< Psalms 54 >
1 Save me, O God, by thy name, and judge me in thy might.
Kwa mwimbishaji. Na ala za nyuzi za uimbaji. Utenzi wa Daudi. Wakati Wazifu walimwendea Sauli na kumjulisha, “Je, Daudi hajifichi miongoni mwetu?” Ee Mungu uniokoe kwa jina lako, unifanyie hukumu kwa uwezo wako.
2 Hear my prayer, O God. Give ear to the words of my mouth.
Ee Mungu, sikia maombi yangu, usikilize maneno ya kinywa changu.
3 For strangers are risen up against me, and violent men have sought after my soul. They have not set God before them. (Selah)
Wageni wananishambulia, watu wakatili wanayatafuta maisha yangu, watu wasiomjali Mungu.
4 Behold, God is my helper. The Lord is of those who uphold my soul.
Hakika Mungu ni msaada wangu, Bwana ndiye anayenitegemeza.
5 He will requite the evil to my enemies. Destroy thou them in thy truth.
Mabaya na yawarudie wale wanaonisingizia, kwa uaminifu wako uwaangamize.
6 With a freewill offering I will sacrifice to thee. I will give thanks to thy name, O Jehovah, for it is good.
Nitakutolea dhabihu za hiari; Ee Bwana, nitalisifu jina lako kwa kuwa ni vyema.
7 For he has delivered me out of all trouble, and my eye has seen it upon my enemies.
Kwa maana ameniokoa katika shida zangu zote, na macho yangu yamewatazama adui zangu kwa ushindi.