< John 16 >

1 “I have said these things to you so that you would not be caused to stumble.
“Nimewaambieni hayo kusudi msiiache imani yenu.
2 They will put you out of the synagogues. Yes, the time is coming that whoever kills you will think that he offers service to God.
Watu watawatenga ninyi na masunagogi yao. Tena, wakati unakuja ambapo kila atakayewaua ninyi atadhani anamhudumia Mungu.
3 They will do these things because they have not known the Father nor me.
Watawatendeeni mambo hayo kwa sababu hawamjui Baba, wala hawanijui mimi.
4 But I have told you these things so that when the time comes, you may remember that I told you about them. I did not tell you these things from the beginning, because I was with you.
Basi, nimewaambieni mambo haya ili saa yake itakapofika mkumbuke kwamba niliwaambieni. “Sikuwaambieni mambo haya tangu mwanzo kwa sababu nilikuwa pamoja nanyi.
5 But now I am going to him who sent me, and none of you asks me, ‘Where are you going?’
Lakini sasa namwendea yule aliyenituma; na hakuna hata mmoja wenu anayeniuliza: Unakwenda wapi?
6 But because I have told you these things, sorrow has filled your heart.
Kwa kuwa nimewaambieni mambo hayo mmejaa huzuni mioyoni mwenu.
7 Nevertheless I tell you the truth: It is to your advantage that I go away; for if I do not go away, the Counselor will not come to you. But if I go, I will send him to you.
Lakini, nawaambieni ukweli: afadhali kwenu mimi niende zangu, maana nisipokwenda Msaidizi hatakuja kwenu. Lakini nikienda, basi, nitamtuma kwenu.
8 When he has come, he will convict the world about sin, about righteousness, and about judgment;
Naye atakapokuja atawathibitishia walimwengu kwamba wamekosea kuhusu dhambi, uadilifu na hukumu ya Mungu.
9 about sin, because they do not believe in me;
Wamekosea kuhusu dhambi kwa sababu hawaniamini;
10 about righteousness, because I am going to my Father, and you will not see me any more;
kuhusu uadilifu, kwa sababu naenda zangu kwa Baba, nanyi hamtaniona tena;
11 about judgment, because the prince of this world has been judged.
kuhusu hukumu kwa sababu mkuu wa ulimwengu huu amekwisha hukumiwa.
12 “I still have many things to tell you, but you cannot bear them now.
“Ninayo bado mengi ya kuwaambieni, ila kwa sasa hamwezi kuyastahimili.
13 However, when he, the Spirit of truth, has come, he will guide you into all truth, for he will not speak from himself; but whatever he hears, he will speak. He will declare to you things that are coming.
Lakini atakapokuja huyo Roho wa kweli atawaongoza kwenye ukweli wote; maana hatasema kwa mamlaka yake mwenyewe, bali atawaambieni yote atakayosikia, na atasema mambo yatakayokuwa yanakuja.
14 He will glorify me, for he will take from what is mine and will declare it to you.
Yeye atanitukuza mimi kwa kuwa atawaambieni yale atakayopata kutoka kwangu.
15 All things that the Father has are mine; therefore I said that he takes of mine and will declare it to you.
Vyote alivyo navyo Baba ni vyangu; ndiyo maana nimesema kwamba huyo Roho Mtakatifu atawaambieni yale atakayopata kutoka kwangu.
16 “A little while, and you will not see me. Again a little while, and you will see me.”
“Bado kitambo kidogo nanyi hamtaniona; na baada ya kitambo kidogo tena mtaniona!”
17 Some of his disciples therefore said to one another, “What is this that he says to us, ‘A little while, and you will not see me, and again a little while, and you will see me;’ and, ‘Because I go to the Father’?”
Hapo baadhi ya wanafunzi wake wakaulizana, “Ana maana gani anapotwambia: Bado kitambo kidogo nanyi hamtaniona; na baada ya kitambo kidogo tena mtaniona? Tena anasema: Kwa kuwa ninakwenda kwa Baba!”
18 They said therefore, “What is this that he says, ‘A little while’? We do not know what he is saying.”
Basi, wakawa wanaulizana, “Ana maana gani anaposema: Bado kitambo kidogo? Hatuelewi anaongelea nini.”
19 Therefore Jesus perceived that they wanted to ask him, and he said to them, “Do you inquire among yourselves concerning this, that I said, ‘A little while, and you will not see me, and again a little while, and you will see me’?
Yesu alijua kwamba walitaka kumwuliza, basi akawaambia, “Je, mnaulizana juu ya yale niliyosema: Bado kitambo kidogo nanyi hamtaniona; na baada ya kitambo kidogo tena mtaniona?
20 Most certainly I tell you that you will weep and lament, but the world will rejoice. You will be sorrowful, but your sorrow will be turned into joy.
Nawaambieni kweli, ninyi mtalia na kuomboleza, lakini ulimwengu utafurahi: mtaona huzuni lakini huzuni yenu itageuka kuwa furaha.
21 A woman, when she gives birth, has sorrow because her time has come. But when she has delivered the child, she does not remember the anguish any more, for the joy that a human being is born into the world.
Wakati mama anapojifungua huona huzuni kwa sababu saa ya maumivu imefika; lakini akisha jifungua hayakumbuki tena maumivu hayo kwa sababu ya furaha kwamba mtu amezaliwa duniani.
22 Therefore you now have sorrow, but I will see you again, and your heart will rejoice, and no one will take your joy away from you.
Ninyi pia mna huzuni sasa; lakini nitawajieni tena, nanyi mtajaa furaha mioyoni mwenu, na furaha hiyo hakuna mtu atakayeiondoa kwenu.
23 “In that day you will ask me no questions. Most certainly I tell you, whatever you may ask of the Father in my name, he will give it to you.
Siku hiyo hamtaniomba chochote. Kweli nawaambieni, chochote mtakachomwomba Baba kwa jina langu, atawapeni.
24 Until now, you have asked nothing in my name. Ask, and you will receive, that your joy may be made full.
Mpaka sasa hamjaomba chochote kwa jina langu. Ombeni nanyi mtapata ili furaha yenu ikamilike.
25 “I have spoken these things to you in figures of speech. But the time is coming when I will no more speak to you in figures of speech, but will tell you plainly about the Father.
“Nimewaambieni mambo hayo kwa mafumbo. Lakini wakati utakuja ambapo sitasema tena nanyi kwa mafumbo, bali nitawaambieni waziwazi juu ya Baba.
26 In that day you will ask in my name; and I do not say to you that I will pray to the Father for you,
Siku hiyo mtaomba kwa jina langu, na siwaambii kwamba nitamwomba Baba kwa niaba yenu;
27 for the Father himself loves you, because you have loved me, and have believed that I came from God.
maana yeye mwenyewe anawapenda ninyi, kwa sababu ninyi mmenipenda mimi na mmeamini kwamba nimetoka kwa Mungu.
28 I came from the Father and have come into the world. Again, I leave the world and go to the Father.”
Mimi nilitoka kwa Baba, nikaja ulimwenguni; na sasa nauacha ulimwengu na kurudi kwa Baba.”
29 His disciples said to him, “Behold, now you are speaking plainly, and using no figures of speech.
Basi, wanafunzi wake wakamwambia, “Ahaa! Sasa unasema waziwazi kabisa bila kutumia mafumbo.
30 Now we know that you know all things, and do not need for anyone to question you. By this we believe that you came from God.”
Sasa tunajua kwamba wewe unajua kila kitu, na huna haja ya kuulizwa maswali na mtu yeyote; kwa hiyo tunaamini kwamba umetoka kwa Mungu.”
31 Jesus answered them, “Do you now believe?
Yesu akawajibu, “Je, mnaamini sasa?
32 Behold, the time is coming, yes, and has now come, that you will be scattered, everyone to his own place, and you will leave me alone. Yet I am not alone, because the Father is with me.
Wakati unakuja, tena umekwisha fika, ambapo ninyi nyote mtatawanyika kila mtu kwake, nami nitaachwa peke yangu. Kumbe, lakini mimi siko peke yangu, maana Baba yu pamoja nami.
33 I have told you these things, that in me you may have peace. In the world you have trouble; but cheer up! I have overcome the world.”
Nimewaambieni mambo haya ili mpate kuwa na amani katika kuungana nami. Ulimwenguni mtapata masumbuko; lakini jipeni moyo! Mimi nimeushinda ulimwengu!”

< John 16 >