< Psalms 81 >
1 Sing aloud to God our strength. Make a joyful noise to the God of Jacob.
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa gitithi. Zaburi ya Asafu. Mwimbieni kwa furaha, Mungu aliye nguvu yetu; mpigieni kelele za shangwe Mungu wa Yakobo!
2 Raise a song, and bring here the timbrel, the pleasant harp with the psaltery.
Anzeni wimbo, pigeni matari, pigeni kinubi na zeze kwa sauti nzuri.
3 Blow the trumpet at the new moon, at the full moon, on our feast-day.
Pigeni baragumu za pembe za kondoo dume wakati wa Mwandamo wa Mwezi, na wakati wa mwezi mpevu, katika siku ya Sikukuu yetu;
4 For it is a statute for Israel, an ordinance of the God of Jacob.
hii ni amri kwa Israeli, agizo la Mungu wa Yakobo.
5 He appointed it in Joseph for a testimony when he went out over the land of Egypt, where I heard a language that I knew not.
Aliiweka iwe kama sheria kwa Yosefu alipotoka dhidi ya Misri, huko tulikosikia lugha ambayo hatukuielewa.
6 I removed his shoulder from the burden. His hands were freed from the basket.
Asema, “Nimeondoa mzigo mabegani mwao; mikono yao iliwekwa huru kutoka kwenye kikapu.
7 Thou called in trouble, and I delivered thee. I answered thee in the secret place of thunder. I proved thee at the waters of Meribah. (Selah)
Katika shida yako uliniita nami nikakuokoa, nilikujibu katika mawingu yenye ngurumo; nilikujaribu katika maji ya Meriba.
8 Hear, O my people, and I will testify to thee, O Israel, if thou would hearken to me!
“Enyi watu wangu, sikieni, nami nitawaonya: laiti kama mngenisikiliza, ee Israeli!
9 There shall no strange god be in thee, nor shall thou worship any foreign god.
Hamtakuwa na mungu mgeni miongoni mwenu; msimsujudie mungu wa kigeni.
10 I am Jehovah thy God who brought thee up out of the land of Egypt. Open thy mouth wide, and I will fill it.
Mimi ni Bwana Mungu wako, niliyekutoa nchi ya Misri. Panua sana kinywa chako nami nitakijaza.
11 But my people hearkened not to my voice, and Israel would none of me.
“Lakini watu wangu hawakutaka kunisikiliza; Israeli hakutaka kunitii.
12 So I let them go after the stubbornness of their heart, that they might walk in their own counsels.
Basi niliwaacha katika ukaidi wa mioyo yao wafuate mashauri yao wenyewe.
13 O that my people would hearken to me, that Israel would walk in my ways!
“Laiti kama watu wangu wangalinisikiliza, kama Israeli wangalifuata njia zangu,
14 I would soon subdue their enemies, and turn my hand against their adversaries.
ningaliwatiisha adui zao kwa haraka, na kuugeuza mkono wangu dhidi ya watesi wao!
15 (The haters of Jehovah feign obedience to him, but their time is forever.)
Wale wanaomchukia Bwana wangalinyenyekea mbele zake, na adhabu yao ingedumu milele.
16 He would feed them also with the finest of the wheat. And I would satisfy thee with honey out of the rock.
Bali ninyi mngalilishwa ngano iliyo bora, na kuwatosheleza kwa asali itokayo kwenye mwamba.”