< Job 38 >

1 Then the LORD answered Job out of the whirlwind,
Kisha Bwana akamjibu Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli. Akasema:
2 “Who is this who darkens counsel by words without knowledge?
“Nani huyu atiaye mashauri yangu giza kwa maneno yasiyo na maarifa?
3 Brace yourself like a man, for I will question you, then you answer me!
Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza swali, nawe unijibu.
4 “Where were you when I laid the foundations of the earth? Declare, if you have understanding.
“Ulikuwa wapi nilipoweka misingi ya dunia? Niambie, kama unafahamu.
5 Who determined its measures, if you know? Or who stretched the line on it?
Ni nani aliyeweka alama vipimo vyake? Hakika wewe unajua! Ni nani aliyenyoosha kamba ya kupimia juu yake?
6 What were its foundations fastened on? Or who laid its cornerstone,
Je, misingi yake iliwekwa juu ya nini, au ni nani aliyeweka jiwe la pembeni,
7 when the morning stars sang together, and all the sons of God shouted for joy?
wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja, na malaika wote walipokuwa wakipiga kelele kwa furaha?
8 “Or who shut up the sea with doors, when it broke out of the womb,
“Ni nani aliyeifungia bahari milango ilipopasuka kutoka tumbo,
9 when I made clouds its garment, and wrapped it in thick darkness,
nilipoyafanya mawingu kuwa vazi lake, na kuyafungia katika giza nene,
10 marked out for it my bound, set bars and doors,
nilipoamuru mipaka yake, na kuiweka milango yake na makomeo mahali pake,
11 and said, ‘You may come here, but no further. Your proud waves shall be stopped here’?
niliposema, ‘Unaweza kufika mpaka hapa wala si zaidi; hapa ndipo mawimbi yako yenye kiburi yatakapokomea’?
12 “Have you commanded the morning in your days, and caused the dawn to know its place,
“Umepata kuiamrisha asubuhi ipambazuke, au kuyaonyesha mapambazuko mahali pake,
13 that it might take hold of the ends of the earth, and shake the wicked out of it?
yapate kushika miisho ya dunia, na kuwakungʼuta waovu waliomo?
14 It is changed as clay under the seal, and presented as a garment.
Dunia hubadilika kama udongo wa mfinyanzi chini ya lakiri; sura yake hukaa kama ile ya vazi.
15 From the wicked, their light is withheld. The high arm is broken.
Waovu huzuiliwa nuru yao, nao mkono wao ulioinuliwa huvunjwa.
16 “Have you entered into the springs of the sea? Or have you walked in the recesses of the deep?
“Je, umepata kufika kwenye chemchemi za bahari? Au kutembea mahali pa ndani pa vilindi?
17 Have the gates of death been revealed to you? Or have you seen the gates of the shadow of death?
Umewahi kuonyeshwa malango ya mauti? Umewahi kuiona milango ya uvuli wa mauti?
18 Have you comprehended the earth in its width? Declare, if you know it all.
Je, wewe unafahamu ukubwa wa dunia? Niambie kama unajua haya yote.
19 “What is the way to the dwelling of light? As for darkness, where is its place,
“Njia ya kufika kwenye makao ya nuru ni ipi? Nako maskani mwa giza ni wapi?
20 that you should take it to its bound, that you should discern the paths to its house?
Je, unaweza kuvirudisha kwenye makao yake? Unajua njia za kufika maskani mwake?
21 Surely you know, for you were born then, and the number of your days is great!
Hakika unajua, kwa kuwa ulikuwa umeshazaliwa! Kwani umeishi miaka mingi!
22 Have you entered the storehouses of the snow, or have you seen the storehouses of the hail,
“Je, umeshawahi kuingia katika ghala za theluji, au kuona ghala za mvua ya mawe,
23 which I have reserved against the time of trouble, against the day of battle and war?
ambazo nimeziweka akiba kwa ajili ya wakati wa taabu, na kwa ajili ya wakati wa vita na mapigano?
24 By what way is the lightning distributed, or the east wind scattered on the earth?
Ni ipi njia iendayo mahali umeme wa radi unapotawanyiwa, au mahali upepo wa mashariki unaposambaziwa juu ya dunia?
25 Who has cut a channel for the flood water, or the path for the thunderstorm,
Ni nani aliyepasua mifereji kwa ajili ya maji mengi ya mvua yaendayo kasi na njia ya umeme wa radi,
26 to cause it to rain on a land where there is no man, on the wilderness, in which there is no man,
ili kusababisha mvua kunyeshea mahali pasipokaliwa na mtu, jangwa lisilo na yeyote ndani yake,
27 to satisfy the waste and desolate ground, to cause the tender grass to grow?
ili kuitosheleza nchi ya ukiwa na jangwa, na majani yaanze kumea ndani yake?
28 Does the rain have a father? Or who fathers the drops of dew?
Je, mvua ina baba? Ni nani baba azaaye matone ya umande?
29 Whose womb did the ice come out of? Who has given birth to the gray frost of the sky?
Barafu inatoka tumbo la nani? Ni nani azaaye ukungu kutoka mbinguni,
30 The waters become hard like stone, when the surface of the deep is frozen.
wakati maji yawapo magumu kama jiwe, wakati uso wa vilindi vya maji unapoganda?
31 “Can you bind the cluster of the Pleiades, or loosen the cords of Orion?
“Je, waweza kuufunga mnyororo wa Kilimia? Waweza kulegeza kamba za Orioni?
32 Can you lead the constellations out in their season? Or can you guide the Bear with her cubs?
Waweza kuyaongoza makundi ya nyota kwa majira yake, au kuongoza Dubu na watoto wake?
33 Do you know the laws of the heavens? Can you establish its dominion over the earth?
Je, unajua sheria zinazotawala mbingu? Waweza kuweka utawala wa Mungu duniani?
34 “Can you lift up your voice to the clouds, that abundance of waters may cover you?
“Waweza kuiinua sauti yako mpaka mawinguni, na kujifunika mwenyewe na gharika ya maji?
35 Can you send out lightnings, that they may go? Do they report to you, ‘Here we are’?
Je, wewe hutuma umeme wa radi kwenye njia zake? Je, hutoa taarifa kwako kukuambia, ‘Sisi tuko hapa’?
36 Who has put wisdom in the inward parts? Or who has given understanding to the mind?
Ni nani aliyeujalia moyo hekima au kuzipa akili ufahamu?
37 Who can count the clouds by wisdom? Or who can pour out the containers of the sky,
Nani mwenye hekima ya kuyahesabu mawingu? Ni nani awezaye kuinamisha magudulia ya mbinguni
38 when the dust runs into a mass, and the clods of earth stick together?
wakati mavumbi yawapo magumu, na mabonge ya udongo kushikamana pamoja?
39 “Can you hunt the prey for the lioness, or satisfy the appetite of the young lions,
“Je, utamwindia simba jike mawindo, na kuwashibisha simba wenye njaa
40 when they crouch in their dens, and lie in wait in the thicket?
wakati wao wamejikunyata mapangoni mwao, au wakivizia kichakani?
41 Who provides for the raven his prey, when his young ones cry to God, and wander for lack of food?
Ni nani ampaye kunguru chakula wakati makinda yake yanamlilia Mungu, yakizungukazunguka kwa ajili ya kukosa chakula?

< Job 38 >