< Numbers 17 >

1 And Jehovah spoke to Moses, saying,
Bwana akamwambia Mose,
2 Speak to the sons of Israel, and take rods from them, one for each father's house, from all their rulers according to their fathers' houses, twelve rods. Write thou every man's name upon his rod.
“Sema na Waisraeli, na ujipatie fimbo kumi na mbili kutoka kwao, moja kutoka kwa kila mmoja wa viongozi wa kabila za baba zao. Andika jina la kila mtu kwenye fimbo yake.
3 And thou shall write Aaron's name upon the rod of Levi, for there shall be one rod for each head of their fathers' houses.
Kwenye fimbo ya Lawi andika jina la Aroni, kwa maana ni lazima iwepo fimbo moja kwa kila kiongozi kwa ajili ya kila kabila la baba zao.
4 And thou shall lay them up in the tent of meeting before the testimony, where I meet with you.
Ziweke hizo fimbo ndani ya Hema la Kukutania mbele ya Sanduku la Ushuhuda, mahali nikutanapo nawe.
5 And it shall come to pass, that the rod of the man whom I shall choose shall bud. And I will make to cease from me the murmurings of the sons of Israel, which they murmur against you.
Fimbo ya mtu nitakayemchagua itachipuka, nami mwenyewe nitayakomesha haya manungʼuniko ya mara kwa mara ya Waisraeli dhidi yako.”
6 And Moses spoke to the sons of Israel. And all their rulers gave him rods, for each ruler one, according to their fathers' houses, even twelve rods, and the rod of Aaron was among their rods.
Hivyo Mose akasema na Waisraeli, nao viongozi wao wakampa fimbo kumi na mbili, fimbo moja kwa ajili ya kila kabila la baba zao, nayo fimbo ya Aroni ikiwa miongoni mwa hizo.
7 And Moses laid up the rods before Jehovah in the tent of the testimony.
Mose akaziweka hizo fimbo mbele za Bwana ndani ya Hema la Ushuhuda.
8 And it came to pass on the morrow, that Moses went into the tent of the testimony, and, behold, the rod of Aaron for the house of Levi was budded, and put forth buds, and produced blossoms, and bore ripe almonds.
Siku iliyofuata Mose aliingia kwenye Hema la Ushuhuda akaona ile fimbo ya Aroni ambayo iliwakilisha jamaa ya Lawi haikuwa tu imechipuka, bali pia ilikuwa imetoa machipukizi, kuchanua maua na kuzaa malozi.
9 And Moses brought out all the rods from before Jehovah to all the sons of Israel. And they looked, and took every man his rod.
Ndipo Mose akaleta zile fimbo zote kwa Waisraeli wote kutoka mbele za Bwana. Wakaziangalia, na kila mtu akaichukua fimbo yake mwenyewe.
10 And Jehovah said to Moses, Put back the rod of Aaron before the testimony, to be kept for a sign against the sons of rebellion, that thou may make an end of their murmurings against me, that they not die.
Bwana akamwambia Mose, “Rudisha fimbo ya Aroni mbele ya Sanduku la Ushuhuda, ili ihifadhiwe kama alama kwa waasi. Hili litakomesha manungʼuniko yao dhidi yangu, ili kwamba wasife.”
11 Thus Moses did. As Jehovah commanded him, so he did.
Mose akafanya kama Bwana alivyomwamuru.
12 And the sons of Israel spoke to Moses, saying, Behold, we perish, we are undone, we are all undone.
Waisraeli wakamwambia Mose, “Tutakufa! Tumepotea, sote tumepotea!
13 Every man who comes near, who comes near to the tabernacle of Jehovah, dies. Shall we all of us perish?
Yeyote akaribiaye Maskani ya Bwana atakufa. Je, sisi sote tutakufa?”

< Numbers 17 >