< Psalms 107 >

1 Give thanks to the LORD, for he is good, for his loving kindness endures forever.
Mshukuruni Bwana, kwa kuwa yeye ni mwema, upendo wake wadumu milele.
2 Let the redeemed by the LORD say so, whom he has redeemed from the hand of the adversary,
Waliokombolewa wa Bwana na waseme hivi, wale aliowaokoa kutoka mkono wa adui,
3 and gathered out of the lands, from the east and from the west, from the north and from the south.
wale aliowakusanya kutoka nchi mbalimbali, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
4 They wandered in the wilderness in a desert way. They found no city to live in.
Baadhi yao walitangatanga jangwani, hawakuona njia ya kuwafikisha mji ambao wangeweza kuishi.
5 Hungry and thirsty, their soul fainted in them.
Walikuwa na njaa na kiu, nafsi zao zikadhoofika.
6 Then they cried to the LORD in their trouble, and he delivered them out of their distresses.
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
7 He led them also by a straight way, that they might go to a city to live in.
Akawaongoza kwa njia iliyo sawa hadi mji ambao wangeweza kuishi.
8 Let them praise the LORD for his loving kindness, for his wonderful deeds to the children of men!
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
9 For he satisfies the longing soul. He fills the hungry soul with good.
kwa maana yeye humtosheleza mwenye kiu, na kumshibisha mwenye njaa kwa vitu vyema.
10 Some sat in darkness and in the shadow of death, being bound in affliction and iron,
Wengine walikaa gizani na katika huzuni kuu, wafungwa wakiteseka katika minyororo,
11 because they rebelled against the words of God, and condemned the counsel of the Most High.
kwa sababu walikuwa wameasi dhidi ya maneno ya Mungu na kudharau shauri la Aliye Juu Sana.
12 Therefore he brought down their heart with labor. They fell down, and there was no one to help.
Aliwatumikisha kwa kazi ngumu; walijikwaa na hapakuwepo yeyote wa kuwasaidia.
13 Then they cried to the LORD in their trouble, and he saved them out of their distresses.
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
14 He brought them out of darkness and the shadow of death, and broke away their chains.
Akawatoa katika giza na huzuni kuu na akavunja minyororo yao.
15 Let them praise the LORD for his loving kindness, for his wonderful deeds to the children of men!
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
16 For he has broken the gates of bronze, and cut through bars of iron.
kwa kuwa yeye huvunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
17 Fools are afflicted because of their disobedience, and because of their iniquities.
Wengine wakawa wapumbavu kutokana na uasi wao, wakapata mateso kwa sababu ya uovu wao.
18 Their soul abhors all kinds of food. They draw near to the gates of death.
Wakachukia kabisa vyakula vyote, wakakaribia malango ya mauti.
19 Then they cry to the LORD in their trouble, and he saves them out of their distresses.
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
20 He sends his word, and heals them, and delivers them from their graves.
Akalituma neno lake na kuwaponya, akawaokoa kutoka maangamizo yao.
21 Let them praise the LORD for his loving kindness, for his wonderful deeds to the children of men!
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
22 Let them offer the sacrifices of thanksgiving, and declare his deeds with singing.
Na watoe dhabihu za kushukuru, na wasimulie matendo yake kwa nyimbo za furaha.
23 Those who go down to the sea in ships, who do business in great waters,
Wengine walisafiri baharini kwa meli, walikuwa wafanyabiashara kwenye maji makuu.
24 these see the LORD’s deeds, and his wonders in the deep.
Waliziona kazi za Bwana, matendo yake ya ajabu kilindini.
25 For he commands, and raises the stormy wind, which lifts up its waves.
Kwa maana alisema na kuamsha tufani iliyoinua mawimbi juu.
26 They mount up to the sky; they go down again to the depths. Their soul melts away because of trouble.
Yakainuka juu mbinguni, yakashuka chini hadi vilindini, katika hatari hii ujasiri wao uliyeyuka.
27 They reel back and forth, and stagger like a drunken man, and are at their wits’ end.
Walipepesuka na kuyumbayumba kama walevi, ujanja wao ukafikia ukomo.
28 Then they cry to the LORD in their trouble, and he brings them out of their distress.
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawatoa kwenye taabu yao.
29 He makes the storm a calm, so that its waves are still.
Akatuliza dhoruba kwa mnongʼono, mawimbi ya bahari yakatulia.
30 Then they are glad because it is calm, so he brings them to their desired haven.
Walifurahi ilipokuwa shwari, naye akawaongoza hadi bandari waliyoitamani.
31 Let them praise the LORD for his loving kindness, for his wonderful deeds for the children of men!
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
32 Let them exalt him also in the assembly of the people, and praise him in the seat of the elders.
Na wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu, na wamsifu katika baraza la wazee.
33 He turns rivers into a desert, water springs into a thirsty ground,
Yeye aligeuza mito kuwa jangwa, chemchemi za maji zitiririkazo kuwa ardhi yenye kiu,
34 and a fruitful land into a salt waste, for the wickedness of those who dwell in it.
nchi izaayo ikawa ya chumvi isiyofaa, kwa sababu ya uovu wa wale walioishi humo.
35 He turns a desert into a pool of water, and a dry land into water springs.
Aligeuza jangwa likawa madimbwi ya maji, nayo ardhi kame kuwa chemchemi za maji zitiririkazo;
36 There he makes the hungry live, that they may prepare a city to live in,
aliwaleta wenye njaa wakaishi humo, nao wakajenga mji wangeweza kuishi.
37 sow fields, plant vineyards, and reap the fruits of increase.
Walilima mashamba na kupanda mizabibu, nayo ikazaa matunda mengi,
38 He blesses them also, so that they are multiplied greatly. He does not allow their livestock to decrease.
Mungu aliwabariki, hesabu yao ikaongezeka sana, wala hakuruhusu mifugo yao kupungua.
39 Again, they are diminished and bowed down through oppression, trouble, and sorrow.
Kisha hesabu yao ilipungua, na walinyenyekeshwa kwa kuonewa, maafa na huzuni.
40 He pours contempt on princes, and causes them to wander in a trackless waste.
Yeye ambaye huwamwagia dharau wakuu, aliwafanya watangetange nyikani isiyo na njia.
41 Yet he lifts the needy out of their affliction, and increases their families like a flock.
Lakini yeye aliwainua wahitaji katika taabu zao, na kuongeza jamaa zao kama makundi ya kondoo.
42 The upright will see it, and be glad. All the wicked will shut their mouths.
Wanyofu wataona na kufurahi, lakini waovu wote watafunga vinywa vyao.
43 Whoever is wise will pay attention to these things. They will consider the loving kindnesses of the LORD.
Yeyote aliye na hekima, ayasikie mambo haya, na atafakari upendo mkuu wa Bwana.

< Psalms 107 >