< Psalms 41 >

1 For the Chief Musician. A Psalm by David. Blessed is he who considers the poor. The LORD will deliver him in the day of evil.
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Heri mtu yule anayemjali mnyonge, Bwana atamwokoa wakati wa shida.
2 The LORD will preserve him, and keep him alive. He shall be blessed on the earth, and he will not surrender him to the will of his enemies.
Bwana atamlinda na kuyahifadhi maisha yake, atambariki katika nchi na hatamwacha katika tamaa ya adui zake.
3 The LORD will sustain him on his sickbed, and restore him from his bed of illness.
Bwana atamtegemeza awapo mgonjwa kitandani, atamwinua kutoka kitandani mwake.
4 I said, “LORD, have mercy on me! Heal me, for I have sinned against you.”
Nilisema, “Ee Bwana nihurumie, niponye, maana nimekutenda dhambi wewe.”
5 My enemies speak evil against me: “When will he die, and his name perish?”
Adui zangu wanasema kwa hila, “Lini atakufa, na jina lake litokomee kabisa.”
6 If he comes to see me, he speaks falsehood. His heart gathers iniquity to itself. When he goes abroad, he tells it.
Kila anapokuja mtu kunitazama, huzungumza uongo, huku moyo wake hukusanya masingizio; kisha huondoka na kuyasambaza huku na huko.
7 All who hate me whisper together against me. They imagine the worst for me.
Adui zangu wote hunongʼonezana dhidi yangu, hao huniwazia mabaya sana, wakisema,
8 “An evil disease”, they say, “has afflicted him. Now that he lies he shall rise up no more.”
“Ugonjwa mbaya sana umempata, kamwe hatainuka tena kitandani mwake.”
9 Yes, my own familiar friend, in whom I trusted, who ate bread with me, has lifted up his heel against me.
Hata rafiki yangu wa karibu niliyemwamini, yule aliyekula chakula changu ameniinulia kisigino chake.
10 But you, LORD, have mercy on me, and raise me up, that I may repay them.
Lakini wewe, Ee Bwana, nihurumie, ukaniinue tena, ili niweze kuwalipiza kisasi.
11 By this I know that you delight in me, because my enemy does not triumph over me.
Najua kwamba wapendezwa nami, kwa kuwa adui yangu hanishindi.
12 As for me, you uphold me in my integrity, and set me in your presence forever.
Katika uadilifu wangu unanitegemeza na kuniweka kwenye uwepo wako milele.
13 Blessed be the LORD, the God of Israel, from everlasting and to everlasting! Amen and amen.
Msifuni Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele.

< Psalms 41 >