< Philemon 1 >

1 Paul, a prisoner of Christ Jesus, and Timothy the brother, to Philemon our beloved and co-workman,
Mimi Paulo, mfungwa kwa ajili ya Kristo Yesu, na ndugu Timotheo, ninakuandikia wewe Filemoni mpendwa, mfanyakazi mwenzetu
2 and to the beloved Apphia, and Archippus our fellow soldier, and to the congregation at thy house:
na kanisa linalokutana nyumbani kwako, na wewe dada Afia, na askari mwenzetu Arkupo.
3 Grace to you and peace from God our Father and the Lord Jesus Christ.
Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu, na kwa Bwana yesu Kristo.
4 I thank my God, making recollection of thee always in my prayers,
Kila wakati ninaposali nakukumbuka wewe Filemoni, na kumshukuru Mungu
5 hearing of thy love and faith, which thou have toward the Lord Jesus and for all the sanctified,
maana nasikia habari za imani yako kwa Bwana wetu Yesu na upendo wako kwa watu wote wa Mungu.
6 so that the fellowship of thy faith may become potent (in the knowledge of every good thing in us) for Christ Jesus.
Naomba ili imani hiyo unayoshiriki pamoja nasi ikuwezeshe kuwa na ujuzi mkamilifu zaidi wa baraka zote tunazopata katika kuungana kwetu na Kristo.
7 For we have much joy and encouragement in thy love, because the bowels of the sanctified have been refreshed by thee, brother.
Ndugu, upendo wako yameniletea furaha kubwa na kunipa moyo sana! Nawe umeichangamsha mioyo ya watu wa Mungu.
8 Therefore, though I have much boldness in Christ to command thee that which is befitting,
Kwa sababu hiyo, ningeweza, kwa uhodari kabisa, nikiwa ndugu yako katika Kristo, kukuamuru ufanye unachopaswa kufanya.
9 because of love I rather beseech, being such as aged Paul, and now also a prisoner of Jesus Christ.
Lakini kwa sababu ya upendo, ni afadhali zaidi nikuombe. Nafanya hivi ingawa mimi ni Paulo, balozi wa Kristo Yesu, na sasa pia mfungwa kwa ajili yake.
10 I beseech thee for my child Onesimus, whom I begot in my bonds.
Basi, ninalo ombi moja kwako kuhusu mwanangu Onesimo, ambaye ni mwanangu katika Kristo kwani nimekuwa baba yake nikiwa kifungoni.
11 A man formerly unprofitable to thee, but now is profitable to thee and to me, whom I sent back.
Ni Onesimo yuleyule ambaye wakati mmoja alikuwa hakufai kitu, lakini sasa ananifaa mimi na wewe pia.
12 And thou should welcome him, that is, my bowels.
Sasa namrudisha kwako, naye ni kama moyo wangu mimi mwenyewe.
13 Whom I wanted to keep back for myself, so that in thy behalf he might serve me in the bonds of the good news.
Ningependa akae nami hapa anisaidie badala yako wakati niwapo kifungoni kwa sababu ya Habari Njema.
14 But I wanted to do nothing without thy mind, so that thy goodness might not be as from obligation, but from volition.
Lakini sitafanya chochote bila kibali chako. Sipendi kukulazimisha unisaidie, kwani wema wako unapaswa kutokana na hiari yako wewe mwenyewe na si kwa kulazimika.
15 For perhaps because of this he departed for an hour, so that thou might receive him back forever, (aiōnios g166)
Labda Onesimo aliondoka kwako kwa kitambo tu, kusudi uweze tena kuwa naye daima. (aiōnios g166)
16 no longer as a bondman, but above a bondman, a beloved brother, especially to me, but how much more to thee, both in flesh and in the Lord.
Na sasa yeye si mtumwa tu, ila ni bora zaidi ya mtumwa: yeye ni ndugu yetu mpenzi. Na wa maana sana kwangu mimi, na kwako atakuwa wa maana zaidi kama mtumwa na kama ndugu katika Bwana.
17 If then thou have me a partner, accept him as myself.
Basi, ikiwa wanitambua mimi kuwa mwenzako, mpokee tena kama vile ungenipokea mimi mwenyewe.
18 But if he has wronged thee, or owes anything, charge this to me.
Kama alikuwa amekukosea kitu, au alikuwa na deni lako, basi, unidai mimi.
19 I Paul write with my hand, I will repay, so that I may not say to thee that thou owe me in return even thyself.
Naandika jambo hili kwa mkono wangu mwenyewe: Mimi Paulo nitalipa! (Tena sina haja ya kusema kwamba wewe unalo deni kwangu la nafsi yako.)
20 Yes, brother, let me have a favor of thee in the Lord. Refresh my bowels in the Lord.
Haya, basi, ndugu yangu, nifanyie jambo hilo kwa ajili ya jina la Bwana; burudisha moyo wangu kama ndugu katika Kristo.
21 Being confident in thine obedience I wrote to thee, knowing that thou will do above what I say.
Naandika nikitumaini kwamba utanikubalia ombi langu; tena najua kwamba utafanya hata zaidi ya haya ninayokuomba.
22 But simultaneously also prepare a lodging for me, for I hope that by your prayers I will be granted to you.
Pamoja na hayo, nitayarishie chumba kwani natumaini kwamba kwa sala zenu, Mungu atanijalia niwatembeleeni.
23 Epaphras, my fellow prisoner in Christ Jesus, salutes thee,
Epafra, mfungwa mwenzangu kwa ajili ya Kristo Yesu, anakusalimu.
24 and Mark, Aristarchus, Demas, Luke, my co-workmen.
Nao akina Marko, Aristarko, Dema na Luka, wafanyakazi wenzangu, wanakusalimu.
25 The grace of our Lord Jesus Christ is with your spirit. Truly.
Nawatakieni ninyi nyote neema ya Bwana wetu Yesu Kristo.

< Philemon 1 >