< Psalms 130 >
1 Out of the depths I have cried to thee, O Jehovah.
Wimbo wa kwenda juu. Kutoka vilindini ninakulilia, Ee Bwana.
2 Lord, hear my voice. Let thine ears be attentive to the voice of my supplications.
Ee Bwana, sikia sauti yangu. Masikio yako na yawe masikivu kwa kilio changu unihurumie.
3 If thou, Jehovah, should note iniquities, O Lord, who could stand?
Kama wewe, Ee Bwana, ungeweka kumbukumbu ya dhambi, Ee Bwana, ni nani angeliweza kusimama?
4 But there is forgiveness with thee, that thou may be feared.
Lakini kwako kuna msamaha, kwa hiyo wewe unaogopwa.
5 I wait for Jehovah. My soul waits, and in his word do I hope,
Namngojea Bwana, nafsi yangu inangojea, katika neno lake naweka tumaini langu.
6 my soul for the Lord more than watchmen for the morning, watchmen for the morning.
Nafsi yangu inamngojea Bwana kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi, naam, kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi.
7 O Israel, hope in Jehovah, for with Jehovah there is loving kindness, and with him is plentiful redemption.
Ee Israeli, mtumaini Bwana, maana kwa Bwana kuna upendo usiokoma, na kwake kuna ukombozi kamili.
8 And he will redeem Israel from all his iniquities.
Yeye mwenyewe ataikomboa Israeli kutoka dhambi zao zote.