< Zechariah 1 >

1 In the eighth month, in the second year of Darius, the word of Jehovah came to Zechariah the son of Berechiah, the son of Iddo, the prophet, saying,
Katika mwezi wa nane wa mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario, neno la Bwana lilimjia nabii Zekaria mwana wa Berekia, mwana wa Ido, kusema:
2 Jehovah was greatly displeased with your fathers.
“Bwana aliwakasirikia sana baba zako wa zamani.
3 Therefore say thou to them, Thus says Jehovah of hosts: Return to me, says Jehovah of hosts, and I will return to you, says Jehovah of hosts.
Kwa hiyo waambie watu: Hivi ndivyo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemavyo: ‘Nirudieni mimi,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, ‘nami nitawarudia ninyi,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
4 Be ye not as your fathers, to whom the former prophets cried, saying, Thus says Jehovah of hosts: Return ye now from your evil ways, and from your evil doings, but they did not hear, nor hearken to me, says Jehovah.
Msiwe kama baba zenu, ambao manabii waliotangulia waliwatangazia: Hivi ndivyo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemavyo: ‘Geukeni, mziache njia zenu mbaya na matendo yenu maovu.’ Lakini hawakunisikiliza wala kufuata maelekezo yangu, asema Bwana.
5 Your fathers, where are they? And the prophets, do they live forever?
Wako wapi baba zako sasa? Nao manabii, je, wanaishi milele?
6 But my words and my statutes, which I commanded my servants the prophets, did they not overtake your fathers? And they turned and said, Like as Jehovah of hosts thought to do to us, according to our ways, and according to our doings, so he has dealt with us.
Je, maneno yangu na amri zangu nilizowaagiza manabii watumishi wangu, hayakuwapata baba zenu?” “Kisha walitubu na kusema, ‘Bwana Mwenye Nguvu Zote ametutenda sawasawa na njia zetu na matendo yetu yalivyostahili, kama alivyokusudia kufanya.’”
7 Upon the twenty-fourth day of the eleventh month, which is the month Shebat, in the second year of Darius, the word of Jehovah came to Zechariah the son of Berechiah, the son of Iddo, the prophet, saying,
Katika siku ya ishirini na nne ya mwezi wa kumi na moja, yaani mwezi uitwao Shebati, katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario, neno la Bwana lilimjia nabii Zekaria mwana wa Berekia mwana wa Ido.
8 I saw in the night, and, behold, a man riding upon a red horse, and he stood among the myrtle trees that were in the bottom. And behind him there were horses, red, sorrel, and white.
Wakati wa usiku nilipata maono, mbele yangu alikuwepo mtu akiendesha farasi mwekundu! Alikuwa amesimama katikati ya miti ya mihadasi kwenye bonde. Nyuma yake walikuwepo farasi wekundu, wa kikahawia na weupe.
9 Then I said, O my lord, what are these? And the agent who talked with me said to me, I will show thee what these are.
Nikauliza, “Hivi ni vitu gani bwana wangu?” Malaika aliyekuwa akizungumza na mimi akanijibu, “Nitakuonyesha kuwa ni nini.”
10 And the man who stood among the myrtle trees answered and said, These are they whom Jehovah has sent to walk to and fro through the earth.
Kisha yule mtu aliyesimama katikati ya miti ya mihadasi akaeleza, “Ni wale ambao Bwana amewatuma waende duniani kote.”
11 And they answered the agent of Jehovah who stood among the myrtle trees, and said, We have walked to and fro through the earth, and, behold, all the earth sits still, and is at rest.
Nao wakatoa taarifa kwa yule malaika wa Bwana, aliyekuwa amesimama katikati ya miti ya mihadasi, “Tumepita duniani kote na kukuta ulimwengu wote umepumzika kwa amani.”
12 Then the agent of Jehovah answered and said, O Jehovah of hosts, how long will thou not have mercy on Jerusalem and on the cities of Judah, against which thou have had indignation these seventy years?
Kisha malaika wa Bwana akasema, “Bwana Mwenye Nguvu Zote, utazuia mpaka lini rehema kutoka Yerusalemu na miji ya Yuda, ambayo umeikasirikia kwa miaka hii sabini?”
13 And Jehovah answered the agent who talked with me with good words, comforting words.
Kwa hiyo Bwana akazungumza maneno ya upole na ya kufariji kwa malaika aliyezungumza nami.
14 So the agent who talked with me said to me, Cry thou, saying, Thus says Jehovah of hosts: I am jealous for Jerusalem and for Zion with a great jealousy.
Kisha malaika yule aliyekuwa akizungumza nami akasema, “Tangaza neno hili: Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: ‘Nina wivu sana kwa ajili ya Yerusalemu na Sayuni,
15 And I am very greatly displeased with the nations that are at ease. For I was but a little displeased, and they helped forward the affliction.
lakini nimeyakasirikia sana mataifa yanayojisikia kuwa yako salama. Nilikuwa nimewakasirikia Israeli kidogo tu, lakini mataifa hayo yaliwazidishia maafa.’
16 Therefore thus says Jehovah: I have returned to Jerusalem with mercies. My house shall be built in it, says Jehovah of hosts, and a line shall be stretched forth over Jerusalem.
“Kwa hiyo, hivi ndivyo asemavyo Bwana: ‘Nitairudia Yerusalemu kwa rehema na huko nyumba yangu itajengwa tena. Nayo kamba ya kupimia itanyooshwa Yerusalemu,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
17 Cry yet again, saying, Thus says Jehovah of hosts: My cities shall yet overflow with prosperity, and Jehovah shall yet comfort Zion, and shall yet choose Jerusalem.
“Endelea kutangaza zaidi kwamba: Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Miji yangu itafurika tena ustawi na Bwana atamfariji tena Sayuni na kumchagua Yerusalemu.’”
18 And I lifted up my eyes, and saw, and, behold, four horns.
Kisha nikatazama juu, na pale mbele yangu nikaona pembe nne!
19 And I said to the agent who talked with me, What are these? And he answered me, These are the horns which have scattered Judah, Israel, and Jerusalem.
Nikamuuliza yule malaika aliyekuwa akizungumza nami, “Ni nini hivi?” Akanijibu, “Hizi ni zile pembe zilizowatawanya Yuda, Israeli na Yerusalemu.”
20 And Jehovah showed me four smiths.
Kisha Bwana akanionyesha mafundi wanne.
21 Then I said, What are these coming to do? And he spoke, saying, These are the horns which scattered Judah, so that no man lifted up his head. But these have come to terrify them, to cast down the horns of the nations, which lifted up their horn against the land of Judah to scatter it.
Nikauliza, “Hawa wanakuja kufanya nini?” Akanijibu, “Hizi ndizo pembe zilizowatawanya Yuda ili asiwepo atakayeweza kuinua kichwa chake, lakini mafundi wamekuja kuzitia hofu na kuzitupa chini hizi pembe za mataifa ambayo yaliinua pembe zao dhidi ya nchi ya Yuda na kuwatawanya watu wake.”

< Zechariah 1 >