< Hosea 13 >

1 When Ephraim spoke, there was trembling. He exalted himself in Israel, but when he became guilty through Baal, he died.
Wakati Efraimu alipozungumza, watu walitetemeka, alikuwa ametukuzwa katika Israeli. Lakini alikuwa na hatia ya kumwabudu Baali naye akafa.
2 Now they sin more and more, and have made themselves molten images of their silver, even idols according to their own understanding, all of them the work of the craftsmen. They say of them, ‘They offer human sacrifice and kiss the calves.’
Sasa wanatenda dhambi zaidi na zaidi; wanajitengenezea sanamu kutokana na fedha yao, vinyago vilivyotengenezwa kwa uhodari, vyote kazi ya fundi stadi. Inasemekana kuhusu hawa watu, “Hutoa dhabihu za binadamu na kubusu sanamu za ndama.”
3 Therefore they will be like the morning mist, like the dew that passes away early, like the chaff that is driven with the whirlwind out of the threshing floor, and like the smoke out of the chimney.
Kwa hiyo watakuwa kama ukungu wa asubuhi, kama umande wa alfajiri utowekao, kama makapi yapeperushwayo kutoka sakafu ya kupuria nafaka, kama moshi utorokao kupitia dirishani.
4 “Yet I am the LORD your God from the land of Egypt; and you shall acknowledge no god but me, and besides me there is no savior.
“Bali mimi ndimi Bwana Mungu wenu, niliyewaleta ninyi toka Misri. Msimkubali Mungu mwingine ila mimi, hakuna Mwokozi isipokuwa mimi.
5 I knew you in the wilderness, in the land of great drought.
Niliwatunza huko jangwani, katika nchi yenye joto liunguzalo.
6 According to their pasture, so were they filled; they were filled, and their heart was exalted. Therefore they have forgotten me.
Nilipowalisha, walishiba, waliposhiba, wakajivuna, kisha wakanisahau mimi.
7 Therefore I am like a lion to them. Like a leopard, I will lurk by the path.
Kwa hiyo nitakuja juu yao kama simba, kama chui nitawavizia kando ya njia.
8 I will meet them like a bear that is bereaved of her cubs, and will tear the covering of their heart. There I will devour them like a lioness. The wild animal will tear them.
Kama dubu aliyenyangʼanywa watoto wake, nitawashambulia na kurarua vifua vyenu. Kama simba nitawala; mnyama pori atawararua vipande vipande.
9 You are destroyed, Israel, because you are against me, against your helper.
“Ee Israeli, umeangamizwa, kwa sababu wewe u kinyume nami, kinyume na msaidizi wako.
10 Where is your king now, that he may save you in all your cities? And your judges, of whom you said, ‘Give me a king and princes’?
Yuko wapi mfalme wako, ili apate kukuokoa? Wako wapi watawala wako katika miji yako yote ambao ulisema kuwahusu, ‘Nipe mfalme na wakuu’?
11 I have given you a king in my anger, and have taken him away in my wrath.
Hivyo katika hasira yangu nilikupa mfalme na katika ghadhabu yangu nilimwondoa.
12 The guilt of Ephraim is stored up. His sin is stored up.
Kosa la Efraimu limehifadhiwa, dhambi zake zimewekwa katika kumbukumbu.
13 The sorrows of a travailing woman will come on him. He is an unwise son, for when it is time, he does not come to the opening of the womb.
Utungu kama wa mwanamke anayejifungua mtoto humjia, lakini yeye ni mtoto asiyekuwa na hekima; wakati utakapowadia hatatoka katika tumbo la mama yake.
14 I will ransom them from the power of Sheol (Sheol h7585). I will redeem them from death! Death, where are your plagues? Sheol (Sheol h7585), where is your destruction? "Compassion will be hidden from my eyes.
“Nitawakomboa watu hawa kutoka nguvu za kaburi, nitawakomboa kutoka mautini. Yako wapi, ee mauti, mateso yako? Uko wapi, ee kuzimu, uharibifu wako? “Sitakuwa na huruma, (Sheol h7585)
15 Though he is fruitful among his brothers, an east wind will come, the breath of the LORD coming up from the wilderness; and his spring will become dry, and his fountain will be dried up. He will plunder the storehouse of treasure.
hata ingawa Efraimu atastawi miongoni mwa ndugu zake. Upepo wa mashariki kutoka kwa Bwana utakuja, ukivuma kutoka jangwani, chemchemi yake haitatoa maji na kisima chake kitakauka. Ghala lake litatekwa hazina zake zote.
16 Samaria will bear her guilt, for she has rebelled against her God. They will fall by the sword. Their infants will be dashed in pieces, and their pregnant women will be ripped open.”
Watu wa Samaria ni lazima wabebe hatia yao, kwa sababu wameasi dhidi ya Mungu wao. Wataanguka kwa upanga; watoto wao wadogo watatupwa kwa nguvu ardhini, wanawake wao walio na mimba watatumbuliwa.”

< Hosea 13 >