< Deuteronomy 27 >

1 Moses and the elders of Israel commanded the people, saying, “Keep all the commandment which I command you today.
Mose na wazee wa Israeli wakawaagiza watu: “Yashikeni maagizo haya yote ninayowaagiza leo.
2 It shall be on the day when you shall pass over the Jordan to the land which the LORD your God gives you, that you shall set yourself up great stones, and coat them with plaster.
Mtakapokuwa mmevuka Mto Yordani na kuingia katika nchi awapayo Bwana Mungu wenu, msimamishe mawe makubwa na mkayatie lipu.
3 You shall write on them all the words of this law, when you have passed over, that you may go in to the land which the LORD your God gives you, a land flowing with milk and honey, as the LORD, the God of your fathers, has promised you.
Andikeni juu yake maneno yote ya sheria hii wakati mtakapokuwa mmevuka na kuingia katika nchi awapayo Bwana Mungu wenu, nchi itiririkayo maziwa na asali, kama vile Bwana, Mungu wa baba zenu, alivyowaahidi.
4 It shall be, when you have crossed over the Jordan, that you shall set up these stones, which I command you today, on Mount Ebal, and you shall coat them with plaster.
Mtakapokuwa mmevuka Yordani, simamisheni mawe haya juu ya Mlima Ebali, kama ninavyowaagiza leo, mkayatie lipu.
5 There you shall build an altar to the LORD your God, an altar of stones. You shall not use any iron tool on them.
Huko mjengeeni Bwana Mungu wenu madhabahu, madhabahu ya mawe. Msitumie kifaa chochote cha chuma juu yake.
6 You shall build the LORD your God’s altar of uncut stones. You shall offer burnt offerings on it to the LORD your God.
Jengeni madhabahu ya Bwana Mungu wenu kwa mawe ya shambani, na mtoe sadaka za kuteketezwa juu yake kwa Bwana Mungu wenu.
7 You shall sacrifice peace offerings, and shall eat there. You shall rejoice before the LORD your God.
Toeni sadaka za amani juu yake, mkizila na kufurahia mbele za Bwana Mungu wenu.
8 You shall write on the stones all the words of this law very plainly.”
Nanyi mtaandika maneno yote ya sheria hii kwa wazi sana juu ya mawe haya ambayo mmesimamisha.”
9 Moses and the Levitical priests spoke to all Israel, saying, “Be silent and listen, Israel! Today you have become the people of the LORD your God.
Kisha Mose na makuhani, ambao ni Walawi, wakawaambia Israeli wote, “Nyamaza ee Israeli, sikiliza! Sasa umekuwa taifa la Bwana Mungu wako.
10 You shall therefore obey the LORD your God’s voice, and do his commandments and his statutes, which I command you today.”
Mtii Bwana Mungu wako, na kufuata amri zake na maagizo ninayokupa leo.”
11 Moses commanded the people the same day, saying,
Siku ile ile Mose akawaagiza watu:
12 “These shall stand on Mount Gerizim to bless the people, when you have crossed over the Jordan: Simeon, Levi, Judah, Issachar, Joseph, and Benjamin.
Mtakapovuka Mto Yordani, makabila haya yatasimama juu ya Mlima Gerizimu kubariki watu: Simeoni, Lawi, Yuda, Isakari, Yosefu na Benyamini.
13 These shall stand on Mount Ebal for the curse: Reuben, Gad, Asher, Zebulun, Dan, and Naphtali.
Makabila haya yatasimama juu ya Mlima Ebali kwa kutamka laana: Reubeni, Gadi, Asheri, Zabuloni, Dani na Naftali.
14 With a loud voice, the Levites shall say to all the men of Israel,
Nao Walawi watawasomea watu wote wa Israeli kwa sauti kubwa:
15 ‘Cursed is the man who makes an engraved or molten image, an abomination to the LORD, the work of the hands of the craftsman, and sets it up in secret.’ All the people shall answer and say, ‘Amen.’
“Alaaniwe mtu afanyaye sanamu ya kuchonga au mwenye kusubu sanamu, kitu ambacho ni chukizo kwa Bwana, kazi ya mikono ya fundi stadi, na kuisimamisha kwa siri.”
16 ‘Cursed is he who dishonors his father or his mother.’ All the people shall say, ‘Amen.’
“Alaaniwe mtu amdharauye baba yake na mama yake.”
17 ‘Cursed is he who removes his neighbor’s landmark.’ All the people shall say, ‘Amen.’
“Alaaniwe mtu asogezaye jiwe la mpaka wa jirani yake.”
18 ‘Cursed is he who leads the blind astray on the road.’ All the people shall say, ‘Amen.’
“Alaaniwe mtu ampotoshaye kipofu njiani.”
19 ‘Cursed is he who withholds justice from the foreigner, fatherless, and widow.’ All the people shall say, ‘Amen.’
“Alaaniwe mtu apotoshaye haki ya mgeni, yatima au mjane.”
20 ‘Cursed is he who lies with his father’s wife, because he dishonors his father’s bed.’ All the people shall say, ‘Amen.’
“Alaaniwe mtu akutanaye kimwili na mke wa baba yake, kwa maana anadharau malazi ya baba yake.”
21 ‘Cursed is he who lies with any kind of animal.’ All the people shall say, ‘Amen.’
“Alaaniwe mtu akutanaye kimwili na mnyama yeyote.”
22 ‘Cursed is he who lies with his sister, his father’s daughter or his mother’s daughter.’ All the people shall say, ‘Amen.’
“Alaaniwe mtu akutanaye kimwili na dada yake, binti wa baba yake au binti wa mama yake.”
23 ‘Cursed is he who lies with his mother-in-law.’ All the people shall say, ‘Amen.’
“Alaaniwe mtu akutanaye kimwili na mama mkwe wake.”
24 ‘Cursed is he who secretly kills his neighbor.’ All the people shall say, ‘Amen.’
“Alaaniwe mtu amuuaye jirani yake kwa siri.”
25 ‘Cursed is he who takes a bribe to kill an innocent person.’ All the people shall say, ‘Amen.’
“Alaaniwe mtu apokeaye rushwa ili kumuua mtu asiye na hatia.”
26 ‘Cursed is he who does not uphold the words of this law by doing them.’ All the people shall say, ‘Amen.’”
“Alaaniwe mtu yule ambaye hatashikilia maneno ya sheria hii kwa kuyatekeleza.”

< Deuteronomy 27 >