< Matthew 2 >

1 Now Jesus having been born in Bethlehem of Judea in the days of Herod the king, behold, wise men from the east came to Jerusalem, saying,
Yesu alizaliwa mjini Bethlehemu, mkoani Yudea, wakati Herode alipokuwa mfalme. Punde tu baada ya kuzaliwa kwake, wataalamu wa nyota kutoka mashariki walifika Yerusalemu,
2 Where is he who is born king of the Jews? For we saw his star in the east, and have come to worship him.
wakauliza, “Yuko wapi mtoto, Mfalme wa Wayahudi, aliyezaliwa? Tumeiona nyota yake ilipotokea mashariki, tukaja kumwabudu.”
3 And Herod the king having heard it, he was troubled, and all Jerusalem with him.
Mfalme Herode aliposikia hayo, alifadhaika, yeye pamoja na wakazi wote wa Yerusalemu.
4 And having gathered together all the chief priests and scholars of the people, he inquired of them where the Christ is born.
Basi akawaita pamoja makuhani wakuu wote na walimu wa Sheria, akawauliza, “Kristo atazaliwa wapi?”
5 And they said to him, In Bethlehem of Judea. For thus it is written through the prophet,
Nao wakamjibu, “Mjini Bethlehemu, mkoani Yudea. Ndivyo nabii alivyoandika:
6 And thou Bethlehem, land of Judah, are in no way least among the rulers of Judah, for out of thee will come forth a man who rules, who will tend my people Israel.
Ewe Bethlehemu katika nchi ya Yuda, kwa vyovyote wewe si mdogo kabisa kati ya viongozi wa Yuda; maana kwako atatokea kiongozi atakayewaongoza watu wangu, Israeli.”
7 Then Herod having called the wise men privately, ascertained from them what time the star appeared.
Hapo, Herode aliwaita faraghani hao wataalamu wa nyota, akawauliza wakati hasa ile nyota ilipowatokea.
8 And having sent them to Bethlehem, he said, After going, search diligently about the child. And when ye find him, report to me, so that I also having come, may worship him.
Kisha akawatuma Bethlehemu akisema, “Nendeni mkachunguze kwa makini habari za mtoto huyo. Mkisha mpata nileteeni habari ili nami niende nikamwabudu.”
9 And when they heard the king, they departed. And lo, the star that they saw in the east went before them until, having come, it stood over where the child was.
Baada ya kumsikiliza mfalme, hao wataalamu wa nyota wakaenda. Kumbe ile nyota waliyokuwa wameiona upande wa mashariki iliwatangulia hata ikaenda kusimama juu ya mahali pale alipokuwa mtoto.
10 And when they saw the star, they rejoiced with exceedingly great joy.
Walipoiona hiyo nyota, walifurahi mno.
11 And having come into the house, they saw the child with Mary his mother, and having fallen down, they worshiped him. And having opened their treasures, they brought to him gifts, gold and frankincense and myrrh.
Basi, wakaingia nyumbani, wakamwona yule mtoto pamoja na Maria mama yake; wakapiga magoti, wakamsujudia. Kisha wakafungua hazina zao, wakampa zawadi: dhahabu, ubani na manemane.
12 And divinely warned in a dream not to return to Herod, they departed into their own country by another way.
Mungu aliwaonya katika ndoto wasimrudie Herode; hivyo wakarudi makwao kwa njia nyingine.
13 Now after they departed, behold, an agent of the Lord appears to Joseph in a dream, saying, After rising, take the child and his mother, and flee into Egypt, and thou be there until I tell thee, for Herod is going to seek the child to destroy it.
Baada ya wale wageni kuondoka, malaika wa Bwana alimtokea Yosefu katika ndoto, akamwambia, “Amka! Mchukue mtoto pamoja na mama yake, mkimbilie Misri. Kaeni huko mpaka nitakapokwambia, maana Herode anakusudia kumwua huyu mtoto.”
14 And having awakened, he took the child and his mother by night, and departed into Egypt.
Hivyo, Yosefu aliamka, akamchukua mtoto pamoja na mama yake, akaondoka usiku, akaenda Misri.
15 And he was there until the end of Herod, so that what was spoken by the Lord through the prophet might be fulfilled, which says, Out of Egypt I called my Son.
Akakaa huko mpaka Herode alipokufa. Jambo hilo lilifanyika ili neno alilosema Bwana kwa njia ya nabii litimie: “Nilimwita Mwanangu kutoka Misri.”
16 Then Herod, when he saw that he was scorned by the wise men, was exceedingly angry, and having sent forth, he killed all the boys in Bethlehem, and in all the borders of it, from two years old and under, according to the time that he had ascertained from the wise men.
Herode alipogundua kwamba wale wataalamu wa nyota walikuwa wamemhadaa, alikasirika sana. Akaamuru watoto wote wa kiume mjini Bethlehemu na kandokando yake wenye umri wa miaka miwili na chini yake wauawe. Alifanya hivyo kufuatana na muda aliopata kujua kutoka kwa wale wataalamu wa nyota.
17 Then that which was spoken through Jeremiah the prophet was fulfilled, which says,
Ndivyo yalivyotimia maneno yaliyosemwa kwa njia ya nabii Yeremia:
18 A voice was heard in Ramah, lamentation, and weeping, and great mourning, Rachel weeping for her children. And she did not want to be comforted, because they are not.
“Sauti imesikika mjini Rama, kilio na maombolezo mengi. Raheli anawalilia watoto wake, wala hataki kutulizwa, maana wote wamefariki.”
19 But when Herod perished, behold, an agent of the Lord appears in a dream to Joseph in Egypt, saying,
Baada ya kifo cha Herode, malaika wa Bwana alimtokea Yosefu katika ndoto kule Misri,
20 After rising, take the child and his mother, and go into the land of Israel, for those seeking the child's life have died.
akamwambia, “Amka! Mchukue mtoto pamoja na mama yake, urudi tena katika nchi ya Israeli, maana wale waliotaka kumwua mtoto huyo wamekwisha kufa.”
21 And having awaken, he took the child and his mother, and came into the land of Israel.
Basi, Yosefu aliamka, akamchukua mtoto pamoja na mama yake, akarejea katika nchi ya Israeli.
22 But when he heard that Archelaus was reigning over Judea in place of his father Herod, he was afraid to go there. And divinely warned in a dream, he withdrew into the parts of Galilee.
Lakini Yosefu aliposikia kwamba Arkelao mwanawe Herode alikuwa mfalme wa Yudea mahali pa baba yake, aliogopa kwenda huko. Naye baada ya kuonywa katika ndoto, alikwenda katika mkoa wa Galilaya,
23 And having come, he dwelt in a city called Nazareth, so that what was spoken through the prophets might be fulfilled, that he will be called a Nazarene.
akahamia katika mji uitwao Nazareti. Ndivyo yalivyotimia maneno yaliyonenwa kwa njia ya manabii: “Ataitwa Mnazare.”

< Matthew 2 >