< John 16 >

1 I have spoken these things to you, so that ye may not be caused to stumble.
“Nimewaambia mambo haya yote ili msije mkaiacha imani.
2 They will make you excommunicated from the synagogues. But the hour comes that every man who kills you will presume to be offering service to God.
Watawatenga na masinagogi. Naam, saa yaja ambayo mtu yeyote atakayewaua atadhani kwa kufanya hivyo anamtumikia Mungu.
3 And they will do these things, because they have not known the Father nor me.
Nao watawatenda haya kwa sababu hawamjui Baba wala mimi.
4 But I have told you these things, so that when the hour comes, ye may remember that I told you of them. But I did not tell you these things from the beginning because I was with you.
Lakini nimewaambia ninyi mambo haya, ili saa hiyo ikiwadia mpate kukumbuka ya kuwa nilikuwa nimewaambia. Sikuwaambia mambo haya tangu mwanzo kwa sababu nilikuwa pamoja nanyi.
5 But now I go to him who sent me, and none of you asks me, Where do thou go?
“Sasa mimi ninakwenda kwake yeye aliyenituma, lakini hakuna hata aniulizaye, ‘Unakwenda wapi?’
6 But because I have spoken these things to you, sorrow has filled your heart.
Kwa sababu nimewaambia mambo haya, mioyo yenu imejawa na huzuni.
7 Nevertheless I tell you the truth, it is expedient for you that I depart, for if I do not depart, the helper will not come to you. But whenever I go, I will send him to you.
Lakini nawaambia kweli, yafaa mimi niondoke, kwa kuwa nisipoondoka, huyo Msaidizi hatakuja kwenu, lakini nikienda nitamtuma kwenu.
8 And having come, that will convict the world about sin, and about justice, and about judgment.
Naye atakapokuja, atauthibitishia ulimwengu kuhusu dhambi, haki na hukumu.
9 About sin because they truly did not believe in me,
Kwa habari ya dhambi, kwa sababu hawaniamini mimi,
10 and about justice because I go to the Father, and ye see me no more,
kwa habari ya haki, kwa sababu ninakwenda kwa Baba, nanyi hamtaniona tena,
11 and about judgment because the ruler of this world has been judged.
kwa habari ya hukumu, kwa sababu yule mkuu wa ulimwengu huu amekwisha kuhukumiwa.
12 I have yet many things to say to you, but ye cannot bear them now.
“Bado ninayo mambo mengi ya kuwaambia, lakini hamwezi kuyastahimili sasa.
13 However when that, the Spirit of truth, comes, he will guide you into all the truth. For he will not speak from himself, but as many things as he may hear, he will speak. And he will report to you the things that are coming.
Atakapokuja huyo Roho wa kweli atawaongoza awatie katika kweli yote. Yeye hatanena kwa ajili yake mwenyewe, bali atanena yale yote atakayosikia, naye atawaonyesha mambo yajayo.
14 He will glorify me because he will receive from me, and will report to you.
Atanitukuza mimi, kwa maana atayachukua yaliyo yangu na kuwajulisha ninyi.
15 All things, as many as the Father has are mine. Because of this I said that he takes from me, and will report to you.
Vyote alivyo navyo Baba ni vyangu. Ndiyo maana nimesema Roho atachukua yaliyo yangu na kuwajulisha ninyi.
16 A little while, and ye do not see me. Again a little while, and ye will look at me, because I go to the Father.
“Bado kitambo kidogo nanyi hamtaniona na tena bado kitambo kidogo nanyi mtaniona.”
17 Therefore some of his disciples said among themselves, What is this that he says to us, A little while, and ye do not see me, and, Again a little while, and ye will look at me, and, Because I go to the Father?
Baadhi ya wanafunzi wakaulizana, “Ana maana gani asemapo, ‘Bado kitambo kidogo nanyi hamtaniona na tena bado kitambo kidogo nanyi mtaniona’? Naye ana maana gani asemapo, ‘Kwa sababu ninakwenda kwa Baba’?”
18 They said therefore What is this that he says, A little while? We know not what he says.
Wakaendelea kuulizana, “Ana maana gani asemapo, ‘Kitambo kidogo’? Hatuelewi hilo analosema.”
19 Therefore Jesus knew that they wanted to ask him, and he said to them, Do ye inquire among yourselves about this, because I said, A little while, and ye do not see me, and, Again a little while, and ye will look at me?
Yesu akatambua kuwa walitaka kumuuliza juu ya hilo, hivyo akawaambia, “Je, mnaulizana nina maana gani niliposema, ‘Bado kitambo kidogo nanyi hamtaniona na tena bado kitambo kidogo nanyi mtaniona’?
20 Truly, truly, I say to you, that ye will weep and lament, but the world will rejoice. Ye will be sorrowful, but your sorrow will become into joy.
Amin, amin nawaambia, ninyi mtalia na kuomboleza, lakini ulimwengu utafurahi. Ninyi mtahuzunika, lakini huzuni yenu itageuka kuwa furaha.
21 When a woman brings forth she has pain because her hour has come. But when she has given birth to the child she no longer remembers the anguish because of the joy that a man was born into the world.
Mwanamke anapokuwa na utungu wa kuzaa huwa na maumivu kwa sababu saa yake imewadia. Lakini mtoto akiisha kuzaliwa, yule mwanamke husahau maumivu hayo kwa sababu ya furaha ya kuzaliwa mtoto ulimwenguni.
22 And now therefore indeed ye have sorrow, but I will see you again, and your heart will rejoice, and no man takes your joy away from you.
Hivyo ninyi mna maumivu sasa, lakini nitawaona tena, nayo mioyo yenu itafurahi na furaha yenu hakuna awaondoleaye.
23 And in that day ye will ask me nothing. Truly, truly, I say to you, that as many things as ye may ask the Father in my name, he will give you.
Katika siku hiyo hamtaniuliza neno lolote. Amin, amin nawaambia, kama mkimwomba Baba jambo lolote kwa jina langu, yeye atawapa.
24 Until now ye have asked nothing in my name. Ask, and ye will receive, so that your joy may be made full.
Mpaka sasa hamjaomba jambo lolote kwa Jina langu. Ombeni nanyi mtapewa, ili furaha yenu ipate kuwa kamili.
25 These things I have spoken to you in veiled words. The hour comes, when I will no more speak to you in veiled words, but will inform you plainly about the Father.
“Nimewaambia mambo haya kwa mafumbo. Saa yaja ambapo sitazungumza nanyi tena kwa mafumbo bali nitawaeleza waziwazi kuhusu Baba.
26 In that day ye will ask in my name, and I do not say to you, that I will pray the Father about you,
Siku hiyo mtaomba kwa Jina langu. Wala sitawaambia kwamba nitamwomba Baba kwa ajili yenu,
27 for the Father himself loves you, because ye have loved me, and have believed that I came forth from God.
kwa maana Baba mwenyewe anawapenda, kwa sababu mmenipenda mimi na mmeamini kwamba nimetoka kwa Mungu.
28 I came forth from the Father, and have come into the world. Again I leave the world, and go to the Father.
Nilitoka kwa Baba na kuja ulimwenguni, sasa naondoka ulimwenguni na kurudi kwa Baba.”
29 His disciples say to him, Lo, now thou speak plainly, and speak not one veiled word.
Ndipo wanafunzi wake wakasema, “Sasa unazungumza waziwazi, wala si kwa mafumbo.
30 Now we know that thou know all things, and have no need that any man should question thee. By this we believe that thou came forth from God.
Sasa tumejua kwamba wewe unajua mambo yote, wala hakuna haja ya mtu kukuuliza maswali. Kwa jambo hili tunaamini kwamba ulitoka kwa Mungu.”
31 Jesus answered them, Do ye now believe?
Yesu akawajibu, “Je, sasa mnaamini?
32 Behold, the hour comes, and now has come, that ye will be scattered, each man to his own things, and ye will leave me alone. And yet I am not alone, because the Father is with me.
Saa inakuja, naam, imekwisha kuwadia, mtakapotawanyika kila mmoja kwenda nyumbani kwake na kuniacha peke yangu. Lakini mimi siko peke yangu kwa sababu Baba yu pamoja nami.
33 These things I have spoken to you, so that in me ye might have peace. In the world ye have tribulation. But cheer up, I have overcome the world.
Nimewaambia mambo haya, ili mpate kuwa na amani mkiwa ndani yangu. Ulimwenguni mtapata dhiki. Lakini jipeni moyo, kwa maana mimi nimeushinda ulimwengu.”

< John 16 >