< Proverbs 25 >
1 These also are proverbs of Solomon, which the men of Hezekiah king of Judah copied out.
Hizi tena ni mithali za Sulemani, zilinakiliwa na watu wa Hezekia, mfalme wa Yuda.
2 It is the glory of God to conceal a thing, but the glory of kings is to search out a matter.
Ni utukufu wa Mungu kuficha jambo, bali utukufu wa wafalme kutafiti juu ya jambo.
3 As the heavens for height, and the earth for depth, so the heart of kings is unsearchable.
Kama mbingu ni kwa kimo na dunia ni kwa kina, ndivyo hivyo moyo wa wafalme hauchunguziki.
4 Take away the dross from the silver, and there comes forth a vessel for the refiner.
Ondoa takataka kutoka kwenye fedha na mfua vyuma anaweza kutumia fedha katika ufundi wake.
5 Take away the wicked from before the king, and his throne shall be established in righteousness.
Pamoja na hayo, waondoe watu waovu mbele ya mfalme na kiti chake cha enzi kitaimarishwa kwa kutenda haki.
6 Put not thyself forward in the presence of the king, and stand not in the place of great men.
Usijitukuze mwenyewe mbele ya mfalme na usisimame katika sehemu iliyoteuliwa kwa watu wakuu.
7 For it is better that it be said to thee, Come up here, than that thou should be put lower in the presence of the prince, whom thine eyes have seen.
Ni bora yeye akuambie, “Njoo hapa” kuliko wewe kujiaibisha mbele ya mkuu.
8 Go not forth hastily to strive. What will thou do in the end of it when thy neighbor has put thee to shame?
Usiharakishe kufanya kuhukumu, kwa kile ulichokishuhudia. Maana utafanya nini mwishoni, wakati jirani yako atakapokuaibisha?
9 Debate thy case with thy neighbor himself, and disclose not the secret of another,
Jitetee kesi yako kati ya jirani yako na wewe na usifunue siri ya mtu mwingine,
10 lest he who hears it revile thee, and thine infamy turn not away.
au vinginevyo anayekusikia ataleta aibu juu yako na taarifa mbaya juu yako haiwezi kunyamazishwa.
11 A word fitly spoken is apples of gold in a network of silver.
Kunena maneno yenye kuchaguliwa vizuri, ni kama nakshi za dhahabu iliyoungwa kwenye fedha.
12 An earring of gold, and an ornament of fine gold, is a wise reprover upon an obedient ear.
Kama pete ya dhahabu au kito kilichotengenezwa kwa dhahabu safi ndivyo lilivyo karipio la busara kwenye sikio linalosikia.
13 As the cold of snow in the time of harvest, is a faithful messenger to those who send him, for he refreshes the soul of his masters.
Kama baridi ya theluji wakati wa mavuno ndivyo alivyo mjumbe mwaminifu kwa wenye kumtuma; huyahifadhi maisha ya mabwana wake.
14 Clouds and wind without rain, is he who boasts himself of his gifts falsely.
Kama mawingu na upepo bila mvua ndivyo alivyo mwenye kujisifu kuhusu zawadi asiyoitoa.
15 By long-suffering a ruler is persuaded, and a soft tongue breaks the bone.
Kwa uvumilivu mtawala anaweza kushawishiwa na ulimi raini unaweza kuvunja mfupa.
16 Have thou found honey? Eat as much as is sufficient for thee, lest thou be filled with it, and vomit it.
Kama utapata asali, kula ya kutosha- vingenevyo, ukila nyingi sana, utaitapika.
17 Let thy foot be seldom in thy neighbor's house, lest he be weary of thee, and hate thee.
Usiweke mguu wako kwenye nyumba ya jirani yako mara nyingi, anaweza kuchoshwa nawe na kukuchukia.
18 A man who bears false witness against his neighbor is a maul, and a sword, and a sharp arrow.
Mtu anayetoa ushuhuda wa uongo dhidi ya jirani yake ni kama rungu lililotumiwa katika vita, au upanga, au mshale mkali.
19 Confidence in an unfaithful man in time of trouble is a broken tooth, and a foot out of joint.
Kumtumaini mtu asiye mwaminifu wakati wa taabu ni kama jino bovu au mguu unaoteleza.
20 As he who takes off a garment in cold weather, and vinegar upon soda, so is he who sings songs to a heavy heart.
Kama mtu anayevua nguo katika hali ya baridi, au kama siki iliyotiwa kwenye magadi, ndivyo alivyo anayeimba wimbo kwa mwenye moyo mzito.
21 If thine enemy is hungry, give him bread to eat, and if he is thirsty, give him water to drink.
Kama adui yako ana njaa, mpe chakula ale na kama ana kiu, mpe maji ya kunywa,
22 For thou will heap coals of fire upon his head, and Jehovah will reward thee.
maana utamwekea mkaa juu ya kichwa chake na Yehova atakupa thawabu.
23 The north wind brings forth rain. So does a backbiting tongue, an angry countenance.
Ni hakika upepo wa kaskazini huleta mvua, ndivyo mtu anayesema siri hufanya sura zikasirike.
24 It is better to dwell in the corner of the housetop, than with a contentious woman in a wide house.
Ni bora kuishi kwenye pembe ya darini kuliko kuchangia nyumba pamoja na mwanamke mgomvi.
25 As cold waters to a thirsty soul, so is good news from a far country.
Kama maji ya baridi kwa mwenye kiu, ndivyo ilivyo habari njema kutoka nchi ya mbali.
26 A troubled fountain, and a corrupted spring, is a righteous man who gives way before the wicked.
Kama chemchemi iliyochafuliwa au kisima kilichoharibiwa ndivyo alivyo mtu mwema ambaye huyumbayumba mbele ya watu waovu.
27 It is not good to eat much honey, so for men to search out their own glory is grievous.
Si vema kula asali nyingi mno; hivyo ni kama kutafuta heshima baada heshima.
28 He whose spirit is without restraint is a city that is broken down and without walls.
Mtu bila kujitawala ni kama mji ulibomolewa na usiokuwa na kuta.