< Psalms 60 >

1 For the Chief Musician. To the tune of “The Lily of the Covenant.” A teaching poem by David, when he fought with Aram Naharaim and with Aram Zobah, and Joab returned, and killed twelve thousand of Edom in the Valley of Salt. God, you have rejected us. You have broken us down. You have been angry. Restore us, again.
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Shushani Eduthi.” Utenzi wa Daudi wa kufundisha. Wakati alipopigana na Waaramu kutoka Aramu-Naharaimu na Aramu-Soba, naye Yoabu akarudi nyuma na kuwaua Waedomu 12,000 katika Bonde la Chumvi. Ee Mungu, umetukataa na kutokea ghafula juu yetu, umekasirika: sasa turejeshe upya!
2 You have made the land tremble. You have torn it. Mend its fractures, for it quakes.
Umetetemesha nchi na kuipasua; uiponye mavunjiko yake, kwa maana inatetemeka.
3 You have shown your people hard things. You have made us drink the wine that makes us stagger.
Umewaonyesha watu wako nyakati za kukata tamaa; umetunywesha mvinyo unaotuyumbisha.
4 You have given a banner to those who fear you, that it may be displayed because of the truth. (Selah)
Kwa wale wanaokucha wewe, umewainulia bendera, ili iweze kutwekwa dhidi ya upinde.
5 So that your beloved may be delivered, save with your right hand, and answer us.
Tuokoe na utusaidie kwa mkono wako wa kuume, ili wale uwapendao wapate kuokolewa.
6 God has spoken from his sanctuary: “I will triumph. I will divide Shechem, and measure out the valley of Succoth.
Mungu amenena kutoka patakatifu pake: “Nitaigawa Shekemu kwa ushindi na kulipima Bonde la Sukothi.
7 Gilead is mine, and Manasseh is mine. Ephraim also is the defense of my head. Judah is my scepter.
Gileadi ni yangu na Manase ni yangu; Efraimu ni kofia yangu ya chuma, nayo Yuda ni fimbo yangu ya utawala.
8 Moab is my wash basin. I will throw my sandal on Edom. I shout in triumph over Philistia.”
Moabu ni sinia langu la kunawia, juu ya Edomu natupa kiatu changu; nashangilia kwa kushindwa kwa Ufilisti.”
9 Who will bring me into the strong city? Who has led me to Edom?
Ni nani atakayenipeleka hadi mji wenye ngome? Ni nani atakayeniongoza hadi nifike Edomu?
10 Have not you, God, rejected us? You do not go out with our armies, God.
Ee Mungu, si ni wewe uliyetukataa sisi, na hutoki tena na majeshi yetu?
11 Give us help against the adversary, for the help of man is vain.
Tuletee msaada dhidi ya adui, kwa maana msaada wa mwanadamu haufai kitu.
12 Through God we will do valiantly, for it is he who will tread down our adversaries.
Kwa msaada wa Mungu tutapata ushindi, naye atawaponda adui zetu.

< Psalms 60 >