< Psalms 31 >

1 In thee, O Jehovah, do I take refuge. Let me never be put to shame. Deliver me in thy righteousness.
Kwa kiongozi wa muziki. Zaburi ya Daudi. In wewe, Yahwe, nakimbilia usalama; usiniache niaibishwe. Katika haki yako uniokoe.
2 Bow down thine ear to me. Deliver me speedily. Be thou to me a strong rock, a house of defense to save me.
Unisikie; uniokoe haraka; uwe mwamba wangu wa usalama, ngome ya kuniokoa.
3 For thou are my rock and my fortress. Therefore for thy name's sake lead me and guide me.
Kwa kuwa wewe ni mwamba wangu na ngome yangu; kwa hiyo kwa ajili ya jina lako, uniongoze na unielekeze.
4 Pluck me out of the net that they have laid secretly for me, for thou are my stronghold.
Unitoe katika mtego ambao wameuficha kwa ajili yangu, kwa kuwa wewe ni usalama wangu.
5 Into thy hand I commend my spirit. Thou have redeemed me, O Jehovah, thou God of truth.
Mikononi mwako naikabidhi roho yangu; nawe utaniokoa, Yahwe, mwenye kuaminika.
6 I hate those who regard lying vanities, but I trust in Jehovah.
Ninawachukia wale wanaotumikia miungu isiyo na maana, bali ninaamini katika Yahwe.
7 I will be glad and rejoice in thy loving kindness, for thou have seen my affliction. Thou have known my soul in adversities,
Nitafurahi na kushangilia katika uaminifu wa agano lako, kwa kuwa uliyaona mateso yangu; wewe uliijua dhiki ya moyo wangu.
8 and thou have not shut me up into the hand of the enemy. Thou have set my feet in a large place.
Wewe haujaniweka kwenye mkono wa maadui zangu. Nawe umeiweka miguu yangu mahali pa wazi papana.
9 Have mercy upon me, O Jehovah, for I am in distress. My eye wastes away with grief, yea, my soul and my body.
Uniurumie, Yahwe, kwa maana niko katika dhiki; macho yangu yanafifia kwa huzuni pamoja na moyo wangu na mwili wangu.
10 For my life is spent with sorrow, and my years with sighing. My strength fails because of my iniquity, and my bones are wasted away.
Kwa kuwa maisha yangu yamechoshwa kwa huzuni na miaka yangu kwa kuugua kwangu. Nimekuwa dhaifu kwa sababu ya dhambi zangu, na mifupa yangu inachakaa.
11 I have become a reproach because of all my adversaries, yea, to my neighbors exceedingly, and a fear to my acquaintances. Those who saw me outside fled from me.
Kwa sababu ya maadui zangu wote, watu wananibeza; majirani zangu wanaishangaa hali yangu, na wale wanao nifahamu wanashtuka. Wale wanionao mitaani hunikimbia.
12 I am forgotten as a dead man out of mind. I am like a broken vessel.
Nimesahaulika kama mtu aliye kufa ambaye hakuna mtu anaye mfikiria. Niko kama chungu kilicho pasuka.
13 For I have heard the slander of many. Fear was on every side, while they took counsel together against me. They devised to take away my life.
Kwa maana nimesikia minong'ono ya wengi, habari za kutisha kutoka pande zote kwa pamoja wamepanga njama kinyume na mimi. Wao wanapanga njama ya kuniua.
14 But I trusted in thee, O Jehovah. I said, Thou are my God.
Bali mimi ninakuamini wewe, Yahwe; Ninasema, “Wewe ni Mungu wangu.”
15 My times are in thy hand. Deliver me from the hand of my enemies, and from those who persecute me.
Hatima yangu iko mikononi mwako. Uniokoe mikononi mwa maadui zangu na wale wanao nifukuzia.
16 Make thy face to shine upon thy servant. Save me in thy loving kindness.
Nuru ya uso wako imuangazie mtumishi wako; uniokoe katika uaminifu wa agano lako.
17 Let me not be put to shame, O Jehovah, for I have called upon thee. Let the wicked be put to shame. Let them be silent in Sheol. (Sheol h7585)
Usiniache niaibishwe, Yahwe; kwa maana ninakuita wewe! Waovu waaibishwe! Na wanyamaze kimya kuzimuni. (Sheol h7585)
18 Let the lying lips be dumb, which speak against the righteous man insolently, with pride and contempt.
Na inyamazishwe midomo midanganyifu ambayo husema maneno mabaya kuhusu watu wenye haki huku wakiwa na kiburi na dharau.
19 O how great is thy goodness, which thou have laid up for those who fear thee, which thou have wrought for those who take refuge in thee before the sons of men!
Uzuri wako ni wa namna gani nao umeuhifadhii kwa ajili ya wale wanao kuheshimu sana, ambao wewe huufanya kwa ajili ya wale ambao hukimbilia kwako kwa ajili ya usalama mbele ya watoto wote wa wanadamu!
20 In the covert of thy presence thou will hide them from the plotting of man. Thou will keep them secretly in a pavilion from the strife of tongues.
Katika makao ya uwepo wako, wewe huwaficha mbali na njama za watu. Wewe huwaficha mahali salama na ndimi zenye vurugu.
21 Blessed be Jehovah, for he has shown me his marvelous loving kindness in a strong city.
Atukuzwe Yahwe, kwa maana yeye alinionesha maajabu ya uaminifu wa agano lake mahali nilipoishi.
22 As for me, I said in my haste, I am cut off from before thine eyes. Nevertheless thou heard the voice of my supplications when I cried to thee.
Ingawa kwa haraka zangu nilisema, “Nimeondolewa machoni pako,” bali wewe ulisikia kusihi kwangu nilipokulilia wewe.
23 O love Jehovah, all ye his sanctified. Jehovah preserves the faithful, and plentifully repays him who deals proudly.
Enyi wafuasi waaminifu, mpendeni Yahwe, Yahwe huwalinda waaminifu, lakini huwalipa wakaidi ipasavyo.
24 Be strong, and let your heart take courage, all ye who hope in Jehovah.
Iweni imara na jasiri, ninyi nyote mnao mwamini Mungu kuwasaidia.

< Psalms 31 >