< Job 14 >

1 “Man, who is born of a woman, is of few days, and full of trouble.
“Mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke siku zake ni chache nazo zimejaa taabu.
2 He grows up like a flower, and is cut down. He also flees like a shadow, and does not continue.
Huchanua kama ua kisha hunyauka; huwa kama kivuli kipitacho upesi, wala hadumu.
3 Do you open your eyes on such a one, and bring me into judgment with you?
Je, unamwekea jicho lako mtu kama huyo? Je, utamleta mbele yako katika hukumu?
4 Who can bring a clean thing out of an unclean? Not one.
Ni nani awezaye kutoa kitu safi kutoka kitu najisi? Hakuna awezaye!
5 Seeing his days are determined, the number of his months is with you, and you have appointed his bounds that he cannot pass.
Siku za mwanadamu zimewekewa mpaka; umekwisha kutangaza idadi ya miezi yake na kuweka mpaka ambao hawezi kuuvuka.
6 Look away from him, that he may rest, until he accomplishes, as a hireling, his day.
Hivyo angalia mbali umwache, hadi awe amekamilisha muda wake kama mtu aliyeajiriwa.
7 “For there is hope for a tree if it is cut down, that it will sprout again, that the tender branch of it will not cease.
“Kwa maana lipo tumaini kwa mti; kama ukikatwa utachipuka tena, nayo machipukizi yake mapya hayatakoma.
8 Though its root grows old in the earth, and its stock dies in the ground,
Mizizi yake yaweza kuchakaa ardhini na kisiki chake kufa udongoni,
9 yet through the scent of water it will bud, and sprout boughs like a plant.
lakini kwa kupata dalili ya maji utachipua na kutoa machipukizi kama mche.
10 But man dies, and is laid low. Yes, man gives up the spirit, and where is he?
Lakini mwanadamu hufa, na huo ndio mwisho wake; hutoa pumzi ya mwisho, naye hayuko tena!
11 As the waters fail from the sea, and the river wastes and dries up,
Kama vile maji yatowekavyo katika bahari, au mkondo wa mto ukaushwavyo na kuwa mkavu,
12 so man lies down and does not rise. Until the heavens are no more, they will not awake, nor be roused out of their sleep.
ndivyo mwanadamu alalavyo chini asiamke; hadi mbingu zitakapokuwa hazipo tena, wanadamu hawataamka au kuamshwa kutoka kwenye usingizi wao.
13 "Oh that you would hide me in Sheol (Sheol h7585), that you would keep me secret until your wrath is past, that you would appoint me a set time and remember me!
“Laiti kama ungenificha kaburini, na kunisitiri hadi hasira yako ipite! Laiti ungeniwekea wakati, na kisha ukanikumbuka! (Sheol h7585)
14 If a man dies, will he live again? I would wait all the days of my warfare, until my release should come.
Je, kama mtu akifa, aweza kuishi tena? Siku zote za kazi zangu ngumu nitangojea kufanywa upya kwangu.
15 You would call, and I would answer you. You would have a desire for the work of your hands.
Utaniita nami nitakuitika; utakionea shauku kiumbe ambacho mikono yako ilikiumba.
16 But now you count my steps. Do not you watch over my sin?
Hakika ndipo utakapozihesabu hatua zangu, lakini hutazifuatia dhambi zangu.
17 My disobedience is sealed up in a bag. You fasten up my iniquity.
Makosa yangu yatafungiwa kwa lakiri kwenye mfuko, nawe utazifunika dhambi zangu.
18 “But the mountain falling comes to nothing. The rock is removed out of its place.
“Lakini kama mlima umomonyokavyo na kufikichika na kama vile mwamba uondolewavyo mahali pake,
19 The waters wear the stones. The torrents of it wash away the dust of the earth. So you destroy the hope of man.
kama maji yamalizavyo mawe, na mafuriko yachukuavyo udongo, ndivyo unavyoharibu tegemeo la mwanadamu.
20 You forever prevail against him, and he departs. You change his face, and send him away.
Humshinda mara moja kwa daima, naye hutoweka; waibadilisha sura yake na kumwondoa.
21 His sons come to honor, and he does not know it. They are brought low, but he does not perceive it of them.
Kama wanawe wakipewa heshima, yeye hafahamu; kama wakidharauliwa, yeye haoni.
22 But his flesh on him has pain, and his soul within him mourns.”
Yeye hasikii kingine isipokuwa maumivu ya mwili wake mwenyewe, naye huomboleza kwa ajili yake mwenyewe.”

< Job 14 >