< Proverbs 10 >

1 The proverbs of Solomon. A wise son makes a glad father; but a foolish son brings grief to his mother.
Mithali za Solomoni: Mwana mwenye hekima huleta furaha kwa baba yake, lakini mwana mpumbavu huleta huzuni kwa mama yake.
2 Treasures of wickedness profit nothing, but righteousness delivers from death.
Hazina zilizopatikana kwa njia mbaya hazifai, lakini uadilifu huokoa kutoka mautini.
3 The LORD will not allow the soul of the righteous to go hungry, but he thrusts away the desire of the wicked.
Bwana hawaachi waadilifu kukaa njaa, lakini hupinga tamaa ya mtu mwovu.
4 He becomes poor who works with a lazy hand, but the hand of the diligent brings wealth.
Mikono mivivu hufanya mtu kuwa maskini lakini mikono yenye bidii huleta utajiri.
5 He who gathers in summer is a wise son, but he who sleeps during the harvest is a son who causes shame.
Yeye akusanyaye mazao wakati wa kiangazi ni mwana mwenye hekima, lakini yeye alalaye wakati wa mavuno ni mwana mwenye kuaibisha.
6 Blessings are on the head of the righteous, but violence covers the mouth of the wicked.
Baraka huwa taji kichwani mwa mwenye haki, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
7 The memory of the righteous is blessed, but the name of the wicked will rot.
Kumbukumbu ya mwenye haki itakuwa baraka, lakini jina la mwovu litaoza.
8 The wise in heart accept commandments, but a chattering fool will fall.
Mwenye hekima moyoni hupokea maagizo, lakini mpumbavu apayukaye huangamia.
9 He who walks blamelessly walks surely, but he who perverts his ways will be found out.
Mtu mwadilifu hutembea salama, lakini mtu aendaye katika njia zilizopotoka atagunduliwa.
10 One who winks with the eye causes sorrow, but a chattering fool will fall.
Yeye akonyezaye kwa nia mbaya husababisha huzuni, naye mpumbavu apayukaye huangamia.
11 The mouth of the righteous is a spring of life, but violence covers the mouth of the wicked.
Kinywa cha mwenye haki ni chemchemi ya uzima, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
12 Hatred stirs up strife, but love covers all wrongs.
Chuki huchochea faraka, lakini upendo husitiri mabaya yote.
13 Wisdom is found on the lips of him who has discernment, but a rod is for the back of him who is void of understanding.
Hekima hupatikana katika midomo ya wenye kupambanua, lakini fimbo ni kwa ajili ya mgongo wake asiye na ufahamu.
14 Wise men lay up knowledge, but the mouth of the foolish is near ruin.
Wenye hekima huhifadhi maarifa, bali kinywa cha mpumbavu hualika maangamizi.
15 The rich man’s wealth is his strong city. The destruction of the poor is their poverty.
Mali ya tajiri ni mji wake wenye ngome, bali ufukara ni maangamizi ya maskini.
16 The labor of the righteous leads to life. The increase of the wicked leads to sin.
Ujira wa wenye haki huwaletea uzima, lakini mapato ya waovu huwaletea adhabu.
17 He is in the way of life who heeds correction, but he who forsakes reproof leads others astray.
Anayekubali kuadibishwa yuko katika njia ya uzima, lakini yeyote anayepuuza maonyo hupotosha wengine.
18 He who hides hatred has lying lips. He who utters a slander is a fool.
Yeye afichaye chuki yake ana midomo ya uongo, na yeyote anayeeneza uchonganishi ni mpumbavu.
19 In the multitude of words there is no lack of disobedience, but he who restrains his lips does wisely.
Wakati maneno ni mengi, dhambi haikosekani, lakini yeye ambaye huzuia ulimi wake ni mwenye busara.
20 The tongue of the righteous is like choice silver. The heart of the wicked is of little worth.
Ulimi wa mwenye haki ni fedha iliyo bora, bali moyo wa mwovu una thamani ndogo.
21 The lips of the righteous feed many, but the foolish die for lack of understanding.
Midomo ya mwenye haki hulisha wengi, lakini wapumbavu hufa kwa kukosa ufahamu.
22 The LORD’s blessing brings wealth, and he adds no trouble to it.
Baraka ya Bwana hutajirisha, wala haichanganyi huzuni.
23 It is a fool’s pleasure to do wickedness, but wisdom is a man of understanding’s pleasure.
Mpumbavu hufurahia tabia mbaya, lakini mtu mwenye ufahamu hupendezwa na hekima.
24 What the wicked fear will overtake them, but the desire of the righteous will be granted.
Kile anachoogopa mwovu ndicho kitakachompata; kile anachoonea shauku mwenye haki atapewa.
25 When the whirlwind passes, the wicked is no more; but the righteous stand firm forever.
Tufani inapopita, waovu hutoweka, lakini wenye haki husimama imara milele.
26 As vinegar to the teeth, and as smoke to the eyes, so is the sluggard to those who send him.
Kama siki ilivyo kwa meno na moshi kwa macho, ndivyo alivyo mvivu kwa wale waliomtuma.
27 The fear of the LORD prolongs days, but the years of the wicked shall be shortened.
Kumcha Bwana huongeza urefu wa maisha, lakini miaka ya mwovu inafupishwa.
28 The prospect of the righteous is joy, but the hope of the wicked will perish.
Tarajio la mwenye haki ni furaha, bali matumaini ya mwovu huwa si kitu.
29 The way of the LORD is a stronghold to the upright, but it is a destruction to the workers of iniquity.
Njia ya Bwana ni kimbilio kwa wenye haki, lakini ni maangamizi ya wale watendao mabaya.
30 The righteous will never be removed, but the wicked will not dwell in the land.
Kamwe wenye haki hawataondolewa, bali waovu hawatasalia katika nchi.
31 The mouth of the righteous produces wisdom, but the perverse tongue will be cut off.
Kinywa cha mwenye haki hutoa hekima, bali ulimi wa upotovu utakatwa.
32 The lips of the righteous know what is acceptable, but the mouth of the wicked is perverse.
Midomo ya wenye haki inajua kile kinachofaa, bali kinywa cha mwovu hujua kile kilichopotoka tu.

< Proverbs 10 >