< Leviticus 10 >

1 And Nadab and Abihu, the sons of Aaron, each of them took his censer, and put fire in it, and laid incense on it, and offered strange fire before Jehovah, which he had not commanded them.
Nadabu na Abihu, wana wa Aroni, wakachukua vyetezo vyao, wakaweka moto ndani yake na kuongeza uvumba; kisha wakamtolea Bwana moto usio halali, kinyume na agizo la Mungu.
2 And there came forth fire from before Jehovah, and devoured them, and they died before Jehovah.
Hivyo moto ukaja kutoka kwa uwepo wa Bwana na kuwaramba, nao wakafa mbele za Bwana.
3 Then Moses said to Aaron, This is it that Jehovah spoke, saying, I will be sanctified in those who come near me. And I will be glorified before all the people. And Aaron remained silent.
Kisha Mose akamwambia Aroni, “Hili ndilo alilonena Bwana wakati aliposema: “‘Miongoni mwa wale watakaonikaribia nitajionyesha kuwa mtakatifu; machoni pa watu wote nitaheshimiwa.’” Aroni akanyamaza.
4 And Moses called Mishael and Elzaphan, the sons of Uzziel the uncle of Aaron, and said to them, Draw near. Carry your brothers from before the sanctuary out of the camp.
Mose akawaita Mishaeli na Elisafani, wana wa Uzieli mjomba wake Aroni, akawaambia, “Njooni hapa. Ondoeni miili ya binamu zenu mbele ya mahali patakatifu, mkaipeleke nje ya kambi.”
5 So they drew near, and carried them in their tunics out of the camp, as Moses had said.
Hivyo wakaja na kuwaondoa, wakiwa bado wamevalia makoti yao ya ibada, wakawapeleka nje ya kambi, kama Mose alivyoamuru.
6 And Moses said to Aaron, and to Eleazar and to Ithamar, his sons, Let not the hair of your heads go loose, neither tear your clothes, that ye not die, and that he not be angry with all the congregation, but let your brothers, the whole house of Israel, bewail the burning which Jehovah has kindled.
Ndipo Mose akamwambia Aroni pamoja na wanawe, Eleazari na Ithamari, “Msifunue vichwa vyenu wala msirarue mavazi yenu, la sivyo mtakufa na Bwana ataikasirikia jumuiya nzima. Lakini ndugu zenu, nyumba yote ya Israeli, wanaweza kuwaombolezea wale ambao Bwana amewaangamiza kwa moto.
7 And ye shall not go out from the door of the tent of meeting, lest ye die, for the anointing oil of Jehovah is upon you. And they did according to the word of Moses.
Msitoke nje ya ingilio la Hema la Kukutania, la sivyo mtakufa, kwa sababu mafuta ya Bwana ya upako yako juu yenu.” Hivyo wakafanya kama vile Mose alivyosema.
8 And Jehovah spoke to Aaron, saying,
Kisha Bwana akamwambia Aroni,
9 Drink no wine nor strong drink, thou, nor thy sons with thee, when ye go into the tent of meeting, that ye not die-it shall be a statute forever throughout your generations-
“Wewe na wanao msinywe mvinyo wala kinywaji kingine kilichochachuka wakati mwingiapo katika Hema la Kukutania, la sivyo mtakufa. Hili litakuwa Agizo la kudumu kwa vizazi vijavyo.
10 and that ye may make a distinction between the holy and the common, and between the unclean and the clean,
Ni lazima mtenganishe kilicho kitakatifu na kile kilicho cha kawaida, kati ya yaliyo najisi na yaliyo safi,
11 and that ye may teach the sons of Israel all the statutes which Jehovah has spoken to them by Moses.
na lazima mwafundishe Waisraeli amri zote ambazo Bwana aliwapa kupitia Mose.”
12 And Moses spoke to Aaron, and to Eleazar and to Ithamar, his sons who were left, Take the meal offering that remains of the offerings of Jehovah made by fire, and eat it without leaven beside the altar, for it is most holy.
Mose akamwambia Aroni pamoja na wanawe waliosalia, Eleazari na Ithamari, “Chukueni sadaka ya nafaka iliyobaki kutoka sadaka zilizotolewa kwa Bwana kwa moto, muile hapo kando ya madhabahu ikiwa imeandaliwa bila chachu, kwa sababu ni takatifu sana.
13 And ye shall eat it in a holy place, because it is thy portion, and thy sons' portion, of the offerings of Jehovah made by fire. For so I am commanded.
Mtaila katika mahali patakatifu kwa sababu ni fungu lenu na fungu la wana wenu la sadaka zilizotolewa kwa Bwana kwa moto, kwa maana hivyo ndivyo nilivyoamriwa.
14 And ye shall eat the wave-breast and the heave-thigh in a clean place, thou, and thy sons, and thy daughters with thee. For they are given as thy portion, and thy sons' portion, out of the sacrifices of the peace offerings of the sons of Israel.
Lakini wewe na wanao na binti zako mwaweza kula kidari kile kilichoinuliwa na paja lile lililotolewa. Mtavila mahali safi pa kawaida ya ibada; mmepewa wewe na watoto wako kuwa fungu lenu la sadaka za amani za Waisraeli.
15 They shall bring the heave-thigh and the wave-breast with the offerings made by fire of the fat, to wave it for a wave offering before Jehovah, and it shall be thine, and thy sons' with thee, as a portion forever, as Jehovah has commanded.
Paja lile lililotolewa na kidari kile kilichoinuliwa lazima viletwe pamoja na sehemu za mafuta ya sadaka za kuteketezwa kwa moto, ili kuinuliwa mbele za Bwana kama sadaka ya kuinuliwa. Hili litakuwa fungu lako la kawaida na wanao, kama Bwana alivyoagiza.”
16 And Moses diligently sought the goat of the sin offering, and, behold, it was burnt. And he was angry with Eleazar and with Ithamar, the sons of Aaron who were left, saying,
Mose alipouliza kuhusu mbuzi atolewaye kwa ajili ya sadaka ya dhambi, na kukuta kwamba ameteketezwa, aliwakasirikia Eleazari na Ithamari, wana wa Aroni waliobaki, akawauliza,
17 Why have ye not eaten the sin offering in the place of the sanctuary, seeing it is most holy, and he has given it to you to bear the iniquity of the congregation, to make atonement for them before Jehovah?
“Kwa nini hamkula sadaka ya dhambi katika eneo la mahali patakatifu? Ni takatifu sana. Mlipewa ninyi ili kuondoa hatia ya jumuiya kwa ajili ya kuwafanyia upatanisho mbele za Bwana.
18 Behold, the blood of it was not brought into the sanctuary inside. Ye should certainly have eaten it in the sanctuary, as I commanded.
Kwa kuwa damu yake haikuletwa ndani ya Mahali Patakatifu, mngemla mbuzi huyo katika sehemu ya mahali patakatifu kama nilivyoagiza.”
19 And Aaron spoke to Moses, Behold, this day they have offered their sin offering and their burnt offering before Jehovah, and there have befallen me such things as these. And if I had eaten the sin offering today, would it have been well-pleasing in the sight of Jehovah?
Aroni akamjibu Mose, “Leo wanangu wametoa sadaka zao za dhambi na sadaka zao za kuteketezwa mbele za Bwana, lakini mambo kama haya yamenitokea mimi. Je, Bwana angependezwa kama ningekuwa nimekula sadaka ya dhambi leo?”
20 And when Moses heard, it was well-pleasing in his sight.
Mose aliposikia haya, akaridhika.

< Leviticus 10 >