoka kwenye maneno ya maarifa.
28 A worthless witness mocketh at justice; And the mouth of the wicked swalloweth iniquity.
Shahidi mpotofu huidhihaki haki na kinywa cha waovu humeza uovu.
29 Judgments are prepared for scoffers, And stripes for the back of fools.
Hukumu ipo tayari kwa wenye dhihaka na mjeledi kwa migongo ya wapumbavu.