< Deuteronomy 23 >

1 He who is emasculated by crushing or cutting shall not enter into the LORD’s assembly.
Asiingie mtu yeyote aliyehasiwa kwa kupondwa makende au kwa kukatwa uume wake katika kusanyiko la Bwana.
2 A person born of a forbidden union shall not enter into the LORD’s assembly; even to the tenth generation shall no one of his enter into the LORD’s assembly.
Mtu yeyote ambaye amezaliwa kwenye ndoa isiyo halali au wazao wake wasiingie kwenye kusanyiko la Bwana, hata mpaka kizazi cha kumi.
3 An Ammonite or a Moabite shall not enter into the LORD’s assembly; even to the tenth generation shall no one belonging to them enter into the LORD’s assembly forever,
Hapatakuwa na Mwamoni au Mmoabu au yeyote wa wazao wao atakayeruhusiwa kuingia katika kusanyiko la Bwana, hata mpaka kizazi cha kumi.
4 because they did not meet you with bread and with water on the way when you came out of Egypt, and because they hired against you Balaam the son of Beor from Pethor of Mesopotamia, to curse you.
Kwa kuwa hawakuja kuwalaki wakiwa na mkate na maji mlipokuwa njiani mlipotoka Misri, tena walimwajiri Balaamu mwana wa Beori kutoka Pethori iliyoko Aramu-Naharaimu ili kuwalaani ninyi.
5 Nevertheless the LORD your God would not listen to Balaam, but the LORD your God turned the curse into a blessing to you, because the LORD your God loved you.
Hata hivyo, Bwana Mungu wenu hakumsikiliza Balaamu bali aligeuza laana kuwa baraka kwenu kwa sababu Bwana Mungu wenu anawapenda.
6 You shall not seek their peace nor their prosperity all your days forever.
Msitafute mapatano ya urafiki nao maisha yenu yote.
7 You shall not abhor an Edomite, for he is your brother. You shall not abhor an Egyptian, because you lived as a foreigner in his land.
Usimchukie Mwedomu, kwa kuwa yeye ni ndugu yako. Usimchukie Mmisri, kwa sababu uliishi kama mgeni katika nchi yake.
8 The children of the third generation who are born to them may enter into the LORD’s assembly.
Kizazi cha tatu cha watoto watakaozaliwa nao wanaweza kuingia katika kusanyiko la Bwana.
9 When you go out and camp against your enemies, then you shall keep yourselves from every evil thing.
Unapokuwa umepiga kambi dhidi ya adui zako, jitenge na kitu chochote kisicho safi.
10 If there is among you any man who is not clean by reason of that which happens to him by night, then shall he go outside of the camp. He shall not come within the camp;
Ikiwa mtu amechafuka kwa sababu ya kutokwa na shahawa usiku, inampasa atoke nje ya kambi na kukaa huko.
11 but it shall be, when evening comes, he shall bathe himself in water. When the sun is down, he shall come within the camp.
Lakini jioni ikikaribia ataoga, na baada ya jua kuzama ataingia tena kambini.
12 You shall have a place also outside of the camp where you go relieve yourself.
Tengeni mahali nje ya kambi ambapo mnaweza kwenda kujisaidia.
13 You shall have a trowel among your weapons. It shall be, when you relieve yourself, you shall dig with it, and shall turn back and cover your excrement;
Kama sehemu ya vifaa vyenu kuweni na kitu cha kulimia, nanyi mnapojisaidia, chimba shimo na kisha funika kile kikutokacho.
14 for the LORD your God walks in the middle of your camp, to deliver you, and to give up your enemies before you. Therefore your camp shall be holy, that he may not see an unclean thing in you, and turn away from you.
Kwa kuwa Bwana Mungu wenu hutembea katika kambi yenu ili kuwalinda na kuwaweka adui zenu mikononi mwenu. Kambi yenu ni lazima iwe takatifu, ili asione kitu chochote miongoni mwenu kilicho kichafu akageuka na kuwaacha.
15 You shall not deliver to his master a servant who has escaped from his master to you.
Ikiwa mtumwa amekimbilia kwako, usimrudishe kwa bwana wake.
16 He shall dwell with you, among you, in the place which he shall choose within one of your gates, where it pleases him best. You shall not oppress him.
Mwache aishi miongoni mwenu mahali popote anapopapenda na katika mji wowote anaochagua. Usimwonee.
17 There shall be no prostitute of the daughters of Israel, neither shall there be a sodomite of the sons of Israel.
Asiwepo Mwisraeli mwanamke kahaba au mwanaume hanithi wa mahali pa kuabudia miungu.
18 You shall not bring the hire of a prostitute, or the wages of a male prostitute, into the house of the LORD your God for any vow; for both of these are an abomination to the LORD your God.
Kamwe usilete mapato ya ukahaba ikiwa ni ya mwanamke au ni ya mwanaume katika nyumba ya Bwana Mungu wako kwa ajili ya nadhiri yoyote, kwa sababu Bwana Mungu wako anachukizwa na yote mawili.
19 You shall not lend on interest to your brother: interest of money, interest of food, interest of anything that is lent on interest.
Usimtoze ndugu yako riba, iwe ni fedha ama chakula ama kitu kingine chochote ambacho waweza kupata riba juu yake.
20 You may charge a foreigner interest; but you shall not charge your brother interest, that the LORD your God may bless you in all that you put your hand to, in the land where you go in to possess it.
Unaweza kumtoza mgeni riba, lakini siyo nduguyo Mwisraeli, ili kwamba Bwana Mungu wako akubariki katika kila kitu unachoweka mkono katika nchi unayoingia kuimiliki.
21 When you vow a vow to the LORD your God, you shall not be slack to pay it, for the LORD your God will surely require it of you; and it would be sin in you.
Ukiweka nadhiri kwa Bwana Mungu wako, usichelewe kuitimiza, kwa kuwa Bwana Mungu wako atakudai, nawe utakuwa na hatia ya dhambi.
22 But if you refrain from making a vow, it shall be no sin in you.
Lakini ukijizuia kuweka nadhiri, hutakuwa na hatia.
23 You shall observe and do that which has gone out of your lips. Whatever you have vowed to the LORD your God as a free will offering, which you have promised with your mouth, you must do.
Chochote kitakachotamkwa kwa midomo yako ni lazima uhakikishe umekifanya, kwa sababu uliweka nadhiri yako kwa hiari mbele za Bwana Mungu wako kwa kinywa chako mwenyewe.
24 When you come into your neighbor’s vineyard, then you may eat your fill of grapes at your own pleasure; but you shall not put any in your container.
Kama ukiingia katika shamba la mizabibu la jirani yako, unaweza kula zabibu kadiri utakavyo, lakini usiweke chochote kwenye kikapu chako.
25 When you come into your neighbor’s standing grain, then you may pluck the ears with your hand; but you shall not use a sickle on your neighbor’s standing grain.
Kama ukiingia katika shamba la nafaka la jirani yako, unaweza kukwanyua kwa mikono yako, lakini usikate kwa mundu nafaka iliyosimama.

< Deuteronomy 23 >