< Psalms 72 >
1 Give the king thy judgments, O God, and thy righteousness to the king's son.
Mpe mfalme amri ya haki yako, Mungu, haki yako kwa wana wa mfalme.
2 He will judge thy people with righteousness, and thy poor with justice.
Naye awaamue watu wako kwa haki na maskini wako kwa haki sawa.
3 The mountains shall bring peace to the people, and the hills, in righteousness.
Milima iwazalie watu amani; vilima navyo vizae haki.
4 He will judge the poor of the people. He will save the sons of the needy, and will break in pieces the oppressor.
Naye awahukumu watu maskini; awaokoe watoto wa wahitaji na kuwavunja vipande vipande wenye kuwatesa.
5 They shall fear thee while the sun endures, and as long as the moon, throughout all generations.
Na wakuheshimu wewe wakati wa jua, na kwa kipindi cha kudumu kwa mwezi katika vizazi vyote.
6 He will come down like rain upon the mown grass, as showers that water the earth.
Naye apate kuja kama mvua juu ya nyasi zilizokatwa, kama manyuyu yanyunyizayo nchi.
7 In his days righteousness shall flourish, and abundance of peace, till the moon is no more.
Mwenye haki na astawi kwa wakati wake, na amani iwepo kwa wingi mpaka mwezi utakapotoweka.
8 He shall also have dominion from sea to sea, and from the River to the ends of the earth.
Na awe na mamlaka toka bahari na bahari, na kutoka Mto hadi miisho ya dunia.
9 Those who dwell in the wilderness shall bow before him, and his enemies shall lick the dust.
Na wote waishio jangwani wainame mbele zake; adui zake na walambe mavumbi.
10 The kings of Tarshish and of the isles shall render tribute. The kings of Sheba and Seba shall offer gifts.
Wafalme wa Tashishi na visiwa walete kodi; wafalme wa Sheba na Seba watoe zawadi.
11 Yea, all kings shall fall down before him. All nations shall serve him.
Hakika wafalme wote wamwinamie yeye; mataifa yote yamtumikie yeye.
12 For he will deliver a needy man when he cries, and a poor man, who has no helper.
Kwa kuwa yeye humsaidia mhitaji na maskini asiye na msaidizi.
13 He will have pity on a poor and needy man, and he will save the souls of the needy.
Yeye huwahurumia maskini na wahitaji, na huokoa maisha ya wahitaji.
14 He will redeem their soul from oppression and violence. And their blood will be precious in his sight,
Huyaokoa maisha yao dhidi ya mateso na vurugu, na damu yao ni ya thamani machoni pake.
15 and they shall live. And to him shall be given of the gold of Sheba. And men shall pray for him continually. They shall bless him all the day long.
Naye apate kuishi! Na dhahabu za Sheba apewe yeye. Watu wamuombee yeye siku zote; Mungu ambariki daima.
16 There shall be abundance of grain in the earth upon the top of the mountains. The fruit of it shall shake like Lebanon. And they of the city shall flourish like grass of the earth.
Kuwepo na nafaka nyingi katika ardhi; juu ya milima kuwe na mawimbi ya mimea. Matunda yake yawe kama Lebanoni; watu wasitawi katika miji kama nyansi za kondeni.
17 His name shall endure forever. His name shall be continued as long as the sun. And men shall be blessed in him. All nations shall call him blessed.
Jina lake lidumu milele; jina lake ilindelee kama vile jua ling'aavyo; watu wabarikiwe katika yeye; mataifa yote wamwite mbarikiwa.
18 Blessed be Jehovah God, the God of Israel, who alone does wondrous things.
Yahwe Mungu, Mungu wa Israel, atukuzwe, ambaye pekee hufanya mambo ya ajabu.
19 And blessed be his glorious name forever. And let the whole earth be filled with his glory. Truly, and Truly.
Jina lake tukufu litukuzawe milele, nayo nchi yote ijazwe na utukufu wake. Amina, Amina.
20 The prayers of David the son of Jesse are ended.
Maombi ya Daudi mwana wa Yese yamemalizika. Kutatu cha tatu