< Psalms 42 >
1 As the hart pants after the water brooks, so my soul pants after thee, O God.
Kama ayala ayatamanivyo maji ya mto. ndivyo hivyo ninakiu yako, Mungu.
2 My soul thirsts for God, for the living God. When shall I come and appear before God?
Ninakiu yako Mungu, Mungu uliye hai, ni lini nitaonekana mbele zako?
3 My tears have been my food day and night, while they continually say to me, Where is thy God?
Machozi yangu yamekuwa ni chakula changu mchana na usiku, wakati maadui zangu siku zote wanasema, “Yuko wapi Mungu wako?”
4 These things I remember, and pour out my soul within me, how I went with the throng, and led them to the house of God, with the voice of joy and praise, a multitude keeping holyday.
Mambo haya niayakumbuka ninapoumimina roho yangu: nilipoenda na umati wa watu na kuwaongoza kwenye nyumba ya Mungu kwa sauti ya shangwe na kusifu, ni wengi tulisherekea.
5 Why are thou cast down, O my soul? And why are thou disquieted within me? Hope thou in God, for I shall yet praise him for the help of his countenance.
Roho yangu, kwa nini unainama? Kwa nini unahuzuni ndani yangu? Mtumaini Mungu, Kwa kuwa kwa mara nyingine nitamsifu yeye ambaye ni wokovu wangu.
6 O my God, my soul is cast down within me. Therefore I remember thee from the land of the Jordan, and the Hermons, from the hill Mizar.
Mungu wangu, roho yangu imeinama ndani yangu, kwa hiyo ninakukumbuka toka nchi ya Yordani, toka kwenye vilele vitatu vya mlima Hermoni, na toka mlima wa Mizari.
7 Deep calls to deep at the noise of thy waterfalls. All thy waves and thy billows have gone over me.
Kina huita kina kwenye kelele za maporomoko ya maji yako; mawimbi na mafuriko yako yote yako juu yangu.
8 Yet Jehovah will command his loving kindness in the daytime, and in the night his song shall be with me, even a prayer to the God of my life.
Wakati wa mchana Yahwe ataamuru uaminifu wa agano lake; na usiku wimbo wake utakuwa nami, ombi kwa Mungu wa uhai wangu.
9 I will say to God my rock, Why have thou forgotten me? Why do I go mourning because of the oppression of the enemy?
Nami nitasema kwa Mungu wangu, mwamba wangu, “Kwa nini umenisahau? Kwa nini ninaenenda katika maombolezo kwa sababu ya ukandamizaji wa adui yangu?”
10 As with a sword in my bones, my adversaries reproach me; while they continually say to me, Where is thy God?
Kama upanga mifupani pangu, maadui zangu wananikemea, siku zote wakiniambia, “Yuko wapi Mungu wako?”
11 Why are thou cast down, O my soul? And why are thou disquieted within me? Hope thou in God, for I shall yet praise him, the help of my countenance, and my God.
Roho yangu, kwa nini umeinama chini? Kwa nini unahuzuni ndani yangu? Mtumaini Mungu kwa kuwa nitamsifu tena yeye aliye wokovu wangu na Mungu wangu.