< Matthew 26 >

1 When Jesus had finished all these words, he said to his disciples,
Yesu alipomaliza kusema hayo yote, aliwaambia wanafunzi wake,
2 “You know that after two days the Passover is coming, and the Son of Man will be delivered up to be crucified.”
“Mnajua kwamba baada ya siku mbili tutakuwa na sikukuu ya Pasaka, na Mwana wa Mtu atatolewa ili asulubiwe.”
3 Then the chief priests, the scribes, and the elders of the people were gathered together in the court of the high priest, who was called Caiaphas.
Wakati huo makuhani wakuu na wazee wa watu walikutana pamoja katika ukumbi wa Kayafa, Kuhani Mkuu.
4 They took counsel together that they might take Jesus by deceit and kill him.
Wakashauriana jinsi ya kumtia Yesu nguvuni kwa hila wamuue.
5 But they said, “Not during the feast, lest a riot occur among the people.”
Lakini wakaamua jambo hilo lisifanyike wakati wa sikukuu, kusije kukatokea ghasia kati ya watu.
6 Now when Jesus was in Bethany, in the house of Simon the leper,
Yesu alipokuwa Bethania, nyumbani kwa Simoni, aitwaye Mkoma,
7 a woman came to him having an alabaster jar of very expensive ointment, and she poured it on his head as he sat at the table.
mama mmoja aliyekuwa na chupa ya alabasta yenye marashi ya thamani kubwa, alimjia pale mezani alipokuwa amekaa kula chakula, akammiminia hayo marashi kichwani.
8 But when his disciples saw this, they were indignant, saying, “Why this waste?
Wanafunzi wake walipoona hayo wakakasirika, wakasema, “Ya nini hasara hii?
9 For this ointment might have been sold for much and given to the poor.”
Marashi haya yangaliweza kuuzwa kwa bei kubwa, maskini wakapewa hizo fedha.”
10 However, knowing this, Jesus said to them, “Why do you trouble the woman? She has done a good work for me.
Yesu alitambua mawazo yao, akawaambia, “Mbona mnamsumbua huyu mama? Yeye amenitendea jambo jema.
11 For you always have the poor with you, but you do not always have me.
Maskini mnao daima pamoja nanyi, lakini mimi sitakuwapo pamoja nanyi daima.
12 For in pouring this ointment on my body, she did it to prepare me for burial.
Huyu mama amenimiminia marashi ili kunitayarisha kwa maziko.
13 Most certainly I tell you, wherever this Good News is preached in the whole world, what this woman has done will also be spoken of as a memorial of her.”
Nawaambieni kweli, popote ambapo hii Habari Njema itahubiriwa ulimwenguni, kitendo hiki alichofanya mama huyu kitatajwa kwa kumkumbuka yeye.”
14 Then one of the twelve, who was called Judas Iscariot, went to the chief priests
Kisha, Yuda Iskarioti, mmoja wa wale kumi na wawili, akaenda kwa makuhani wakuu,
15 and said, “What are you willing to give me if I deliver him to you?” So they weighed out for him thirty pieces of silver.
akawaambia, “Mtanipa kitu gani kama nikimkabidhi Yesu kwenu?” Wakamhesabia sarafu thelathini za fedha;
16 From that time he sought opportunity to betray him.
na tangu wakati huo Yuda akawa anatafuta nafasi ya kumsaliti.
17 Now on the first day of unleavened bread, the disciples came to Jesus, saying to him, “Where do you want us to prepare for you to eat the Passover?”
Siku ya kwanza kabla ya Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, wanafunzi walimwendea Yesu wakamwuliza, “Unataka tukuandalie wapi chakula cha Pasaka?”
18 He said, “Go into the city to a certain person, and tell him, ‘The Teacher says, “My time is at hand. I will keep the Passover at your house with my disciples.”’”
Yeye akawajibu, “Nendeni mjini kwa mtu fulani, mkamwambie: Mwalimu anasema, wakati wangu umefika; kwako nitakula Pasaka pamoja na wanafunzi wangu.”
19 The disciples did as Jesus commanded them, and they prepared the Passover.
Wanafunzi wakafanya kama Yesu alivyowaagiza, wakaandaa Pasaka.
20 Now when evening had come, he was reclining at the table with the twelve disciples.
Kulipokuwa jioni, Yesu akakaa mezani pamoja na wanafunzi wake kumi na wawili.
21 As they were eating, he said, “Most certainly I tell you that one of you will betray me.”
Walipokuwa wakila, Yesu akasema, “Nawaambieni kweli, mmoja wenu atanisaliti.”
22 They were exceedingly sorrowful, and each began to ask him, “It is not me, is it, Lord?”
Wanafunzi wakahuzunika sana, wakaanza kuuliza mmojammoja, “Bwana! Je, ni mimi?”
23 He answered, “He who dipped his hand with me in the dish will betray me.
Yesu akajibu, “Atakayechovya mkate pamoja nami katika bakuli ndiye atakayenisaliti.
24 The Son of Man goes even as it is written of him, but woe to that man through whom the Son of Man is betrayed! It would be better for that man if he had not been born.”
Naam, Mwana wa Mtu anakwenda zake kama Maandiko Matakatifu yasemavyo, lakini ole wake mtu yule atakayemsaliti Mwana wa Mtu! Ingalikuwa afadhali kwa mtu huyo kama hangalizaliwa.”
25 Judas, who betrayed him, answered, “It is not me, is it, Rabbi?” He said to him, “You said it.”
Yuda, ambaye ndiye aliyetaka kumsaliti, akamwuliza, “Mwalimu! Je, ni mimi?” Yesu akamjibu, “Wewe umesema.”
26 As they were eating, Jesus took bread, gave thanks for it, and broke it. He gave to the disciples and said, “Take, eat; this is my body.”
Walipokuwa wanakula, Yesu akatwaa mkate, akashukuru, akaumega, akawapa wanafunzi wake akisema, “Twaeni mle; huu ni mwili wangu.”
27 He took the cup, gave thanks, and gave to them, saying, “All of you drink it,
Kisha akatwaa kikombe, akamshukuru Mungu, akawapa akisema, “Nyweni nyote;
28 for this is my blood of the new covenant, which is poured out for many for the remission of sins.
maana hii ni damu yangu inayothibitisha agano, damu inayomwagwa kwa ajili ya watu wengi ili kuwaondolea dhambi.
29 But I tell you that I will not drink of this fruit of the vine from now on, until that day when I drink it anew with you in my Father’s Kingdom.”
Nawaambieni, sitakunywa tena divai ya zabibu mpaka siku ile nitakapoinywa mpya pamoja nanyi katika Ufalme wa Baba yangu.”
30 When they had sung a hymn, they went out to the Mount of Olives.
Baada ya kuimba wimbo, wakaondoka, wakaenda katika mlima wa Mizeituni.
31 Then Jesus said to them, “All of you will be made to stumble because of me tonight, for it is written, ‘I will strike the shepherd, and the sheep of the flock will be scattered.’
Kisha Yesu akawaambia, “Usiku huu wa leo, ninyi nyote mtakuwa na mashaka nami, maana Maandiko Matakatifu yasema: Nitampiga mchungaji, na kondoo wa kundi watatawanyika.
32 But after I am raised up, I will go before you into Galilee.”
Lakini baada ya kufufuka kwangu, nitawatangulieni Galilaya.”
33 But Peter answered him, “Even if all will be made to stumble because of you, I will never be made to stumble.”
Petro akamwambia Yesu “Hata kama wote watakuwa na mashaka nawe na kukuacha, mimi sitakuacha kamwe.”
34 Jesus said to him, “Most certainly I tell you that tonight, before the rooster crows, you will deny me three times.”
Yesu akamwambia, “Kweli nakwambia, usiku huu kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.”
35 Peter said to him, “Even if I must die with you, I will not deny you.” All of the disciples also said likewise.
Petro akamwambia, “Hata kama ni lazima nife pamoja nawe, sitakukana kamwe.” Wale wanafunzi wengine wote wakasema vivyo hivyo.
36 Then Jesus came with them to a place called Gethsemane, and said to his disciples, “Sit here, while I go there and pray.”
Kisha Yesu akaenda pamoja nao bustanini Gethsemane, akawaambia wanafunzi wake, “Kaeni hapa nami niende pale mbele kusali.”
37 He took with him Peter and the two sons of Zebedee, and began to be sorrowful and severely troubled.
Akawachukua Petro na wana wawili wa Zebedayo, akaanza kuwa na huzuni na mahangaiko.
38 Then Jesus said to them, “My soul is exceedingly sorrowful, even to death. Stay here and watch with me.”
Hapo akawaambia, “Nina huzuni kubwa moyoni hata karibu kufa. Kaeni hapa mkeshe pamoja nami.”
39 He went forward a little, fell on his face, and prayed, saying, “My Father, if it is possible, let this cup pass away from me; nevertheless, not what I desire, but what you desire.”
Basi, akaenda mbele kidogo, akaanguka kifudifudi, akasali: “Baba yangu, kama inawezekana, aacha kikombe hiki cha mateso kinipite; lakini isiwe nitakavyo mimi, ila utakavyo wewe.”
40 He came to the disciples and found them sleeping, and said to Peter, “What, could not you watch with me for one hour?
Akawaendea wale wanafunzi, akawakuta wamelala. Akamwambia Petro, “Ndiyo kusema hamkuweza kukesha pamoja nami hata saa moja?
41 Watch and pray, that you do not enter into temptation. The spirit indeed is willing, but the flesh is weak.”
Kesheni na kusali ili msije mkaingia katika majaribu. Roho i tayari lakini mwili ni dhaifu.”
42 Again, a second time he went away and prayed, saying, “My Father, if this cup cannot pass away from me unless I drink it, your desire be done.”
Akaenda tena mara ya pili akasali: “Baba yangu, kama haiwezekani kikombe hiki kinipite bila mimi kukinywa, basi, mapenzi yako yafanyike.”
43 He came again and found them sleeping, for their eyes were heavy.
Akawaendea tena, akawakuta wamelala, maana macho yao yalikuwa yamebanwa na usingizi.
44 He left them again, went away, and prayed a third time, saying the same words.
Basi, akawaacha, akaenda tena kusali mara ya tatu kwa maneno yaleyale.
45 Then he came to his disciples and said to them, “Are you still sleeping and resting? Behold, the hour is at hand, and the Son of Man is betrayed into the hands of sinners.
Kisha akawaendea wale wanafunzi, akawaambia, “Je, mngali mmelala na kupumzika? Tazameni! Saa yenyewe imefika, na Mwana wa Mtu atatolewa kwa watu wenye dhambi.
46 Arise, let’s be going. Behold, he who betrays me is at hand.”
Amkeni, twendeni zetu. Tazameni! Anakuja yule atakayenisaliti.”
47 While he was still speaking, behold, Judas, one of the twelve, came, and with him a great multitude with swords and clubs, from the chief priests and elders of the people.
Basi, Yesu alipokuwa bado anasema nao, mara akaja Yuda, mmoja wa wale kumi na wawili. Pamoja naye walikuja watu wengi wenye mapanga na marungu ambao walitumwa na makuhani wakuu na wazee wa watu.
48 Now he who betrayed him had given them a sign, saying, “Whoever I kiss, he is the one. Seize him.”
Huyo aliyetaka kumsaliti Yesu, alikuwa amekwisha wapa ishara akisema: “Yule nitakayembusu ndiye; mkamateni.”
49 Immediately he came to Jesus, and said, “Greetings, Rabbi!” and kissed him.
Basi, Yuda akamkaribia Yesu, akamwambia, “Shikamoo, Mwalimu!” Kisha akambusu.
50 Jesus said to him, “Friend, why are you here?” Then they came and laid hands on Jesus, and took him.
Yesu akamwambia, “Rafiki, fanya ulichokuja kufanya.” Hapo wale watu wakaja, wakamkamata Yesu, wakamtia nguvuni.
51 Behold, one of those who were with Jesus stretched out his hand and drew his sword, and struck the servant of the high priest, and cut off his ear.
Mmoja wa wale waliokuwa pamoja na Yesu akanyosha mkono, akauchomoa upanga wake, akampiga mtumishi wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio.
52 Then Jesus said to him, “Put your sword back into its place, for all those who take the sword will die by the sword.
Hapo Yesu akamwambia, “Rudisha upanga wako alani, maana yeyote anayeutumia upanga, atakufa kwa upanga.
53 Or do you think that I could not ask my Father, and he would even now send me more than twelve legions of angels?
Je, hamjui kwamba ningeweza kumwomba Baba yangu naye mara angeniletea zaidi ya majeshi kumi na mawili ya malaika?
54 How then would the Scriptures be fulfilled that it must be so?”
Lakini yatatimiaje Maandiko Matakatifu yasemayo kwamba ndivyo inavyopaswa kuwa?”
55 In that hour Jesus said to the multitudes, “Have you come out as against a robber with swords and clubs to seize me? I sat daily in the temple teaching, and you did not arrest me.
Wakati huohuo Yesu akauambia huo umati wa watu waliokuja kumtia nguvuni, “Je, mmekuja kunikamata kwa mapanga na marungu kama kwamba mimi ni mnyang'anyi? Kila siku nilikuwa Hekaluni nikifundisha, na hamkunikamata!
56 But all this has happened that the Scriptures of the prophets might be fulfilled.” Then all the disciples left him and fled.
Lakini haya yote yametendeka ili Maandiko ya manabii yatimie.” Kisha wanafunzi wote wakamwacha, wakakimbia.
57 Those who had taken Jesus led him away to Caiaphas the high priest, where the scribes and the elders were gathered together.
Basi, hao watu waliomkamata Yesu walimpeleka nyumbani kwa Kayafa, Kuhani Mkuu, walikokusanyika walimu wa Sheria na wazee.
58 But Peter followed him from a distance to the court of the high priest, and entered in and sat with the officers, to see the end.
Petro alimfuata kwa mbali mpaka uani kwa Kuhani Mkuu, akaingia ndani pamoja na walinzi ili apate kuona mambo yatakavyokuwa.
59 Now the chief priests, the elders, and the whole council sought false testimony against Jesus, that they might put him to death,
Basi, makuhani wakuu na Baraza lote wakatafuta ushahidi wa uongo dhidi ya Yesu wapate kumwua,
60 and they found none. Even though many false witnesses came forward, they found none. But at last two false witnesses came forward
lakini hawakupata ushahidi wowote, ingawa walikuja mashahidi wengi wa uongo. Mwishowe wakaja mashahidi wawili,
61 and said, “This man said, ‘I am able to destroy the temple of God, and to build it in three days.’”
wakasema, “Mtu huyu alisema: Ninaweza kuliharibu Hekalu la Mungu na kulijenga tena kwa siku tatu.”
62 The high priest stood up and said to him, “Have you no answer? What is this that these testify against you?”
Kuhani Mkuu akasimama, akamwuliza Yesu, “Je, hujibu neno? Watu hawa wanashuhudia nini dhidi yako?”
63 But Jesus stayed silent. The high priest answered him, “I adjure you by the living God that you tell us whether you are the Christ, the Son of God.”
Lakini Yesu akakaa kimya. Kuhani Mkuu akamwambia, “Nakuapisha kwa Mungu aliye hai, twambie kama wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu!”
64 Jesus said to him, “You have said so. Nevertheless, I tell you, after this you will see the Son of Man sitting at the right hand of Power, and coming on the clouds of the sky.”
Yesu akamwambia, “Wewe umesema! Lakini nawaambieni, tangu sasa mtamwona Mwana wa Mtu ameketi upande wa kulia wa Mwenyezi, akija juu ya mawingu ya mbinguni.”
65 Then the high priest tore his clothing, saying, “He has spoken blasphemy! Why do we need any more witnesses? Behold, now you have heard his blasphemy.
Hapo, Kuhani Mkuu akararua mavazi yake, akasema, “Amekufuru! Tuna haja gani tena ya mashahidi? Sasa mmesikia kufuru yake.
66 What do you think?” They answered, “He is worthy of death!”
Ninyi mwaonaje?” Wao wakamjibu, “Anastahili kufa!”
67 Then they spat in his face and beat him with their fists, and some slapped him,
Kisha wakamtemea mate usoni, wakampiga makofi. Wengine wakiwa wanampiga makofi,
68 saying, “Prophesy to us, you Christ! Who hit you?”
wakasema, “Haya Kristo, tutabirie; ni nani amekupiga!”
69 Now Peter was sitting outside in the court, and a maid came to him, saying, “You were also with Jesus, the Galilean!”
Petro alikuwa ameketi nje uani. Basi, mtumishi mmoja wa kike akamwendea, akasema, “Wewe ulikuwa pamoja na Yesu wa Galilaya.”
70 But he denied it before them all, saying, “I do not know what you are talking about.”
Petro akakana mbele ya wote akisema, “Sijui hata unasema nini.”
71 When he had gone out onto the porch, someone else saw him and said to those who were there, “This man also was with Jesus of Nazareth.”
Alipokuwa akitoka mlangoni, mtumishi mwingine wa kike akamwona, akawaambia wale waliokuwa pale, “Mtu huyu alikuwa pamoja na Yesu wa Nazareti.”
72 Again he denied it with an oath, “I do not know the man.”
Petro akakana tena kwa kiapo: “Simjui mtu huyo.”
73 After a little while those who stood by came and said to Peter, “Surely you are also one of them, for your speech makes you known.”
Baadaye kidogo, watu waliokuwa pale wakamwendea Petro, wakamwambia, “Hakika, wewe pia ni mmoja wao, maana msemo wako unakutambulisha.”
74 Then he began to curse and to swear, “I do not know the man!” Immediately the rooster crowed.
Hapo Petro akaanza kujilaani na kuapa akisema, “Simjui mtu huyo!” Mara jogoo akawika.
75 Peter remembered the word which Jesus had said to him, “Before the rooster crows, you will deny me three times.” Then he went out and wept bitterly.
Petro akakumbuka maneno aliyoambiwa na Yesu: “Kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.” Basi, akatoka nje akalia sana.

< Matthew 26 >