< Matthew 23 >

1 Then Jesus spoke to the multitudes and to his disciples, saying,
Kisha Yesu akauambia umati wa watu pamoja na wanafunzi wake,
2 The scholars and the Pharisees sit on Moses' seat.
“Walimu wa Sheria na Mafarisayo wana mamlaka ya kufafanua Sheria ya Mose.
3 All things therefore, however many they may tell you to observe, observe and do, but do not ye according to their works, for they say, and do not.
Kwa hiyo shikeni na kutekeleza chochote watakachowaambieni. Lakini msiyaige matendo yao, maana hawatekelezi yale wanayoyahubiri.
4 For they bind heavy burdens and difficult to bear, and lay them on men's shoulders, but they do not want to move them with their finger.
Hufunga mizigo mizito na kuwatwika watu mabegani, lakini wao wenyewe hawataki kunyosha hata kidole wapate kuibeba.
5 But all their works they do in order to be seen by men. And they make broad their phylacteries, and enlarge the hems of their garments.
Wao hufanya matendo yao yote ili watu wawaone. Huvaa tepe zenye maandishi ya Sheria juu ya panda la uso na mikononi na hupanua pindo za makoti yao.
6 And they love the chief place at feasts, and the chief seats in the synagogues,
Hupenda nafasi za heshima katika karamu na viti vya heshima katika masunagogi.
7 and the greetings in the marketplaces, and to be designated by men, Rabbi, Rabbi.
Hupenda kusalimiwa kwa heshima sokoni na kupendelea kuitwa na watu: Mwalimu.
8 But be ye not designated Rabbi, for one is your leader, the Christ, and ye are all brothers.
Lakini ninyi msiitwe kamwe Mwalimu, maana mwalimu wenu ni mmoja tu, nanyi nyote ni ndugu.
9 And do not designate a father of you upon the earth, for one is your Father, he in the heavens.
Wala msimwite mtu yeyote Baba hapa duniani, maana Baba yenu ni mmoja tu aliye mbinguni.
10 And be ye not designated leaders, for one is your leader, the Christ.
Wala msiitwe Viongozi, maana kiongozi wenu ni mmoja tu, ndiye Kristo.
11 But the greater of you will be your helper.
Aliye mkubwa miongoni mwenu ni lazima awe mtumishi wenu.
12 And he who will exalt himself will be made low, and he who will make himself low will be exalted.
Anayejikweza atashushwa, na anayejishusha atakwezwa.
13 Woe to you, scholars and Pharisees, hypocrites! Because ye close up the kingdom of the heavens ahead of men. For ye enter not in, nor do ye allow those who are entering to enter in.
“Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnaufunga mlango wa Ufalme wa mbinguni mbele ya macho ya watu. Ninyi wenyewe hamwingii ndani, wala hamwaruhusu wanaotaka kuingia waingie.
14 But woe to you, scholars and Pharisees, hypocrites! Because ye devour widows' houses, and praying long in pretence. Because of this ye will receive greater condemnation.
Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnawanyonya wajane na kujisingizia kuwa watu wema kwa kusali sala ndefu. Kwa sababu hiyo mtapata adhabu kali.
15 Woe to you, scholars and Pharisees, hypocrites! Because ye encompass the sea and the land to make one proselyte, and when it happens, ye make him twice more a son of hell than yourselves. (Geenna g1067)
“Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnasafiri baharini na nchi kavu ili kumpata mtu mmoja afuate dini yenu. Mnapompata, mnamfanya astahili maradufu kwenda katika moto wa Jehanamu kuliko ninyi wenyewe. (Geenna g1067)
16 Woe to you, ye blind guides, who say, Whoever may swear by the temple, it is nothing, but whoever may swear by the gold of the temple, he is obligated.
“Ole wenu viongozi vipofu! Ninyi mwasema ati mtu akiapa kwa Hekalu, kiapo hicho si kitu; lakini akiapa kwa dhahabu ya Hekalu, kiapo hicho kinamshika.
17 Ye foolish and blind men, for which is greater, the gold, or the temple that makes the gold sacred?
Enyi vipofu wapumbavu! Kipi kilicho cha maana zaidi: dhahabu au Hekalu linalofanya hiyo dhahabu kuwa takatifu?
18 And, Whoever may swear by the altar, it is nothing, but whoever may swear by the gift upon it, he is obligated.
Tena mwasema ati mtu akiapa kwa madhabahu si kitu; lakini akiapa kwa zawadi iliyowekwa juu ya madhabahu, kiapo hicho humshika.
19 Ye foolish and blind men, for which is greater, the gift, or the altar that makes the gift sacred?
Enyi vipofu! Ni kipi kilicho cha maana zaidi: ile zawadi, au madhabahu ambayo hufanya hiyo zawadi kuwa takatifu?
20 He therefore who swears by the altar, swears by it, and by all things on it.
Anayeapa kwa madhabahu ameapa kwa hiyo madhabahu, na kwa chochote kilichowekwa juu yake.
21 And he who swears by the temple, swears by it, and by him who dwells in it.
Na anayeapa kwa Hekalu ameapa kwa hilo Hekalu na pia kwa yule akaaye ndani yake.
22 And he who swears by heaven, swears by the throne of God, and by him who sits upon it.
Na anayeapa kwa mbingu ameapa kwa kiti cha enzi cha Mungu, na kwa huyo aketiye juu yake.
23 Woe to you, scholars and Pharisees, hypocrites! Because ye tithe the mint and the anise and the cummin, and have omitted the weightier matters of the law-justice and mercy and faith. These things must be done, and not neglecting those things.
Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnatoza watu zaka, hata juu ya majani yenye harufu nzuri, bizari na jira, na huku mnaacha mambo muhimu ya Sheria kama vile haki, huruma na imani. Haya ndiyo hasa mliyopaswa kuyazingatia bila kusahau yale mengine.
24 Ye blind guides, who strain out the gnat, and swallow the camel.
Viongozi vipofu! Mnatoa nzi katika kinywaji, lakini mnameza ngamia!
25 Woe to you, scholars and Pharisees, hypocrites! Because ye cleanse the outside of the cup and of the platter, but inside they are full of plunder and unrighteousness.
“Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnasafisha kikombe na bakuli kwa nje, lakini ndani mnaacha kumejaa vitu mlivyopata kwa unyang'anyi na uchoyo.
26 Thou blind Pharisee, cleanse first the inside of the cup and of the platter, so that the outside of them may also become clean.
Mfarisayo kipofu! Kisafishe kikombe ndani kwanza na nje kutakuwa safi pia.
27 Woe to you, scholars and Pharisees, hypocrites! Because ye are like whitewashed tombs, which indeed appear beautiful outwardly, but inside are full of dead men's bones, and of all uncleanness.
“Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mko kama makaburi yaliyopakwa chokaa ambayo kwa nje yanaonekana kuwa mazuri, lakini ndani yamejaa mifupa ya maiti na kila namna ya uchafu.
28 In this way also, ye indeed outwardly appear righteous to men, but inside ye are full of hypocrisy and lawlessness.
Hali kadhalika ninyi mnaonekana na watu kwa nje kuwa wema, lakini kwa ndani mmejaa unafiki na uovu.
29 Woe to you, scholars and Pharisees, hypocrites! Because ye build the tombs of the prophets, and adorn the sepulchers of the righteous,
“Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnajenga makaburi ya manabii na kuyapamba makaburi ya watu wema.
30 and say, If we had been in the days of our fathers, we would not have been partakers with them in the blood of the prophets.
Mwasema: Kama sisi tungaliishi nyakati za wazee wetu hatungalishirikiana nao katika mauaji ya manabii!
31 So then ye testify to yourselves that ye are sons of those who murdered the prophets.
Hivyo mnathibitisha ninyi wenyewe kwamba ninyi ni watoto wa watu waliowaua manabii.
32 Then fill ye up the measure of your fathers.
Haya, kamilisheni ile kazi wazee wenu waliyoianza!
33 Ye serpents, ye offspring of vipers, how will ye escape from the damnation of hell? (Geenna g1067)
Enyi kizazi cha nyoka wenye sumu! Mnawezaje kuiepa hukumu ya moto wa Jehanamu? (Geenna g1067)
34 Because of this, behold, I send to you prophets, and wise men, and scholars. And some of them ye will kill and crucify, and some of them ye will scourge in your synagogues, and will persecute from city to city,
Ndiyo maana mimi ninawapelekea ninyi manabii, watu wenye hekima na walimu; mtawaua na kuwasulubisha baadhi yao, na wengine mtawapiga viboko katika masunagogi yenu na kuwasaka katika kila mji.
35 so that upon you may come all the righteous blood shed on the earth, from the blood of righteous Abel to the blood of Zachariah son of Barachiah, whom ye murdered between the sanctuary and the altar.
Hivyo lawama yote itawapateni kwa ajili ya damu yote ya watu wema iliyomwagwa juu ya ardhi. Naam, tangu kuuawa kwa Abeli ambaye hakuwa na hatia, mpaka kuuawa kwa Zakariya, mwana wa Barakia, ambaye mlimuua Hekaluni kati ya patakatifu na madhabahu.
36 Truly I say to you, that all these things will come upon this generation.
Nawaambieni kweli, kizazi hiki kitapata adhabu kwa sababu ya mambo haya.
37 O Jerusalem, Jerusalem, who kills the prophets, and stones those who have been sent to her. How often I wanted to gathered thy children together the way a hen gathers her chicks under her wings, and ye would not.
“Yerusalemu, Ee Yerusalemu! Unawaua manabii na kuwapiga mawe wale waliotumwa kwako. Mara ngapi nimejaribu kuwakusanya watoto wako kwangu, kama vile kuku anavyokusanya vifaranga vyake chini ya mabawa yake, lakini hukutaka.
38 Behold, your house is left to you desolate.
Haya basi, nyumba yako itaachwa mahame.
39 For I say to you, ye will, no, not see me henceforth, until ye say, Blessed is he who comes in the name of the Lord.
Nakwambia kweli, hutaniona tena mpaka wakati utakaposema: Abarikiwe huyo ajaye kwa jina la Bwana.”

< Matthew 23 >