< Psalms 111 >

1 Praise ye Jehovah. I will give thanks to Jehovah with my whole heart, in the council of the upright, and in the congregation.
Msifuni Yahwe. Nitamshukuru Yahwe kwa moyo wangu wote katikati ya kusanyiko la wanye haki, na katika mkutano.
2 The works of Jehovah are great, sought out by all those who have pleasure in it.
Kazi za Yahwe ni kuu, zikisubiriwa na wale wazitamanio.
3 His work is honor and majesty, and his righteousness endures forever.
Kazi yake ni adhama na utukufu, na haki yake yadumu milele.
4 He has made his wonderful works to be remembered. Jehovah is gracious and merciful.
Hufanya mambo makuu ambayo yatakumbukwa; Yahwe ni mwenye huruma na neema.
5 He has given food to those who fear him. He will ever be mindful of his covenant.
Huwapa chakula wafuasi wake waaminifu. Siku zote atalikumbuka agano lake.
6 He has shown his people the power of his works, in giving them the heritage of the nations.
Alionesha uweza wa kazi zake kwa watu wake kwa kuwapa urithi wa mataifa.
7 The works of his hands are truth and justice. All his precepts are sure.
Kazi za mikono yake ni za kuaminika na haki; maagizo yake yote ni ya kuaminika.
8 They are established forever and ever. They are done in truth and uprightness.
Yamethibitika milele, yamefanywa katika uaminifu na vizuri.
9 He has sent redemption to his people. He has commanded his covenant forever. Holy and reverend is his name.
Aliwapa ushindi watu wake; aliliteuwa agano lake milele; jina lake ni takatifu na lakutisha.
10 The fear of Jehovah is the beginning of wisdom, and all who act accordingly have a good understanding. His praise endures forever.
Kumcha Yahwe ni mwanzo wa hekima; wale washikao maagizo yake wana uelewa mzuri. Sifa yake yadumu milele.

< Psalms 111 >