< Psalms 141 >

1 A Psalm by David. LORD, I have called on you. Come to me quickly! Listen to my voice when I call to you.
Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, ninakuita wewe, uje kwangu hima. Sikia sauti yangu ninapokuita.
2 Let my prayer be set before you like incense; the lifting up of my hands like the evening sacrifice.
Maombi yangu na yafike mbele zako kama uvumba; kuinua mikono yangu juu na kuwe kama dhabihu ya jioni.
3 Set a watch, LORD, before my mouth. Keep the door of my lips.
Ee Bwana, weka mlinzi kinywani mwangu, weka ulinzi mlangoni mwa midomo yangu.
4 Do not incline my heart to any evil thing, to practice deeds of wickedness with men who work iniquity. Do not let me eat of their delicacies.
Usiuache moyo wangu uvutwe katika jambo baya, nisije nikashiriki katika matendo maovu pamoja na watu watendao mabaya, wala nisije nikala vyakula vyao vya anasa.
5 Let the righteous strike me, it is kindness; let him reprove me, it is like oil on the head; do not let my head refuse it; Yet my prayer is always against evil deeds.
Mtu mwenye haki na anipige: ni jambo la huruma; na anikemee: ni mafuta kichwani mwangu. Kichwa changu hakitalikataa. Hata hivyo, maombi yangu daima ni kinyume cha watenda mabaya,
6 Their judges are thrown down by the sides of the rock. They will hear my words, for they are well spoken.
watawala wao watatupwa chini kutoka kwenye majabali, waovu watajifunza kwamba maneno yangu yalikuwa kweli.
7 "As when one plows and breaks up the earth, our bones are scattered at the mouth of Sheol (Sheol h7585)."
Watasema, “Kama mtu anavyolima na kuvunja ardhi, ndivyo mifupa yetu imetawanywa kwenye mlango wa kaburi.” (Sheol h7585)
8 For my eyes are on you, LORD, the Lord. I take refuge in you. Do not leave my soul destitute.
Lakini nimekaza macho yangu kwako, Ee Bwana Mwenyezi, ndani yako nimekimbilia, usiniache nife.
9 Keep me from the snare which they have laid for me, from the traps of the workers of iniquity.
Niepushe na mitego waliyonitegea, kutokana na mitego iliyotegwa na watenda mabaya.
10 Let the wicked fall together into their own nets while I pass by.
Waovu na waanguke kwenye nyavu zao wenyewe, wakati mimi ninapita salama.

< Psalms 141 >