< 1 Samuel 12 >
1 And Samuel said unto all Israel, Behold, I have hearkened unto your voice in all that ye said unto me, and have made a king over you.
Samweli akawaambia Israeli wote, “Nimesikiliza kila kitu mlichoniambia nami nimewawekea mfalme juu yenu.
2 And now, behold, the king walketh before you; and I am old and grayheaded; and, behold, my sons are with you: and I have walked before you from my youth unto this day.
Sasa mnaye mfalme kama kiongozi wenu. Lakini kwa habari yangu mimi ni mzee na nina mvi, nao wanangu wapo hapa pamoja nanyi. Nimekuwa kiongozi wenu tangu ujana wangu mpaka siku hii ya leo.
3 Here I am: witness against me before Jehovah, and before his anointed: whose ox have I taken? or whose ass have I taken? or whom have I defrauded? whom have I oppressed? or of whose hand have I taken a ransom to blind mine eyes therewith? and I will restore it you.
Mimi ninasimama hapa. Shuhudieni juu yangu mbele za Bwana na mpakwa mafuta wake. Nimechukua maksai wa nani? Nimechukua punda wa nani? Ni nani nimepata kumdanganya? Ni nani nimepata kumwonea? Ni kutoka kwenye mkono wa nani nimepokea rushwa ili kunifanya nifumbe macho yangu? Kama nimefanya chochote katika hivi, mimi nitawarudishia.”
4 And they said, Thou hast not defrauded us, nor oppressed us, neither hast thou taken aught of any man’s hand.
Wakajibu, “Hujatudanganya wala kutuonea. Hujapokea chochote kutoka kwenye mkono wa mtu awaye yote.”
5 And he said unto them, Jehovah is witness against you, and his anointed is witness this day, that ye have not found aught in my hand. And they said, He is witness.
Samweli akawaambia, “Bwana ni shahidi juu yenu, pia mpakwa mafuta wake ni shahidi siku hii ya leo, kwamba hamkukuta chochote mkononi mwangu.” Wakasema, “Yeye ni shahidi.”
6 And Samuel said unto the people, It is Jehovah that appointed Moses and Aaron, and that brought your fathers up out of the land of Egypt.
Kisha Samweli akawaambia watu, “Bwana ndiye alimchagua Mose na Aroni, na kuwaleta baba zenu akiwapandisha kutoka Misri.
7 Now therefore stand still, that I may plead with you before Jehovah concerning all the righteous acts of Jehovah, which he did to you and to your fathers.
Sasa basi, simameni hapa, kwa sababu nitakabiliana nanyi kwa ushahidi mbele za Bwana wa matendo yote ya haki yaliyofanywa na Bwana kwenu na kwa baba zenu.
8 When Jacob was come into Egypt, and your fathers cried unto Jehovah, then Jehovah sent Moses and Aaron, who brought forth your fathers out of Egypt, and made them to dwell in this place.
“Baada ya Yakobo kuingia Misri, walimlilia Bwana kwa ajili ya msaada, naye Bwana akawatuma Mose na Aroni, ambao waliwatoa baba zenu kutoka Misri na kuwakalisha mahali hapa.
9 But they forgat Jehovah their God; and he sold them into the hand of Sisera, captain of the host of Hazor, and into the hand of the Philistines, and into the hand of the king of Moab; and they fought against them.
“Lakini wakamsahau Bwana Mungu wao, hivyo Mungu akawauza katika mkono wa Sisera, jemadari wa jeshi la Hazori na katika mikono ya Wafilisti na mfalme wa Moabu, ambaye alipigana dhidi yao.
10 And they cried unto Jehovah, and said, We have sinned, because we have forsaken Jehovah, and have served the Baalim and the Ashtaroth: but now deliver us out of the hand of our enemies, and we will serve thee.
Wakamlilia Bwana na kusema, ‘Tumetenda dhambi; tumemwacha Bwana na kutumikia Mabaali na Maashtorethi. Lakini sasa tuokoe kutoka mikono ya adui zetu, nasi tutakutumikia.’
11 And Jehovah sent Jerubbaal, and Bedan, and Jephthah, and Samuel, and delivered you out of the hand of your enemies on every side; and ye dwelt in safety.
Ndipo Bwana akawatuma Yerub-Baali, Baraka, Yefta na Samweli, naye akawaokoa kutoka mikononi mwa adui zenu kila upande, ili ninyi mpate kukaa salama.
12 And when ye saw that Nahash the king of the children of Ammon came against you, ye said unto me, Nay, but a king shall reign over us; when Jehovah your God was your king.
“Lakini mlipomwona yule Nahashi mfalme wa Waamoni anakuja dhidi yenu, mliniambia, ‘Hapana, tunataka mfalme atutawale,’ hata ingawa Bwana Mungu wenu alikuwa mfalme wenu.
13 Now therefore behold the king whom ye have chosen, and whom ye have asked for: and, behold, Jehovah hath set a king over you.
Sasa huyu hapa ndiye mfalme mliyemchagua, yule mliyeomba; tazameni, Bwana amemweka mfalme juu yenu.
14 If ye will fear Jehovah, and serve him, and hearken unto his voice, and not rebel against the commandment of Jehovah, and both ye and also the king that reigneth over you be followers of Jehovah your God, [well]:
Kama mkimcha Bwana na kumtumikia na kumtii nanyi msipoasi dhidi ya amri zake, ninyi pamoja na mfalme anayetawala juu yenu mkimfuata Bwana, Mungu wenu, mambo yatakuwa mema kwenu!
15 but if ye will not hearken unto the voice of Jehovah, but rebel against the commandment of Jehovah, then will the hand of Jehovah be against you, as it was against your fathers.
Lakini kama hamkumtii Bwana, nanyi kama mkiasi dhidi ya amri zake, mkono wake utakuwa dhidi yenu, kama ulivyokuwa dhidi ya baba zenu.
16 Now therefore stand still and see this great thing, which Jehovah will do before your eyes.
“Sasa basi, simameni kimya mkaone jambo hili kubwa ambalo Bwana anakwenda kulifanya mbele ya macho yenu!
17 Is it not wheat harvest to-day? I will call unto Jehovah, that he may send thunder and rain; and ye shall know and see that your wickedness is great, which ye have done in the sight of Jehovah, in asking you a king.
Je, sasa si mavuno ya ngano? Nitamwomba Bwana ili alete ngurumo na mvua. Nanyi mtatambua jambo hili lilivyo baya mlilolifanya mbele za macho ya Bwana mlipoomba mfalme.”
18 So Samuel called unto Jehovah; and Jehovah sent thunder and rain that day: and all the people greatly feared Jehovah and Samuel.
Kisha Samweli akamwomba Bwana, na siku ile ile Bwana akatuma ngurumo na mvua. Hivyo watu wote wakamwogopa sana Bwana na Samweli.
19 And all the people said unto Samuel, Pray for thy servants unto Jehovah thy God, that we die not; for we have added unto all our sins [this] evil, to ask us a king.
Watu wote wakamwambia Samweli, “Mwombe Bwana Mungu wako kwa ajili ya watumishi wako, ili tusije tukafa, kwa kuwa tumeongeza uovu juu ya dhambi zetu nyingine kwa kuomba mfalme.”
20 And Samuel said unto the people, Fear not: ye have indeed done all this evil; yet turn not aside from following Jehovah, but serve Jehovah with all your heart:
Samweli akajibu, “Msiogope, mmefanya uovu huu wote; hata hivyo msimwache Bwana, bali mtumikieni Bwana kwa moyo wenu wote.
21 and turn ye not aside; for [then would ye go] after vain things which cannot profit nor deliver, for they are vain.
Msigeukie sanamu zisizofaa. Haziwezi kuwatendea jema, wala haziwezi kuwaokoa kwa sababu hazina maana.
22 For Jehovah will not forsake his people for his great name’s sake, because it hath pleased Jehovah to make you a people unto himself.
Kwa ajili ya jina lake kuu Bwana hatawakataa watu wake, kwa sababu ilimpendeza Bwana kuwafanya kuwa wake mwenyewe.
23 Moreover as for me, far be it from me that I should sin against Jehovah in ceasing to pray for you: but I will instruct you in the good and the right way.
Kwa habari yangu, iwe mbali nami kutenda dhambi dhidi ya Bwana kwa kushindwa kuwaombea. Mimi nitawafundisha njia iliyo njema na ya kunyooka.
24 Only fear Jehovah, and serve him in truth with all your heart; for consider how great things he hath done for you.
Lakini hakikisheni mnamcha Bwana na kumtumikia kwa uaminifu kwa moyo wenu wote; tafakarini mambo makubwa aliyoyatenda kwa ajili yenu.
25 But if ye shall still do wickedly, ye shall be consumed, both ye and your king.
Hata hivyo mkiendelea kufanya uovu, ninyi na mfalme wenu mtafutiliwa mbali!”