< Psalms 1 >

1 Blessed is the man who does not walk in the counsel of the wicked, nor stand on the path of sinners, nor sit in the seat of scoffers;
Heri mtu yule ambaye haendi katika shauri la watu waovu, wala hasimami katika njia ya wenye dhambi, au kuketi katika baraza la wenye mizaha.
2 but his delight is in the LORD’s law. On his law he meditates day and night.
Bali huifurahia sheria ya Bwana, naye huitafakari hiyo sheria usiku na mchana.
3 He will be like a tree planted by the streams of water, that produces its fruit in its season, whose leaf also does not wither. Whatever he does shall prosper.
Mtu huyo ni kama mti uliopandwa kando ya vijito vya maji, ambao huzaa matunda kwa majira yake na majani yake hayanyauki. Lolote afanyalo hufanikiwa.
4 The wicked are not so, but are like the chaff which the wind drives away.
Sivyo walivyo waovu! Wao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.
5 Therefore the wicked shall not stand in the judgment, nor sinners in the congregation of the righteous.
Kwa hiyo waovu hawatastahimili hukumu, wala wenye dhambi katika kusanyiko la wenye haki.
6 For the LORD knows the way of the righteous, but the way of the wicked shall perish.
Kwa maana Bwana huziangalia njia za mwenye haki, bali njia ya waovu itaangamia.

< Psalms 1 >