< Luke 20 >
1 And it came to pass on one of those days, as he was teaching the people in the temple, and preaching the good news, the chief priests and the scholars with the elders stood near.
Siku moja, Yesu alipokuwa akiwafundisha watu Hekaluni na kuwahubiria juu ya Habari Njema, makuhani wakuu na walimu wa Sheria pamoja na wazee walifika,
2 And they spoke, saying to him, Tell us, by what authority are thou doing these things? Or who is he who gave thee this authority?
wakasema, “Tuambie! Unafanya mambo haya kwa mamlaka gani?”
3 And having answered, he said to them, I also will ask you one word, and ye tell me.
Yesu akawaambia, “Na mimi nitawaulizeni swali:
4 The immersion of John, was it from heaven or from men?
mamlaka ya Yohane ya kubatiza yalitoka kwa Mungu au kwa watu?”
5 And they reasoned with themselves, saying, If we should say, From heaven, he will say, Why did ye not believe him?
Lakini wao wakajadiliana hivi: “Tukisema yalitoka mbinguni, yeye atatuuliza: Mbona hamkumsadiki?
6 But if we say, From men, all the people will stone us, for they are convinced John is a prophet.
Na tukisema yalitoka kwa binadamu, watu wote hapa watatupiga mawe, maana wote wanaamini kwamba Yohane alikuwa nabii.”
7 And they replied not to know from where.
Basi, wakamwambia, “Hatujui mamlaka hayo yalitoka wapi.”
8 And Jesus said to them, Neither do I tell you by what authority I do these things.
Yesu akawaambia, “Hata mimi sitawaambia ninafanya mambo haya kwa mamlaka gani.”
9 And he began to speak this parable to the people. A man planted a vineyard, and leased it to farmers, and went abroad for a considerable time.
Yesu akaendelea kuwaambia watu mfano huu: “Mtu mmoja alilima shamba la mizabibu, akalikodisha kwa wakulima; kisha akasafiri hadi nchi ya mbali, akakaa huko kwa muda mrefu.
10 And at the season he sent a bondman to the farmers, so that they would give him from the fruit of the vineyard. But having beaten him, the farmers sent him away empty.
Wakati wa mavuno, mtu huyo alimtuma mtumishi wake kwa wale wakulima, akachukue sehemu ya matunda ya shamba la mizabibu. Lakini wale wakulima wakampiga mtumishi huyo wakamrudisha mikono mitupu.
11 And he proceeded to send another bondman. And they, having beaten and shamefully treated, sent him also away empty.
Yule bwana akamtuma tena mtumishi mwingine; lakini wao wakampiga huyo vilevile na kumtendea vibaya, wakamrudisha mikono mitupu.
12 And he proceeded to send a third. And they also having wounded this man, cast him out.
Akamtuma tena wa tatu; huyu naye, baada ya kumwumiza, wakamfukuza.
13 And the lord of the vineyard said, What shall I do? I will send my beloved son. Perhaps they will be made ashamed after seeing this man.
Yule mwenye shamba akafikiri: Nitafanya nini? Nitamtuma mwanangu mpenzi; labda watamjali yeye.
14 But when the farmers saw him, they deliberated among themselves, saying, This is the heir. Come, let us kill him, so that the inheritance may become ours.
Wale wakulima walipomwona tu, wakasemezana: Huyu ndiye mrithi. Basi, tumwue ili urithi wake uwe wetu.
15 And having cast him outside of the vineyard, they killed him. What therefore will the lord of the vineyard do to them?
Basi, wakamtoa nje ya lile shamba la mizabibu, wakamwua.” Yesu akauliza, “Yule mwenye shamba atawafanya nini hao wakulima?
16 He will come and destroy these farmers, and will give the vineyard to others. And having heard it, they said, May it not happen!
Atakuja kuwaangamiza wakulima hao, na atawapa wakulima wengine hilo shamba la mizabibu.” Watu waliposikia maneno hayo, walisema: “Hasha! Yasitukie hata kidogo!”
17 But having looked upon them, he said, What then is this that is written, The stone that those who build rejected, this became the head of the corner?
Lakini Yesu akawatazama, akawaambia, “Maandiko haya Matakatifu yana maana gani basi? Jiwe walilokataa waashi, sasa limekuwa jiwe kuu la msingi!
18 Every man who falls on that stone will be broken, but on whomever it may fall, it will grind him to dust.
Mtu yeyote akianguka juu ya jiwe hilo, atavunjika vipandevipande; na likimwangukia mtu yeyote, litamsaga kabisa.”
19 And the chief priests and the scholars sought to throw hands on him in the same hour. And they were afraid, for they knew that he spoke this parable against them.
Walimu wa Sheria na makuhani wakuu walifahamu kwamba mfano huo ulikuwa unawahusu, na hivyo walitaka kumkamata palepale, ila tu waliogopa watu.
20 And having watched him, they sent forth insidious men pretending themselves to be righteous, so that they might take hold of his word, in order to deliver him up to the rule and to the authority of the governor.
Basi, wakawa wanatafuta wakati wa kufaa. Wakawahonga watu fulani wajisingizie kuwa wema, wakawatuma wamnase Yesu kwa maswali, na hivyo waweze kumtia nguvuni na kumpeleka kwa wakuu wa serikali.
21 And they questioned him, saying, Teacher, we know that thou speak and teach rightly, and thou do not accept a personage, but teach the way of God in truth,
Hao wapelelezi wakamwambia, “Mwalimu, tunajua kwamba unasema na kufundisha mambo ya kweli; tunajua kwamba wewe huna ubaguzi; wewe wafundisha ukweli juu ya njia ya Mungu.
22 Is it permitted for us to give tribute to Caesar or not?
Basi, twambie kama ni halali, au la, kulipa kodi kwa Kaisari!”
23 But having perceived their craftiness, he said to them, Why do ye try me?
Yesu alitambua mtego wao, akawaambia,
24 Display to me a denarius. Whose image and inscription has it? And having answered, they said, Caesar's.
“Nionyesheni sarafu. Je, sura na chapa ni vya nani?”
25 And he said to them, Then render the things of Caesar to Caesar, and the things of God to God.
Nao wakamjibu, “Ni vya Kaisari.” Yesu akawaambia, “Basi, mpeni Kaisari vilivyo vyake Kaisari, na Mungu vilivyo vyake Mungu.”
26 And they were unable to lay hold of his word before the people. And having marveled at his answer, they were silent.
Hawakufaulu kumnasa kwa neno lolote pale mbele ya watu na hivyo wakakaa kimya wakilistaajabia jibu lake.
27 And some of the Sadducees having approached, those who say there is no resurrection, they questioned him,
Kisha Masadukayo, ambao husema kwamba wafu hawafufuki, wakamjia Yesu, wakasema:
28 saying, Teacher, Moses wrote to us, if any brother dies, having a wife, and this man dies childless, that his brother should take his wife, and raise up seed to his brother.
“Mwalimu, Mose alituandikia kwamba kama ndugu ya mtu fulani akifa na kumwacha mjane wake bila watoto, ni lazima ndugu yake amchukue huyo mama mjane, amzalie watoto ndugu yake marehemu.
29 There were therefore seven brothers. And the first having taken a wife, died childless.
Sasa, wakati mmoja kulikuwa na ndugu saba. Yule wa kwanza alioa na baadaye akafa bila kuacha mtoto.
30 And the second took the woman, and this man died childless.
Yule ndugu wa pili akamwoa yule mjane, naye pia, akafa;
31 And the third likewise took her, and likewise also the seven; they left behind no children, and died.
na ndugu wa tatu vilevile. Mambo yakawa yaleyale kwa wote saba—wote walikufa bila kuacha watoto.
32 And last of all the woman also died.
Mwishowe akafa pia yule mwanamke.
33 In the resurrection therefore whose wife of them does she become? For the seven had her as wife.
Je, siku wafu watakapofufuliwa, mwanamke huyo atakuwa mke wa nani? Alikuwa ameolewa na wote saba.”
34 And having answered, Jesus said to them, The sons of this age marry, and are given in marriage, (aiōn )
Yesu akawaambia, “Watu wa nyakati hizi huoa na kuolewa; (aiōn )
35 but those who are considered worthy to attain to that age, and the resurrection from the dead, neither marry, nor are given in marriage. (aiōn )
lakini wale ambao Mungu atawawezesha kushiriki ule wakati wa ufufuo, hawataoa wala kuolewa. (aiōn )
36 For neither can they die any more, for they are like the agents, and are sons of God, being sons of the resurrection.
Ama hakika, hawawezi kufa tena, kwa sababu watakuwa kama malaika, na ni watoto wa Mungu kwa vile wamefufuliwa katika wafu.
37 But that the dead are raised, even Moses showed at the Bush when he calls the Lord, the God of Abraham, and the God of Isaac, and the God of Jacob.
Lakini, kwamba kuna kufufuka kutoka wafu, hata Mose alithibitisha jambo hilo katika Maandiko Matakatifu. Katika sehemu ya Maandiko Matakatifu juu ya kile kichaka kilichokuwa kinawaka moto, anamtaja Bwana kama Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo.
38 Now he is not God of the dead, but of the living, for all live to him.
Basi, yeye si Mungu wa wafu, bali ni Mungu wa wale walio hai; maana wale aliowaita kwake, wanaishi naye.”
39 And some of the scholars having answered, they said, Teacher, thou said well.
Baadhi ya wale walimu wa Sheria wakasema, “Mwalimu, umejibu vema kabisa.”
40 For they no longer dared to question him anything.
Walisema hivyo kwa sababu hawakuthubutu kumwuliza tena maswali mengine.
41 And he said to them, How do they say the Christ is David's son?
Yesu akawauliza, “Yasemekanaje kwamba Kristo ni mwana wa Daudi?
42 Even David himself says in the book of Psalms, The Lord said to my Lord, Sit thou at my right hand,
Maana Daudi mwenyewe anasema katika Zaburi: Bwana alimwambia Bwana wangu: Keti upande wangu wa kulia
43 until I will place thine enemies a footstool of thy feet.
mpaka niwafanye adui zako kama kiti cha kuwekea miguu yako.
44 David therefore calls him Lord, and how is he his son?
Ikiwa Daudi anamwita yeye, Bwana, basi atakuwaje mwanawe?”
45 And while all the people were listening, he said to his disciples,
Yesu aliwaambia wanafunzi wake mbele ya watu wote,
46 Beware of the scholars, who desire to walk around in long robes, and love greetings in the marketplaces, and chief seats in the synagogues, and places of honor at the feasts,
“Jihadharini na walimu wa Sheria ambao hupenda kupitapita wamevalia kanzu. Hupenda kusalimiwa na watu kwa heshima masokoni, huketi mahali pa heshima katika masunagogi na kuchukua nafasi za heshima katika karamu.
47 who devour widows' houses, and in pretence make long prayers. These will receive greater damnation.
Huwadhulumu wajane huku wakisingizia kuwa wema kwa kusali sala ndefu. Hao watapata hukumu kali zaidi!”