< Psalms 129 >

1 A Song of Ascents. Many times they have afflicted me from my youth up. Let Israel now say:
Wimbo wa kwenda juu. Wamenionea mno tangu ujana wangu; Israeli na aseme sasa:
2 many times they have afflicted me from my youth up, yet they have not prevailed against me.
wamenionea mno tangu ujana wangu, lakini bado hawajanishinda.
3 The plowers plowed on my back. They made their furrows long.
Wakulima wamelima mgongo wangu, na kufanya mifereji yao mirefu.
4 The LORD is righteous. He has cut apart the cords of the wicked.
Lakini Bwana ni mwenye haki; amenifungua toka kamba za waovu.
5 Let them be disappointed and turned backward, all those who hate Zion.
Wale wote waichukiao Sayuni na warudishwe nyuma kwa aibu.
6 Let them be as the grass on the housetops, which withers before it grows up,
Wawe kama majani juu ya paa, ambayo hunyauka kabla hayajakua;
7 with which the reaper does not fill his hand, nor he who binds sheaves, his bosom.
kwa hayo mvunaji hawezi kujaza vitanga vyake, wala akusanyaye kujaza mikono yake.
8 Neither do those who go by say, “The blessing of the LORD be on you. We bless you in the LORD’s name.”
Wale wapitao karibu na wasiseme, “Baraka ya Bwana iwe juu yako; tunakubariki katika jina la Bwana.”

< Psalms 129 >