< Job 36 >

1 Elihu also continued, and said,
Elihu akaendelea kusema:
2 “Bear with me a little, and I will show you; for I still have something to say on God’s behalf.
“Nivumilie kidogo zaidi nami nitakuonyesha kwamba yako mengi zaidi ya kusemwa kwa ajili ya Mungu.
3 I will get my knowledge from afar, and will ascribe righteousness to my Maker.
Ninayapata maarifa yangu kutoka mbali, nami nitamhesabia haki Muumba wangu.
4 For truly my words are not false. One who is perfect in knowledge is with you.
Uwe na hakika kwamba maneno yangu si ya uongo; mmoja aliye mkamilifu katika maarifa yuko pamoja na wewe.
5 “Behold, God is mighty, and does not despise anyone. He is mighty in strength of understanding.
“Mungu ni mwenye nguvu, lakini hamdharau mwanadamu; ni mwenye nguvu, naye ni thabiti katika shauri lake.
6 He does not preserve the life of the wicked, but gives justice to the afflicted.
Hawaachi waovu waendelee kuishi, bali huwapa walioteswa haki yao.
7 He does not withdraw his eyes from the righteous, but with kings on the throne, he sets them forever, and they are exalted.
Yeye haondoi macho yake kwa wenye haki; huwaketisha penye viti vya enzi pamoja na wafalme na kuwatukuza milele.
8 If they are bound in fetters, and are taken in the cords of afflictions,
Lakini ikiwa watu wamefungwa kwenye minyororo, wakiwa wameshikiliwa na kamba za mateso,
9 then he shows them their work, and their transgressions, that they have behaved themselves proudly.
huwaonyesha yale waliyoyatenda, kwamba wametenda dhambi kwa majivuno.
10 He also opens their ears to instruction, and commands that they return from iniquity.
Huwafanya wao kusikia maonyo, na huwaagiza kutubu uovu wao.
11 If they listen and serve him, they will spend their days in prosperity, and their years in pleasures.
Kama wakitii na kumtumikia, wataishi siku zao zilizobaki katika mafanikio, na miaka yao katika utoshelevu.
12 But if they do not listen, they will perish by the sword; they will die without knowledge.
Lakini wasiposikiliza, wataangamia kwa upanga, nao watakufa pasipo maarifa.
13 “But those who are godless in heart lay up anger. They do not cry for help when he binds them.
“Wasiomcha Mungu moyoni mwao huficha chuki; hata anapowafunga, hawamwombi msaada.
14 They die in youth. Their life perishes among the unclean.
Wanakufa wangali vijana, miongoni mwa wanaume hanithi wa mahali pa kuabudia miungu.
15 He delivers the afflicted by their affliction, and opens their ear in oppression.
Bali wao wanaoteseka huwaokoa katika mateso yao, na kuzungumza nao katika dhiki zao.
16 Yes, he would have allured you out of distress, into a wide place, where there is no restriction. That which is set on your table would be full of fatness.
“Yeye anakubembeleza utoke katika mataya ya dhiki, ili kukuweka mahali palipo na nafasi mbali na kizuizi, hadi kwenye meza yako ya faraja iliyojaa vyakula vizuri.
17 “But you are full of the judgment of the wicked. Judgment and justice take hold of you.
Lakini sasa umelemewa na hukumu kwa ajili ya uovu; hukumu na haki vimekukamata.
18 Do not let riches entice you to wrath, neither let the great size of a bribe turn you aside.
Uwe mwangalifu ili yeyote asikushawishi kwa utajiri; usipotoshwe kwa fungu kubwa la rushwa.
19 Would your wealth sustain you in distress, or all the might of your strength?
Je, utajiri wako hata nguvu zako nyingi vinaweza kukusaidia usiingie kwenye dhiki?
20 Do not desire the night, when people are cut off in their place.
Usiutamani usiku uje, ili uwaburute watu mbali na nyumba zao.
21 Take heed, do not regard iniquity; for you have chosen this rather than affliction.
Jihadhari usigeukie uovu, ambao unaupenda zaidi kuliko mateso.
22 Behold, God is exalted in his power. Who is a teacher like him?
“Mungu ametukuzwa katika nguvu zake. Ni nani aliye mwalimu kama yeye?
23 Who has prescribed his way for him? Or who can say, ‘You have committed unrighteousness’?
Ni nani aliyemwelekeza katika njia zake, au kumwambia, ‘Wewe umetenda yasiyo sawa’?
24 “Remember that you magnify his work, about which men have sung.
Kumbuka kuzitukuza kazi zake, ambazo watu wamezisifu katika wimbo.
25 All men have looked on it. Man sees it afar off.
Wanadamu wote wameiona; watu wanaikazia macho kwa mbali.
26 Behold, God is great, and we do not know him. The number of his years is unsearchable.
Tazama jinsi Mungu alivyo mkuu, kupita ufahamu wetu! Hesabu ya miaka yake haitafutiki.
27 For he draws up the drops of water, which distill in rain from his vapor,
“Yeye huvuta juu matone ya maji, ayachujayo kama mvua kutoka kwenye vijito;
28 which the skies pour down and which drop on man abundantly.
mawingu huangusha chini maji yake, nayo mvua nyingi huwanyeshea wanadamu.
29 Indeed, can anyone understand the spreading of the clouds and the thunderings of his pavilion?
Ni nani ajuaye jinsi ayatandazavyo mawingu, jinsi angurumavyo kutoka hemani mwake.
30 Behold, he spreads his light around him. He covers the bottom of the sea.
Tazama jinsi anavyotandaza umeme wa radi kumzunguka, naye huvifunika vilindi vya bahari.
31 For by these he judges the people. He gives food in abundance.
Hivi ndivyo atawalavyo mataifa, na kuwapa chakula kwa wingi.
32 He covers his hands with the lightning, and commands it to strike the mark.
Huujaza mkono wake kwa umeme wa radi, na kuuagiza kulenga shabaha yake.
33 Its noise tells about him, and the livestock also, concerning the storm that comes up.
Ngurumo zake hutangaza dhoruba inayokuja; hata mifugo hujulisha kukaribia kwake.

< Job 36 >