< Psalms 64 >

1 Hear my voice, O God, in my complaint. Preserve my life from fear of the enemy.
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, unisikie ninapoeleza lalamiko langu, uyahifadhi maisha yangu kutokana na vitisho vya adui.
2 Hide me from the secret counsel of evildoers, from the tumult of the workers of iniquity,
Unifiche kutokana na shauri la siri la waovu, kutokana na zile kelele za kundi la watenda mabaya.
3 who have whet their tongue like a sword, and have aimed their arrows, even bitter words,
Wananoa ndimi zao kama panga na kuelekeza maneno yao kama mishale ya kufisha.
4 that they may shoot in secret places at a blameless man. Suddenly do they shoot at him, and fear not.
Hurusha mishale kutoka kwenye mavizio kwa mtu asiye na hatia, humrushia ghafula bila woga.
5 They encourage themselves in an evil purpose. They converse of laying snares secretly. They say, Who will see them?
Kila mmoja humtia moyo mwenzake katika mipango mibaya; huzungumza juu ya kuficha mitego yao, nao husema, “Ni nani ataiona?”
6 They search out iniquities, saying, We have accomplished a diligent search. And the inward part of man and the heart are deep.
Hufanya shauri baya la dhuluma na kusema, “Tumebuni mpango mkamilifu!” Hakika nia na moyo wa mwanadamu vina hila.
7 But God will shoot at them. With an arrow they shall suddenly be wounded.
Bali Mungu atawapiga kwa mishale, nao ghafula wataangushwa.
8 So they shall be made to stumble, their own tongue being against them. All who see them shall wag the head.
Atageuza ndimi zao wenyewe dhidi yao na kuwaleta kwenye maangamizi; wote wawaonao watatikisa vichwa vyao kwa dharau.
9 And all men shall fear. And they shall declare the work of God, and shall wisely consider of his doing.
Wanadamu wote wataogopa, watatangaza kazi za Mungu na kutafakari yale aliyoyatenda.
10 A righteous man shall be glad in Jehovah, and shall take refuge in him. And all the upright in heart shall glory.
Wenye haki na wafurahi katika Bwana, na wakimbilie kwake; wanyofu wote wa moyo na wamsifu yeye!

< Psalms 64 >