< Luke 1 >

1 Forasmuch as many have taken in hand to draw up a narrative concerning those matters which have been fulfilled among us,
Kwa kuwa watu wengi wamekaa ili kuandika habari za mambo yaliyotukia katikati yetu,
2 even as they delivered them unto us, who from the beginning were eyewitnesses and ministers of the word,
kama vile yalivyokabidhiwa kwetu na wale waliokuwa mashahidi walioyaona na watumishi wa Bwana,
3 it seemed good to me also, having traced the course of all things accurately from the first, to write unto thee in order, most excellent Theophilus;
mimi nami baada ya kuchunguza kila kitu kwa uangalifu kuanzia mwanzo, niliamua kukuandikia habari za mambo hayo, ewe mtukufu Theofilo,
4 that thou mightest know the certainty concerning the things wherein thou wast instructed.
ili upate kujua ukweli kuhusu yale uliyofundishwa.
5 There was in the days of Herod, king of Judæa, a certain priest named Zacharias, of the course of Abijah: and he had a wife of the daughters of Aaron, and her name was Elisabeth.
Wakati wa Herode mfalme wa Uyahudi, palikuwa na kuhani mmoja jina lake Zekaria, ambaye alikuwa wa ukoo wa kikuhani wa Abiya. Elizabeti mkewe alikuwa pia mzao wa Aroni.
6 And they were both righteous before God, walking in all the commandments and ordinances of the Lord blameless.
Zekaria na Elizabeti mkewe wote walikuwa watu wanyofu mbele za Mungu, wakizishika amri zote za Bwana na maagizo yote bila lawama.
7 And they had no child, because that Elisabeth was barren, and they both were [now] well stricken in years.
Lakini walikuwa hawana watoto, kwa sababu Elizabeti alikuwa tasa; nao wote wawili walikuwa wazee sana.
8 Now it came to pass, while he executed the priest’s office before God in the order of his course,
Siku moja ilipokuwa zamu ya kikundi cha Zekaria, yeye akifanya kazi ya ukuhani Hekaluni mbele za Mungu,
9 according to the custom of the priest’s office, his lot was to enter into the temple of the Lord and burn incense.
alichaguliwa kwa kura kwa kufuata desturi za ukuhani, kuingia Hekaluni mwa Bwana ili kufukiza uvumba.
10 And the whole multitude of the people were praying without at the hour of incense.
Nao wakati wa kufukiza uvumba ulipowadia, wale wote waliokuwa wamekusanyika ili kuabudu walikuwa nje wakiomba.
11 And there appeared unto him an angel of the Lord standing on the right side of the altar of incense.
Ndipo malaika wa Bwana, akiwa amesimama upande wa kuume wa madhabahu ya kufukizia uvumba, akamtokea Zekaria.
12 And Zacharias was troubled when he saw [him], and fear fell upon him.
Zekaria alipomwona huyo malaika, akafadhaika sana, akajawa na hofu.
13 But the angel said unto him, Fear not, Zacharias: because thy supplication is heard, and thy wife Elisabeth shall bear thee a son, and thou shalt call his name John.
Lakini malaika akamwambia, “Usiogope, Zekaria, kwa maana Mungu amesikia maombi yako. Mkeo Elizabeti atakuzalia mtoto wa kiume, nawe utamwita jina lake Yohana.
14 And thou shalt have joy and gladness; and many shall rejoice at his birth.
Yeye atakuwa furaha na shangwe kwako, nao watu wengi watashangilia kwa sababu ya kuzaliwa kwake.
15 For he shall be great in the sight of the Lord, and he shall drink no wine nor strong drink; and he shall be filled with the Holy Spirit, even from his mother’s womb.
Kwa kuwa atakuwa mkuu mbele za Bwana, kamwe hataonja mvinyo wala kinywaji chochote cha kulevya, naye atajazwa Roho Mtakatifu hata kabla ya kuzaliwa kwake.
16 And many of the children of Israel shall he turn unto the Lord their God.
Naye atawageuza wengi wa wana wa Israeli warudi kwa Bwana Mungu wao.
17 And he shall go before his face in the spirit and power of Elijah, to turn the hearts of the fathers to the children, and the disobedient [to walk] in the wisdom of the just; to make ready for the Lord a people prepared [for him].
Naye atatangulia mbele za Bwana katika roho na nguvu ya Eliya, ili kuigeuza mioyo ya baba kuwaelekea watoto wao, na wasiotii warejee katika hekima ya wenye haki, ili kuliweka tayari taifa lililoandaliwa kwa ajili ya Bwana.”
18 And Zacharias said unto the angel, Whereby shall I know this? for I am an old man, and my wife well stricken in years.
Zekaria akamuuliza malaika, “Jambo hilo linawezekanaje? Mimi ni mzee na mke wangu pia ana umri mkubwa.”
19 And the angel answering said unto him, I am Gabriel, that stand in the presence of God; and I was sent to speak unto thee, and to bring thee these good tidings.
Malaika akamjibu, akamwambia, “Mimi ni Gabrieli, nisimamaye mbele za Mungu, nami nimetumwa kwako ili nikuambie habari hizi njema.
20 And behold, thou shalt be silent and not able to speak, until the day that these things shall come to pass, because thou believedst not my words, which shall be fulfilled in their season.
Basi sasa kwa kuwa hujaamini maneno yangu ambayo yatatimizwa kwa wakati wake, utakuwa bubu hadi siku ile mambo haya yatakapotukia.”
21 And the people were waiting for Zacharias, and they marvelled while he tarried in the temple.
Wakati huo watu walikuwa wanamngojea Zekaria nje huku wakishangaa kukawia kwake mle Hekaluni.
22 And when he came out, he could not speak unto them: and they perceived that he had seen a vision in the temple: and he continued making signs unto them, and remained dumb.
Alipotoka akawa hawezi kusema nao, wao wakatambua kuwa ameona maono ndani ya Hekalu. Lakini kwa kuwa alikuwa bubu, akawa anawaashiria kwa mikono.
23 And it came to pass, when the days of his ministration were fulfilled, he departed unto his house.
Muda wake wa kuhudumu Hekaluni ulipomalizika, akarudi nyumbani kwake.
24 And after these days Elisabeth his wife conceived; and she hid herself five months, saying,
Baada ya muda usio mrefu, Elizabeti mkewe akapata mimba, naye akajitenga kwa miezi mitano.
25 Thus hath the Lord done unto me in the days wherein he looked upon [me], to take away my reproach among men.
Akasema, “Hili ndilo Bwana alilonitendea aliponiangalia kwa upendeleo na kuniondolea aibu yangu mbele ya watu.”
26 Now in the sixth month the angel Gabriel was sent from God unto a city of Galilee, named Nazareth,
Mwezi wa sita baada ya Elizabeti kupata mimba, Mungu alimtuma malaika Gabrieli aende Galilaya katika mji wa Nazareti,
27 to a virgin betrothed to a man whose name was Joseph, of the house of David; and the virgin’s name was Mary.
kwa mwanamwali bikira aliyekuwa ameposwa na mtu mmoja jina lake Yosefu wa nyumba ya Daudi. Jina la huyu mwanamwali bikira ni Maria.
28 And he came in unto her, and said, Hail, thou that art highly favored, the Lord [is] with thee.
Naye malaika akaja kwake akamwambia: “Salamu, wewe uliyebarikiwa, Bwana yu pamoja nawe!”
29 But she was greatly troubled at the saying, and cast in her mind what manner of salutation this might be.
Maria akafadhaishwa sana na maneno haya, akajiuliza moyoni, “Salamu hii ni ya namna gani?”
30 And the angel said unto her, Fear not, Mary: for thou hast found favor with God.
Ndipo malaika akamwambia, “Usiogope, Maria, umepata kibali kwa Mungu.
31 And behold, thou shalt conceive in thy womb, and bring forth a son, and shalt call his name JESUS.
Tazama, utachukua mimba, nawe utamzaa mtoto mwanaume na utamwita jina lake Yesu.
32 He shall be great, and shall be called the Son of the Most High: and the Lord God shall give unto him the throne of his father David:
Yeye atakuwa mkuu, naye ataitwa Mwana wa Aliye Juu Sana. Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi baba yake.
33 and he shall reign over the house of Jacob for ever; and of his kingdom there shall be no end. (aiōn g165)
Ataimiliki nyumba ya Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho.” (aiōn g165)
34 And Mary said unto the angel, How shall this be, seeing I know not a man?
Maria akamuuliza huyo malaika, “Maadamu mimi ni bikira, jambo hili litawezekanaje?”
35 And the angel answered and said unto her, The Holy Spirit shall come upon thee, and the power of the Most High shall overshadow thee: wherefore also the holy thing which is begotten shall be called the Son of God.
Malaika akamjibu, “Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, nazo nguvu zake Yeye Aliye Juu Sana zitakufunika kama kivuli. Kwa hiyo mtoto atakayezaliwa atakuwa mtakatifu, naye ataitwa Mwana wa Mungu.
36 And behold, Elisabeth thy kinswoman, she also hath conceived a son in her old age; and this is the sixth month with her that was called barren.
Tazama, jamaa yako Elizabeti amechukua mimba katika uzee wake, na huu ni mwezi wake wa sita, yeye aliyeitwa tasa.
37 For no word from God shall be void of power.
Kwa maana kwa Mungu hakuna lisilowezekana.”
38 And Mary said, Behold, the handmaid of the Lord; be it unto me according to thy word. And the angel departed from her.
Maria akasema, “Tazama, mimi ni mtumishi wa Bwana. Na iwe kwangu kama ulivyosema.” Kisha malaika akaondoka, akamwacha.
39 And Mary arose in these days and went into the hill country with haste, into a city of Judah;
Wakati huo Maria akajiandaa, akaharakisha kwenda katika mji mmoja kwenye vilima vya Uyahudi.
40 and entered into the house of Zacharias and saluted Elisabeth.
Akaingia nyumbani kwa Zekaria na kumsalimu Elizabeti.
41 And it came to pass, when Elisabeth heard the salutation of Mary, the babe leaped in her womb; and Elisabeth was filled with the Holy Spirit;
Naye Elizabeti aliposikia salamu ya Maria, mtoto aliyekuwa tumboni mwake akaruka. Elizabeti akajazwa na Roho Mtakatifu,
42 and she lifted up her voice with a loud cry, and said, Blessed [art] thou among women, and blessed [is] the fruit of thy womb.
akapaza sauti kwa nguvu akasema, “Umebarikiwa wewe miongoni mwa wanawake, naye mtoto utakayemzaa amebarikiwa.
43 And whence is this to me, that the mother of my Lord should come unto me?
Lakini ni kwa nini mimi nimepata upendeleo kiasi hiki, hata mama wa Bwana wangu afike kwangu?
44 For behold, when the voice of thy salutation came into mine ears, the babe leaped in my womb for joy.
Mara tu niliposikia sauti ya salamu yako, mtoto aliyeko tumboni mwangu aliruka kwa furaha.
45 And blessed [is] she that believed; for there shall be a fulfilment of the things which have been spoken to her from the Lord.
Amebarikiwa yeye aliyeamini kwamba lile Bwana alilomwambia litatimizwa.”
46 And Mary said, My soul doth magnify the Lord,
Naye Maria akasema: “Moyo wangu wamwadhimisha Bwana,
47 And my spirit hath rejoiced in God my Saviour.
nayo roho yangu inamfurahia Mungu Mwokozi wangu,
48 For he hath looked upon the low estate of his handmaid: For behold, from henceforth all generations shall call me blessed.
kwa kuwa ameangalia kwa fadhili unyonge wa mtumishi wake. Hakika tangu sasa vizazi vyote vitaniita aliyebarikiwa,
49 For he that is mighty hath done to me great things; And holy is his name.
kwa maana yeye Mwenye Nguvu amenitendea mambo ya ajabu: jina lake ni takatifu.
50 And his mercy is unto generations and generations On them that fear him.
Rehema zake huwaendea wale wamchao, kutoka kizazi hadi kizazi.
51 He hath showed strength with his arm; He hath scattered the proud in the imagination of their heart.
Kwa kuwa ametenda mambo ya ajabu kwa mkono wake; amewatawanya wale wenye kiburi ndani ya mioyo yao.
52 He hath put down princes from [their] thrones, And hath exalted them of low degree.
Amewashusha watawala toka kwenye viti vyao vya enzi, lakini amewainua wanyenyekevu.
53 The hungry he hath filled with good things; And the rich he hath sent empty away.
Amewashibisha wenye njaa kwa vitu vizuri, bali matajiri amewafukuza mikono mitupu.
54 He hath given help to Israel his servant, That he might remember mercy
Amemsaidia mtumishi wake Israeli, kwa kukumbuka ahadi yake ya kumrehemu
55 (As he spake unto our fathers) Toward Abraham and his seed for ever. (aiōn g165)
Abrahamu na uzao wake milele, kama alivyowaahidi baba zetu.” (aiōn g165)
56 And Mary abode with her about three months, and returned unto her house.
Maria akakaa na Elizabeti karibu miezi mitatu, kisha akarudi nyumbani kwake.
57 Now Elisabeth’s time was fulfilled that she should be delivered; and she brought forth a son.
Ulipowadia wakati wa Elizabeti kujifungua, alizaa mtoto mwanaume.
58 And her neighbors and her kinsfolk heard that the Lord had magnified his mercy towards her; and they rejoiced with her.
Majirani zake na jamii zake wakasikia jinsi Bwana alivyomfanyia rehema kuu, nao wakafurahi pamoja naye.
59 And it came to pass on the eighth day, that they came to circumcise the child; and they would have called him Zacharias, after the name of his father.
Siku ya nane wakaja kumtahiri mtoto, wakataka yule mtoto aitwe Zekaria, ambalo ndilo jina la baba yake.
60 And his mother answered and said, Not so; but he shall be called John.
Lakini mama yake akakataa na kusema, “Hapana! Jina lake ataitwa Yohana.”
61 And they said unto her, There is none of thy kindred that is called by this name.
Wakamwambia, “Hakuna mtu yeyote katika jamaa yako mwenye jina kama hilo.”
62 And they made signs to his father, what he would have him called.
Basi wakamfanyia Zekaria baba yake ishara ili kujua kwamba yeye angependa kumpa mtoto jina gani.
63 And he asked for a writing tablet, and wrote, saying, His name is John. And they marvelled all.
Akaomba wampe kibao cha kuandikia na kwa mshangao wa kila mtu akaandika: “Jina lake ni Yohana.”
64 And his mouth was opened immediately, and his tongue [loosed], and he spake, blessing God.
Papo hapo kinywa chake kikafunguliwa na ulimi wake ukaachiwa, akawa anaongea akimsifu Mungu.
65 And fear came on all that dwelt round about them: and all these sayings were noised abroad throughout all the hill country of Judæa.
Majirani wote wakajawa na hofu ya Mungu, na katika nchi yote ya vilima vya Uyahudi watu walikuwa wakinena juu ya mambo haya yote.
66 And all that heard them laid them up in their heart, saying, What then shall this child be? For the hand of the Lord was with him.
Kila aliyesikia habari hizi alishangaa akauliza, “Je, mtoto huyu atakuwa mtu wa namna gani?” Maana mkono wa Bwana ulikuwa pamoja naye.
67 And his father Zacharias was filled with the Holy Spirit, and prophesied, saying,
Zekaria, baba yake, akajazwa na Roho Mtakatifu, naye akatoa unabii, akisema:
68 Blessed [be] the Lord, the God of Israel; For he hath visited and wrought redemption for his people,
“Ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, kwa kuwa amewajilia watu wake na kuwakomboa.
69 And hath raised up a horn of salvation for us In the house of his servant David
Naye ametusimamishia pembe ya wokovu katika nyumba ya Daudi mtumishi wake,
70 (As he spake by the mouth of his holy prophets that have been from of old), (aiōn g165)
kama alivyonena kwa vinywa vya manabii wake watakatifu tangu zamani, (aiōn g165)
71 Salvation from our enemies, and from the hand of all that hate us;
kwamba atatuokoa kutoka kwa adui zetu, na kutoka mikononi mwao wote watuchukiao:
72 To show mercy towards our fathers, And to remember his holy covenant;
ili kuonyesha rehema kwa baba zetu na kukumbuka Agano lake takatifu,
73 The oath which he sware unto Abraham our father,
kiapo alichomwapia baba yetu Abrahamu:
74 To grant unto us that we being delivered out of the hand of our enemies Should serve him without fear,
kutuokoa kutoka mikononi mwa adui zetu, tupate kumtumikia yeye pasipo hofu
75 In holiness and righteousness before him all our days.
katika utakatifu na haki mbele zake, siku zetu zote.
76 Yea and thou, child, shalt be called the prophet of the Most High: For thou shalt go before the face of the Lord to make ready his ways;
“Nawe mtoto wangu, utaitwa nabii wa Aliye Juu Sana; kwa kuwa utamtangulia Bwana na kuandaa njia kwa ajili yake,
77 To give knowledge of salvation unto his people In the remission of their sins,
kuwajulisha watu wake juu ya wokovu utakaopatikana kwa kusamehewa dhambi zao,
78 Because of the tender mercy of our God, Whereby the dayspring from on high shall visit us,
kwa ajili ya wingi wa rehema za Mungu wetu, nuru itokayo juu itatuzukia
79 To shine upon them that sit in darkness and the shadow of death; To guide our feet into the way of peace.
ili kuwaangazia wale waishio gizani na katika uvuli wa mauti, kuiongoza miguu yetu katika njia ya amani.”
80 And the child grew, and waxed strong in spirit, and was in the deserts till the day of his showing unto Israel.
Yule mtoto akakua na kuongezeka nguvu katika roho; akaishi nyikani hadi siku ile alipojionyesha hadharani kwa Waisraeli.

< Luke 1 >